nderingosha
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 4,281
- 3,243
Nimefatilia mijadala/kelele za wabunge zinazodai baadhi ya mawaziri wenye matatizo watimuliwe upesi kazi
baadhi ya mawaziri hawa ni:waziri wa fedha, waziri wa biashara na naibu wake,waziri wa tamisemi na waziri wa afya. ..Kinachonishangaza ni kutosikia kelele dhidi ya mawaziri wengine wa wizara ambazo zimekuwa zikipigiwa kelele kwa muda mrefu sasa
mfano: wizara ya ulinzi,wizara ya nishati na madini, wizara ya mambo ya ndani na wizara ya mali asili na utalii na hata wizara ya elimu
.Nasema hivi nikikumbuka kuwa wizara ya ulinzi imekumbwa na uzembe mkubwa
..rejea mauaji ya mabomu mbagala na gongo la mboto
.na hata ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma
rejea malipo hewa ya askari nje etc etc..lakini leo waziri bado yuko kibaruani na mambo yameshasahaulika
.Tukija wizara ya nishati na madini ni hivi majuzi tu iliundiwa tume na kudhihirika kuwa na ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma
.refer sakata la Jairo
..na pia wizara hii imekuwa na ubadhirifu mkubwa kwenye TANESCO
.IPTL
ununuzi wa mafuta
..umeme wa dharura
dowans saga
etc etc
.nashangaa leo mawaziri wa wizara hii
akina Ngeleja na Malima hawapigiwi kelele
Tukija wizara ya mambo ya ndani
..rejea mauaji ya raia wasio na hatia songea
.kauli tata za waziri dhidi ya madai ya Dr.Mwakyembe na hatma ya uchunguzi wa suala lake
mauaji ya Arusha
etc etc
..leo sisikii kelele dhidi ya waziri wa wizara hii
Tukija wizara ya malia asili na utalii
..rejea sakata la vitalu
..wizi wa wanyama pori kule KIA..na hata mtuhumiwa mkuu kutoroka nchini etc etc
..nashangaa leo waziri wa wizara hii hapigiwi kelele
.na mwisho wizara ya elimu
.rejea wizi wa hela za mikopo vyuo vikuu
hiki ni kilio cha kila siku lakini waziri anapeta tu
Ukifatilia kwa makini utakuta baraza zima la mawaziri limeoza
.na mbadala hapa ni kuvunja baraza zima tu
kwa kuanza na kumwondoa PM..
My take: Kwa kuikumbushia mifano hii .bado nabaki kusema kuwa kelele za wabunge haswa wa CCM ni danganya toto tuliyozoea yenye lengo la kupoza vilio vya wananchi dhidi ya udhalimu wa serikali ..Itakumbukwa pia kuwa waziri mkuu alionyesha udhaifu mkubwa katika sakata la madaktari pale alipowadanganya madaktari na umma kuwa atalipeleka swala la madai yao .ikiwamo mawaziri wa wizara ya afya kwa rais lakini kilichotokea baadae wote twakijua pale huyu huyu PM alipojitokeza hadharani akipinga madai ya madaktari na haswa lile la kutimuliwa mawaziri husika .Kwa maana hii nashangaa eti wabunge wamemtuma Pinda aende kumweleza JK madai yao!!!!!!!!........yaaani Pinda tunayemjua akamwambie nini JK???????......nasikitika kwamba kwa Pinda huyu haya yatakuwa ni business as usual ..we have had a very painful experience with him already .so dont expect anything from him
Angalizo: Huu ni utawala wa kulindana .utawala wenye kuwalinda wezi na kuwaadhibu wasema ukweli only time will tell
My take: Kwa kuikumbushia mifano hii .bado nabaki kusema kuwa kelele za wabunge haswa wa CCM ni danganya toto tuliyozoea yenye lengo la kupoza vilio vya wananchi dhidi ya udhalimu wa serikali ..Itakumbukwa pia kuwa waziri mkuu alionyesha udhaifu mkubwa katika sakata la madaktari pale alipowadanganya madaktari na umma kuwa atalipeleka swala la madai yao .ikiwamo mawaziri wa wizara ya afya kwa rais lakini kilichotokea baadae wote twakijua pale huyu huyu PM alipojitokeza hadharani akipinga madai ya madaktari na haswa lile la kutimuliwa mawaziri husika .Kwa maana hii nashangaa eti wabunge wamemtuma Pinda aende kumweleza JK madai yao!!!!!!!!........yaaani Pinda tunayemjua akamwambie nini JK???????......nasikitika kwamba kwa Pinda huyu haya yatakuwa ni business as usual ..we have had a very painful experience with him already .so dont expect anything from him
Angalizo: Huu ni utawala wa kulindana .utawala wenye kuwalinda wezi na kuwaadhibu wasema ukweli only time will tell