SAKATA la UWANJA wa NYAMAGANA: Ubomoaji Wake na Migongano ya Taasisi Husika

attachment.php
 
Wapendwa muda huu kuna maandamano pale mwanza kupinga ubadilishaji wa matumizi ya uwanja wa Nyamagana. Eti mgeni rasmi ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza (mpenda vyeo) sasa wakati anahutubia na waandamaji wakitegemea kuwa atatoa tamko rasmi badala yake akawaambia wananchi wajaze saini zao kwenye daftari lililotolewa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza la kupokea maoni yao.
Waandamanaji walipomzomea akaanza kuwatishia kuwaweka ndani

Ngomanzito,

Tafadhari, endelea kutuletea habari kuhusu jambo hili. Sijui Eddy naye kapotelea wapi siku hizi.

Nilisoma mahali fulani kwamba Masha naye anaupinga mradi huu. Sasa kwa vile yeye ni diwani, aweke ushawishi mkubwa katika baraza la madiwani wenzake ili mradi huu usitishwe haraka.
 
More Pics za maandamano
 

Attachments

  • Picture 004.jpg
    Picture 004.jpg
    3.2 KB · Views: 51
  • Picture 005.jpg
    Picture 005.jpg
    8.5 KB · Views: 45
  • Picture 006.jpg
    Picture 006.jpg
    23.4 KB · Views: 44
  • Picture 003.jpg
    Picture 003.jpg
    24.2 KB · Views: 44
  • Picture 007.jpg
    Picture 007.jpg
    29.3 KB · Views: 46
Habari zilizopo ni kuwa Baadhi ya Madiwani wa CCM wamechukua ten percent kutoka kwa mhindi ili wafanye kila linalowezekana mhindi achukue uwanja wakiongozwa na Diwani Rukambura-CCM Kirumba
 
Hivi hakuna sehemu nyingine ya kufanya ujenzi wa hoteli ni mpaka pawe Nyamagana tu?
haya ndio matatizo ya fikra za kimaskini na tamaa!
 
Ndiyo kusema mpaka leo hakuna city planners mpaka madiwani waplan.Maana hawa planners lazima wameshaandaa maeneo kulingana na matumizi.Au hilo eneo ndiyo limevumbuliwa sasa.This is unbelievable.Either I am not sure of Dar or Ar if they real have and effectively utilize city planners.

very interesting Mkuu, ningekuwa na nakala ya sheria (soft copy)ningeiweka hapa. Sheria inayohusu Mipango Miji inasema kwamba mpangaji ni Kamati ya Mipango miji ya Halmashauri (Urban Planning Comittee kwa kifupi UPC). Hivyo Town Planner ni mtendaji, anapanga then anawasilisha kwenye Kamati. Kamati itatoa maamuzi yake ambayo yanaweza kuwa tofauti na mapendekezo ya wataalam. Maamuzi ya Madiwani unapaswa kuyafuaata kama utashindwa kuwashawishi.

Kumbuka kwamba Waziri wa Ardhi hawezi kuidhinisha mpango (General/detail planning scheme) kama hakuna Muhtasari wa Kamati UPC uliosainiwa na Mwenyekiti wa Kamati (Diwani) na Katibu (Mkurugenzi au Afisa Mipango Miji wa Halmashauri).

Hivyo utaona kwamba Afisa Mipango Miji hana uamuzi katika kupanga. Waamuzi ni Madiwani. Kumbuka katika vikao vya Kamati (UPC) na Kamati zingine za Halmashauri (isipokuwa ile ya kugawa ardhi) Wajumbe ni Madiwani. Wataalam si wajumbe, hivyo hawana nafasi ya maamuzi bali kushauri. Ushauri unaweza kukubaliwa au kukataliwa.
 
Jk amwondoe huyu Mkuu wa mkoa (a.k.a mpenda vyeo) amekuwa ni mchonganishi kati yake na viongozi mbalimbali jana kwenye sakata la uwanja anawatuhumu viongozi wa Wilaya ya Nyamagana eti wanatumia suala la kubinafsisha uwanja la kisiasa mwishowe viongozi wa CCM na wakashuka jukwaani wakamwacha akibwata hana jipya na hawezi kutoa tamko yaelekea hata yeye ni mmojawapo walovuta ten percent Bora Njolay angetoa tamko la msingi
 
Acha chama tawala kizidi kuwakela wananchi hapa mwanza, siku zao zinahesabika,sauti ya umma haisikilizwi sasa ila viongozi, na viongozi maslahi yao kwanza,ccm shitukeni, wasikilizeni wapiga kura wenu, mchawi hajilogi, nyie mbona mwajiloga wenyewe? Wasukuma wanawaomba msiuze huo uwanja wa nyamagana nyie mnang'ang'ania kuuza, haya uzeni!!!, nawajua wasukuma asili yao ni wapole ila ukiwaudhi utawaona wabaya.Mnataka kukatisha starehe yao!! hamjui Wasukuma hao baada kula ugali kwa samaki huja hapo kupumzika pamoja na kufanya mazoezi?
 
Naamini kuna vijielement vya udikteta hapa, huu mji wa Mwanza ni watu wa Mwanza, sasa kwanini matakwa yao yasisikilizwe kabla ya maamuzi hayajatolewa? Naamini wakazi wa mji wa Mwanza bado wana nguvu ya kupata kile wanachokitaka kama hawatachoka kupiga kelele kupinga huu ubabe wa manispaa yao.
Nchi za wenzetu kuliko endelea hata mnara wa simu hausimikwi kijijini bila ridhaa ya wananchi.
 
Jk amwondoe huyu Mkuu wa mkoa (a.k.a mpenda vyeo) amekuwa ni mchonganishi kati yake na viongozi mbalimbali jana kwenye sakata la uwanja anawatuhumu viongozi wa Wilaya ya Nyamagana eti wanatumia suala la kubinafsisha uwanja la kisiasa mwishowe viongozi wa CCM na wakashuka jukwaani wakamwacha akibwata hana jipya na hawezi kutoa tamko yaelekea hata yeye ni mmojawapo walovuta ten percent Bora Njolay angetoa tamko la msingi

Naona huyu apelekwe LINDI au RUKWa kama Njolay anastaafa
 
Oh samahani Mwewe, itabidi tumrudishe tu kwao Tobola/Tabora akarine asali na kulima tumbaku na maembe dodo
 
Nani Mkuu wa Mkoa wa mwanza sasa hivi?

......na hawa viongozi wanamuongoza nani? kwa nini hawataki kusikiliza matakwa ya wananchi?
 
Nani Mkuu wa Mkoa wa mwanza sasa hivi?

......na hawa viongozi wanamuongoza nani? kwa nini hawataki kusikiliza matakwa ya wananchi?

Ogah
Kama unakumbuka Lowassa akiwa WM alikuwa kwenye ziara ya Wilaya ya Ukerewe Kijana mdogo wa shule ya msingi alimuuliza swali kwanini Mkuu wa Mkoa awe na vyeo vingi kama alivyo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (Engineer,Mbunge,Dr,Mkuu wa Mkoa,Mjumbe wa NEC,Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Mkoa yeye,aligombea pia CC akashindwa
 
HEBU angalieni hapa watu walivyojitokeza na mabango, Usafi wa Pinda unaanza kunitia mashaka, Bngo moja linadai kuwa 'Pinda ulienda Nairobi Kenya na mwekezaji wakati wa kuapishwa baraza la Mawaziri', Pinda kauze kwanza Uwanja wa Nelson Mandela, Tulikujua Msimamo wako toka ukiwa TAMISEMI' na mengineyo angalieni katika picha
 

Attachments

  • 1.JPG
    1.JPG
    11 KB · Views: 53
  • 2.JPG
    2.JPG
    10 KB · Views: 39
  • 3.JPG
    3.JPG
    14.2 KB · Views: 55
  • 4.JPG
    4.JPG
    9.7 KB · Views: 51
  • 5.JPG
    5.JPG
    9.2 KB · Views: 38
Ogah
Kama unakumbuka Lowassa akiwa WM alikuwa kwenye ziara ya Wilaya ya Ukerewe Kijana mdogo wa shule ya msingi alimuuliza swali kwanini Mkuu wa Mkoa awe na vyeo vingi kama alivyo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (Engineer,Mbunge,Dr,Mkuu wa Mkoa,Mjumbe wa NEC,Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Mkoa yeye,aligombea pia CC akashindwa

Hivi jina la Mkuu wa Mkoa wa mwanza imekuwa siri siku hizi?.........nimejaribu kusearch naona Ole Njoolay (nafikri huyu alihamishwa).........again nani Mkuu wa Mkoa?......anyhelp Masanja, Bob Mkandara, SteveD!
 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ni Dr James Alex Msekela kama sijakosea, unaweza ukapata Details zake kwenye web ya Bunge. Ni mbunge wa Tabora Kaskazini kama sija kosea.


Sasa tukirudi kwenye maada ya huo Uwanja, hivi haiwezekani kujenga majengo mazuri kuzunguka uwanja ili ziwe Office, Bank, Restaurant, maduka na makazi ya watu???? na katika mambo ya michezo yakaendelea?
 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ni Dr James Alex Msekela kama sijakosea, unaweza ukapata Details zake kwenye web ya Bunge. Ni mbunge wa Tabora Kaskazini kama sija kosea.


Sasa tukirudi kwenye maada ya huo Uwanja, hivi haiwezekani kujenga majengo mazuri kuzunguka uwanja ili ziwe Office, Bank, Restaurant, maduka na makazi ya watu???? na katika mambo ya michezo yakaendelea?

Kuna viwanja vingi katika nchi mbalimbali viko katikati ya majiji yao na vina maduka,restaurant nk kama vilivyopo London hawa jamaa wameshindwa kujenga hoja na kutuletea mpango endelevu
attachment.php
 
Back
Top Bottom