Ukombozi Sasa
Member
- Nov 5, 2010
- 17
- 10
Ndugu zangu watanzania, hali inazidi kuwa tete, maisha yetu yamejeuka usanii mtupu. Kila kukicha ya jana nafuu, yakesho ndiyo itakuwa mbaya zaidi. Mkwere kazi kucheka tu,maisha yetu kwake ni kama mchezo fulani wa kuigiza. Je tunaweza kuwa na sala ya kitaifa ya kuomba uongozi wa nchi ubadilike kabla ya 2015. Miaka mingine minne na nusu ya kwake itakuwa inatutesa sana, kwa mfano kuanzia January mwaka huu tumekuwa na maisha ya kusua sua, hali tete ya Arusha, Mgawo wa Umeme, Viwanda kufungwa na watu kupoteza ajira kwa ajili ya mgao wa umeme, wanafunzi wa kidato cha nne kufeli, Mfumuko wa Bei ya bidhaa muhimu, Polisi kupiga wanafunzi wa vyuo vikuu na kuwarushia mabomu na hatimaye sasa Gongo la Mboto. Ndugu watanzania tumekwisha, kama ya Misri hayawezekani, basi tufanye Sala ya Kitaifa kumuombea huyu KIKWETE aachie nchi kwa namna yeyote, mpaka 2015 naona kama mbali sana vile, tutakuwa tumekwisha. Tupange siku kama inavyokuwa mwaka mpya, Taifa Zima, lipige sala kila mtu katika imani yake ili huyu Mkwere, atuachie nchi yetu kabla haijaharibika zaidi. Labda itasaidia! Je unaweza kumuombea adu yako afe?