Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Wiki chacha zilizopita nilianzisha uzi hapa JF wa kuahirishwa kwa uchaguzi wa kijiji cha Mwanzo Mgumu, kata ya Msimbu wilayani kisarawe Mkoa wa Pwani ( Nyumbani kwa Baba Riz 1) kutokana na 'mabaunsa' wasiofahamika kuvamia chumba cha kuhesabia kura na kutokomea na masanduku yote yaliyohesabiwa kura na yasiyohesabiwa kura. Vile vile nikasema kuwa wakati huo Chadema walikuwa na zaidi ya kura 100 zilizohesabiwa huku CCM ikiwa na kura zaidi ya 20.
Nikasema kuwa Uongozi wa wilaya haukuweza kumchukulia hatua mtu yo yote pamoja na wananchi kuwataja wahusika siku chache baada ya tukio hilo. Nikawapa Changamoto waandishi wa habari watupe undani wa habari ile na kuziweka magazetini.
Habari ile ilileta ubishi mkubwa sana hapa JF wengine wakisema Aweda anafanya proganda za Chadema dhidi ya CCM.
Hata hivyo, leo naomba kuleta taarifa rasmi kwamba Chadema wameshinda uchaguzi huo uliorudiwa na kufanikiwa kuitwaa serikali ya kijiji kwa mara ya kwanza ktk wilaya ya Kisarawe (mkoa wa pwani, Ngome ya Baba Riz 1, to the best of my knowledge).
Huu ni ushidni wa nguvu ya umma kwa sababu serikali ilifanya juhudi kubwa kuwatisha wananchi ili wabadilishe maamuzi yao kumchagua mtu wasiyemtaka, lakini wananchi waligoma kufanya hivyo, uongozi wa wilaya ukafyata mkia na kukubaliana na matakwa ya wananchi bila ridhaa yao.
Uchaguzi ulifanyika tarehe 10 mwezi huu
Kura zilizopatikana baada ya nguvu kubwa kutumika kuwashawishi na kuwalazimisha wananchi wabadilike bila mafanikio ni kama ifuatavyo;
Chadema - Saidi Selemani Mulugendi 148
CCM - Jabiri Nasoro Kibiriti 141
zilizoharibika 13.
Waliokuwa wanasema kuwa nafanya propaganda dhidi ya CCM sasa kubalini kwamba nilikuwa na sema kweli.
Naona CD ya ccm ya Ukabila imepotea, ya Ukanda imepoteza wateja na sasa ya udini nayo imeanza kuchuja (Mwanzo mgumu Msimbu wakristo 5%).. Je, ni CD gani sasa itazinduliwa na ccm? ya Chama cha vurugu? Kazi kwao. Mimi sipo.
Nikasema kuwa Uongozi wa wilaya haukuweza kumchukulia hatua mtu yo yote pamoja na wananchi kuwataja wahusika siku chache baada ya tukio hilo. Nikawapa Changamoto waandishi wa habari watupe undani wa habari ile na kuziweka magazetini.
Habari ile ilileta ubishi mkubwa sana hapa JF wengine wakisema Aweda anafanya proganda za Chadema dhidi ya CCM.
Hata hivyo, leo naomba kuleta taarifa rasmi kwamba Chadema wameshinda uchaguzi huo uliorudiwa na kufanikiwa kuitwaa serikali ya kijiji kwa mara ya kwanza ktk wilaya ya Kisarawe (mkoa wa pwani, Ngome ya Baba Riz 1, to the best of my knowledge).
Huu ni ushidni wa nguvu ya umma kwa sababu serikali ilifanya juhudi kubwa kuwatisha wananchi ili wabadilishe maamuzi yao kumchagua mtu wasiyemtaka, lakini wananchi waligoma kufanya hivyo, uongozi wa wilaya ukafyata mkia na kukubaliana na matakwa ya wananchi bila ridhaa yao.
Uchaguzi ulifanyika tarehe 10 mwezi huu
Kura zilizopatikana baada ya nguvu kubwa kutumika kuwashawishi na kuwalazimisha wananchi wabadilike bila mafanikio ni kama ifuatavyo;
Chadema - Saidi Selemani Mulugendi 148
CCM - Jabiri Nasoro Kibiriti 141
zilizoharibika 13.
Waliokuwa wanasema kuwa nafanya propaganda dhidi ya CCM sasa kubalini kwamba nilikuwa na sema kweli.
Naona CD ya ccm ya Ukabila imepotea, ya Ukanda imepoteza wateja na sasa ya udini nayo imeanza kuchuja (Mwanzo mgumu Msimbu wakristo 5%).. Je, ni CD gani sasa itazinduliwa na ccm? ya Chama cha vurugu? Kazi kwao. Mimi sipo.