Sala ya kumuombea kikwete

Ukombozi Sasa

Member
Nov 5, 2010
17
10
Ndugu zangu watanzania, hali inazidi kuwa tete, maisha yetu yamejeuka usanii mtupu. Kila kukicha ya jana nafuu, yakesho ndiyo itakuwa mbaya zaidi. Mkwere kazi kucheka tu,maisha yetu kwake ni kama mchezo fulani wa kuigiza. Je tunaweza kuwa na sala ya kitaifa ya kuomba uongozi wa nchi ubadilike kabla ya 2015. Miaka mingine minne na nusu ya kwake itakuwa inatutesa sana, kwa mfano kuanzia January mwaka huu tumekuwa na maisha ya kusua sua, hali tete ya Arusha, Mgawo wa Umeme, Viwanda kufungwa na watu kupoteza ajira kwa ajili ya mgao wa umeme, wanafunzi wa kidato cha nne kufeli, Mfumuko wa Bei ya bidhaa muhimu, Polisi kupiga wanafunzi wa vyuo vikuu na kuwarushia mabomu na hatimaye sasa Gongo la Mboto. Ndugu watanzania tumekwisha, kama ya Misri hayawezekani, basi tufanye Sala ya Kitaifa kumuombea huyu KIKWETE aachie nchi kwa namna yeyote, mpaka 2015 naona kama mbali sana vile, tutakuwa tumekwisha. Tupange siku kama inavyokuwa mwaka mpya, Taifa Zima, lipige sala kila mtu katika imani yake ili huyu Mkwere, atuachie nchi yetu kabla haijaharibika zaidi. Labda itasaidia! Je unaweza kumuombea adu yako afe?
 
Kwa sasa kama nataka kuamini kuwa Jamiiforums itakuwa ndio muunganiko mzuri wa tanzania kuanzisha move....... LET US PRAY FOR THAT.
 


WANANCHI HATUKO SALAMA TENA WALA MALI ZETU, KIIO KILA LEO NA MAYATIMA KUONGEZEKA: KWA HILI SERIKALI NZIMA IJIUZULU HATA KABLA YA MAANDAMANO
YA KUTETEA 'UHAI WA WENZETU' KUANZA KOTE NCHINI


Mheshimiwa Kikwete kama amiri jeshi mkuu ajiuzulu pamoja na serikali yake.

Yalianza na vifo vya raia kule (1) Pemba, baadaye (2) Unguja, Kisha (3) Mbagala, nako Arusha Mjini, (4) mauaji ya wakulima kule Mashamba ya mpunga kule Mabuki Mbeya na sasa (5) Gongolamboto.

Ajabu ni kwamba licha ya wananchi wengi kuuaua na mali zao kuteketea, hakuna hata mtu mmoja aliyewahi kuwajibika wala kuwajibishwa serikalini. Kote ni kiburi na jeuri tu mbe ya kupotea uhai wa mtu na watoto kubaki miyatima!!!

Jukumu la msingi halijazingatiwa; kuna watu wanasinzia kwenye majukumu nyeti na sasa kutugharimu kiasi hini, wananchi hatuko salama!! Tusianze kuzungusha kiswahili hapa ni uhai umepotea kwa uzembe!!! Hawa mayatima wanahitaji sauti zetu!!

Hatutaki tena tume kwani hata kule Mbagala chombo kama hicho hakikutusaidia zaidi ya kuwapa wanasiasa na makampuni ya kibiashara kujinadi kwenye kioo cha televisheni mgongoni mwa msiba na damu kwa wengine.

Jukumu la kwanza la kuhitajika uwepo wa serikali katikati yetu NI KUHAKIKISHA USALAMA KILA MMOJA WETU NA MALI ZETU. Kwa mtaji hizi picha nilizoona, serikali nzima ya CCM ijiuzulu mara moja

Mauaji Arusha walitupuuza kana kwamba kuliuaua nzi tu. Kule kwenye mashamba ya mpunga wala hawakujishughulisha kitu kuwajibika mtu. Sasa kama kweli kuna JAMBO AMBALO KIUKWELI KABISA KINATUHITAJI KUANDAMANA MPAKA KUELEWEKE NI KATIKA KUTETEA UHAI WA WENZETU.

Kama tutaona vifo hivi kama vile ni ya 'akina wale' na kwamba sisi wengine hatuhusiki basi hapo ndipo kiama chetu kinapoanzia. Kwa vifo hivi vyote 17 taifa tumepata yatima wangapiii?????????????


Gongo1.jpg


Gongo2.jpg

_51307856_munition_ap.jpg

_51307454_bus_ap.jpg

Debris and arms were hurled across the Tanzanian of city of Dar es Salaam on Wednesday night after an accident triggered a series of explosions at Gongola Mboto military base.
_51310264_lostchildren_ap.jpg
Tanzania's Red Cross says about 200 children who lost their parents during the confusion of the blasts are being cared for at the city's stadium.

_51312030_cherehani.jpg



attachment.php
 
Mungu Ibariki Tanzania, walaani viongozi wake.hekima, umoja na amani zidumu,mafisadi wachomwe jehanamu,hela za watanzania zinazoliwa zirejeshwe, wanajeshi wanaolala uwachukue moja kwa moja dunia hawana faida tena,wameshindwa kukagua silaha zao na kuzihamishaa mbali na makazi ya watu,ona watu wanavoteseka wkt mkwere anaona afadhali nguo za jeshi hazikuharibika,kweli Tumekwisha.nawapa pole wahanga wote hasa kina mama na watoto.
 
Back
Top Bottom