Salaam toka kwa Baba Mtarajiwa..

ELNIN0

JF-Expert Member
Nov 26, 2009
4,161
1,460
Wakubwa,

Mimi ni baba mtarajiwa ambapo mungu akijalia mwezi ujao basi na mimi naanza kuitwa baba au Dingi / Mshua kwa lugha za kisasa.

Kati ya mambo mengi niliyopanga kumfanyia mwanangu mtarajiwa ambayo yana kipaumbele cha pekee ni malezi bora including elimu na akiba yake ya baadae.

Suala geni kidogo kwa wazazi wengi huwa ni kutotunza kumbukumbu za watoto wao, mimi ningefurahi sana kama wazazi wangu wangekuwa wamenitunzia vitu vifuatavyo
a) Kazi zangu za darasani tangu chekechea hadi darasa la saba
b) Baadhi ya mavazi yangu from 0 age mpaka 12
c) Picha zangu nyingi nyingi za utoto katika matukio tofauti.

Lakini wakubwa mimi nina picha moja tu nikiwa 12 age. kwa maana hiyo nimeamua kufanya yafuatayo kwa mwanangu mtarajiwa ili asipate matatizo kama yangu.

a) Kutunza kumbukubu za maisha yake ya utoto - Picha na Video from 0 age hadi 14
b) Kutunza mavazi yake yote ya utoto toka 0 age hadi 14
c) Kutunza kazi zake za darasani toka 3 years hadi std 7, na kumsaidia kuzitunza hata zile za form one hadi four.

Nimeamua kufanya hivi sababu wazazi wengi hawajali sana suala la kumbukumbu lakini ki ukweli linasaidia mtoto kujua ametokea wapi, makuzi yalikuwaje na ni vipi wazazi mlichangia malezi yake.

Ni mimi Baba Mtarajiwa - naomba sara zenu mambo yawe swafi niitwe baba kama baadhi yenu humu.
 
Utaitwa Baba na Mungu atalisimamia hilo. Kila la kheri Elnino
 
Baba mtarajiwa, muhimu pia kushirikiana na mama mtarajiwa ktk malezi kama kukesha usiku na mtoto,kumlisha akifikia wakati huu,kumpeleka clinic nk.
kumbukumbu ni kitu kizuri sana, usafishe picha na ziwe kwenye album hiyo ndiyo raha siyo digital tu..

Maandalizi mema ya malezi,you will be a great dad kwa unavyoonesha kimaandishi!..
 
Tengeneza baby book....piga picha ya ujauzito wa mama, mtoto akizaliwa bandika footprints zake kwenye baby book, na document kila hatua ya mwanao...atakapoanza kutambaa, kutembea, n.k.
 
All the best Elnino !! Kuhifadhi kumbukumbu ni muhimu sana katika maisha... Nakutakia kila la kheri na Mungu
atakuongoza katika ujio wa mwanao ile uwe wa salama na afya njema. Be blessed n hope you will be a great DAD !!
 
Wakubwa,

Mimi ni baba mtarajiwa ambapo mungu akijalia mwezi ujao basi na mimi naanza kuitwa baba au Dingi / Mshua kwa lugha za kisasa.

Kati ya mambo mengi niliyopanga kumfanyia mwanangu mtarajiwa ambayo yana kipaumbele cha pekee ni malezi bora including elimu na akiba yake ya baadae.

Suala geni kidogo kwa wazazi wengi huwa ni kutotunza kumbukumbu za watoto wao, mimi ningefurahi sana kama wazazi wangu wangekuwa wamenitunzia vitu vifuatavyo
a) Kazi zangu za darasani tangu chekechea hadi darasa la saba
b) Baadhi ya mavazi yangu from 0 age mpaka 12
c) Picha zangu nyingi nyingi za utoto katika matukio tofauti.

Lakini wakubwa mimi nina picha moja tu nikiwa 12 age. kwa maana hiyo nimeamua kufanya yafuatayo kwa mwanangu mtarajiwa ili asipate matatizo kama yangu.

a) Kutunza kumbukubu za maisha yake ya utoto - Picha na Video from 0 age hadi 14
b) Kutunza mavazi yake yote ya utoto toka 0 age hadi 14
c) Kutunza kazi zake za darasani toka 3 years hadi std 7, na kumsaidia kuzitunza hata zile za form one hadi four.

Nimeamua kufanya hivi sababu wazazi wengi hawajali sana suala la kumbukumbu lakini ki ukweli linasaidia mtoto kujua ametokea wapi, makuzi yalikuwaje na ni vipi wazazi mlichangia malezi yake.

Ni mimi Baba Mtarajiwa - naomba sara zenu mambo yawe swafi niitwe baba kama baadhi yenu humu.
Hongera kwa kutegemea kupata mtoto na Mungu atakuvusha katika hili.
 
Back
Top Bottom