Kwa mara nyingine tena mhimili wa Mahakama unajikuta katika mtihani mwingine dhidi ya serikali na wananchi baada ya serikali kukimbilia mahakamani katika sakata la mgomo wa walimu.
Masikio ya watanzania wengi yana shauku kubwa ya kusikia kauli ya mahakama juu ya mgomo huu. Huku zikisikika kauli mbalimbali kutoka kwa viongozi wa serikali na bunge zikiashiria kuwa viongozi hawa wanajua tamko la mahakama lijalo! Ni manabii hawa! N/Spika amesema leo bungeni kuwa suala la mgomo wa walimu liko mahakamani na tunasubiri tamko la mahakama na kwenda mbali zaidi kuwa mahakama itatoa tamko lake kesho saa nane mchana! Huku NW Elimu Mh. Mlugo akisisitiza kuwa haitapita siku mbili mahakama haijatoa tamko lake?
Wakati viongozi wa serikali na bunge wakisema hayo naibu katibu mkuu wa CWT Mwl Oluochi anadai mgomo uko palepale kwa kuwa uko umefuata taratibu zote za kisheria na mahakama haitamtaarifu chochote juu ya tamko lake. Hili ni jambo jingine linalohitaji mjadala mpana. Mhimili wa mahakama una options mbili tu kuhusu reputation yake kutokana na kauli yake juu ya hili.
1. Mahakama isubiri kuheshimiwa na serikali kwa kuiokoa kudhalilishwa na walimu kama ilivyofanya wiki chache zilizopita kwa madaktari. Ikitaka kupongezwa na serikali tamko ni wazi "WALIMU WARUDI KAZINI MGOMO WAO NI BATILI" na hivyo walimu watarudi mashuleni (sio darasani) na kuacha serikali ikichekelea bila kujali kama wataenda kufundisha au la! bila kujali mahakama imetenda haki au la! Hayo hayaihusu serikali yetu kabisaaaaaa!
2. Mahakama pia inaweza kusubiri kuheshimiwa na wananchi na jamii kwa ujumla kwa kusimamia haki bila kujali kama swahiba wake serikali yuko upande wa kupoteza au wa kupata. Haki mbele.
Ni maoni yangu tu asije akanisikia Ramadhani Ighondu wa TISS!
Nawasilisha.
Masikio ya watanzania wengi yana shauku kubwa ya kusikia kauli ya mahakama juu ya mgomo huu. Huku zikisikika kauli mbalimbali kutoka kwa viongozi wa serikali na bunge zikiashiria kuwa viongozi hawa wanajua tamko la mahakama lijalo! Ni manabii hawa! N/Spika amesema leo bungeni kuwa suala la mgomo wa walimu liko mahakamani na tunasubiri tamko la mahakama na kwenda mbali zaidi kuwa mahakama itatoa tamko lake kesho saa nane mchana! Huku NW Elimu Mh. Mlugo akisisitiza kuwa haitapita siku mbili mahakama haijatoa tamko lake?
Wakati viongozi wa serikali na bunge wakisema hayo naibu katibu mkuu wa CWT Mwl Oluochi anadai mgomo uko palepale kwa kuwa uko umefuata taratibu zote za kisheria na mahakama haitamtaarifu chochote juu ya tamko lake. Hili ni jambo jingine linalohitaji mjadala mpana. Mhimili wa mahakama una options mbili tu kuhusu reputation yake kutokana na kauli yake juu ya hili.
1. Mahakama isubiri kuheshimiwa na serikali kwa kuiokoa kudhalilishwa na walimu kama ilivyofanya wiki chache zilizopita kwa madaktari. Ikitaka kupongezwa na serikali tamko ni wazi "WALIMU WARUDI KAZINI MGOMO WAO NI BATILI" na hivyo walimu watarudi mashuleni (sio darasani) na kuacha serikali ikichekelea bila kujali kama wataenda kufundisha au la! bila kujali mahakama imetenda haki au la! Hayo hayaihusu serikali yetu kabisaaaaaa!
2. Mahakama pia inaweza kusubiri kuheshimiwa na wananchi na jamii kwa ujumla kwa kusimamia haki bila kujali kama swahiba wake serikali yuko upande wa kupoteza au wa kupata. Haki mbele.
Ni maoni yangu tu asije akanisikia Ramadhani Ighondu wa TISS!
Nawasilisha.