MSAJILI WA HAZINA: Simon Group inamiliki 51% ya Hisa UDA na Serikali 49%, Jiji halina hisa

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
SERIKALI imetetea uuzwaji wa hisa za Shirika la Usafirishaji nchini (UDA) kwa Kampuni ya Simon Group na kwamba, kampuni hiyo inamilika hisa hizo kihalali.

Lawrance Mafuru, Msajiri wa Hazina akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam amesema, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliiuzia UDA hisa kihalali.

Utetezi huo unawapa pumzi Mama Salma Kikwete, Mke wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete na Ridhwan Kikwete, mtoto wa rais huyo na Prof. Juma Kapuya, aliyekuwa Mbunge wa Urambo Magharibi ambao wanatajwa kuwa miongoni mwa wana hisa kwenye kampuni hiyo.

“Bodi ya UDA iliyokuwepo muda ule ilikiuka taratibu za uuzaji wa hisa za serikali bila ya Baraza la Mawaziri ambalo lenye mamlaka ya kufanya maamuzi ya uuzwaji wa hisa kuamua kuuza hisa hizo,” amesema Mafuru.

Anaeleza kuwa, Bodi ya UDA iliamua kuuza hisa kwa Kampuni ya Simon Group baada ya kuona shirika hilo linayumba hivyo lilihitaji muwekezaji ili kulifufua.

“Baraza la Mawaziri chini ya mwenyekiti wake ambaye ni rais halikukaa kikao cha kufanya maamuzi ya kuuza hisa na kwamba, baada ya bodi kuona serikali inachelewa kutoa maamuzi ikaamua kuuza hisa za serikali,” anasema.

Amefafanua kuwa, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ndilo lililouza hisa zake kupitia Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji hilo kwa kushirikiana na wajumbe wenzake watatu akiwemo Mwanasheria wa Jiji.

“Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na jiji, lilipokea fedha kutoka Kampuni ya SGL kwa ajili ya manunuzi ya hisa zake na kwamba kwa sasa jiji halimiliki UDA, ” amesema.

Amedai, UDA linamilikiwa kihalali na Kampuni ya SGL ambayo inahisa asilimia 51 iliyouzwa na jiji pamoja na serikali ambayo ina hisa ya asilimia 49.

“Aliyeuza hisa za UDA kwa SGL ni Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na wajumbe wengine watatu akiwemo Mwanasheria wa Jiji, sasa kama Masaburi hakuwa Meya halali wa jiji basi hisa hazikuuzwa kwa kampuni ya SGL,” ameeleza.

Akieleza mwanzo wa ugawaji wa hisa za UDA kutoka kwa serikali kwenda Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambapo amesema, serikali iliona bora igawe hisa za asilimia 51 kwa jiji hilo ambalo UDA linapofanya kazi zake.

“Mnamo mwaka 1974 serikali ilianzisha shirika la UDA, mwaka mmoja baadaye serikali iliamua kugawa hisa ya asilimia 51 kwenda kwa jiji la Dar es Salaam na yenyewe kubaki na asilimia 49 ambazo inazo hadi sasa,” amesema.

Hivi karibuni Isaya Mwita, Meya wa Jiji la Dar es Salaam na Baraza la Halmashauri ya Jiji hilo lilikana kuitambua Kampuni ya SGL kuwa, mmiliki halali wa UDA.

Kwa mujibu wa maelezo yao, Masaburi alichukua jukumu la kuuza hisa za jiji kwa Kampuni ya SGL bila kulishirikisha baraza la madiwani la kipindi ambacho uuzaji ulipofanyika.

Siku tatu zilizopita, Saed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo alisema, halmashauri haikuuza UDA licha ya Simon Group Limited kudai kununua.

Kwenye mkutano huo ambao pia uliohudhuriwa na Isaya Mwita Charles, Meya wa Jiji la Dar es Salaam Kubenea alisema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu.

“Kwanza tunataka mtambue halmashauri haikuuza UDA kwa kuwa, Simon Group Limited wametumia hati ya UDA – mali ya wananchi kufanya biashara. Haturudishi fedha hizi mpaka tufanye hesabu, tujue kampuni hii imepata faida kiasi gani.

“Hata katika mradi wenyewe wa UDA-TR, kumesheheni utapeli. Unaoitwa mkutano mkuu maalum wa wana-hisa wa tarehe 10 Juni 2011, uliosimamiwa na Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji kuidhinisha pamoja na mengine, uuzaji wa hisa za UDA, haukuwa halali,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu

“Watu hawa ni Dk. Didas Masaburi mwenyewe ambaye alikuwa mwenyekiti; Mkurugenzi wa Simon Group, Robert Kisena ambaye alikuwa katibu; Mwanasheria wa jiji, Isaac Nassor Tasinga na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Phillip Mwakyusa,” amesema Kubenea.
 
WildCardJF-Expert Member
#25 Jul 13, 2011
Joined:Apr 22, 2008 7,47217 38
Watanzania uendeshaji wa mashirika ya umma umetushinda siku nyingi. Tulishindwa TBL, tukashindwa TCC, tukashindwa CRDB, THB, NBC, tukashindwa NMC, mashirika ambayo wateja wake sio wa kutafuta. Wanakuja wenyewe. Sasa hivi tumeshindwa TANESCO, tumeshindwa DAWASA/DAWASCO. Acha tu UDA iondoke. Hebu fikiria kituo kama kile cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo kinavyoendeshwa na mapato yanayopatikana pale! Kama mfumo wa uendeshaji mashirika ya UMMA ni huu tulionao na uongozi wa NCHI ni huu, Bunge ni hili, acha tu UDA iende inakokwenda. Mashirika ya UMMA yanatafunwa sana. Hayana mwenyewe
 
WildCardJF-Expert Member
#25 Jul 13, 2011
Joined:Apr 22, 2008 7,47217 38
Watanzania uendeshaji wa mashirika ya umma umetushinda siku nyingi. Tulishindwa TBL, tukashindwa TCC, tukashindwa CRDB, THB, NBC, tukashindwa NMC, mashirika ambayo wateja wake sio wa kutafuta. Wanakuja wenyewe. Sasa hivi tumeshindwa TANESCO, tumeshindwa DAWASA/DAWASCO. Acha tu UDA iondoke. Hebu fikiria kituo kama kile cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo kinavyoendeshwa na mapato yanayopatikana pale! Kama mfumo wa uendeshaji mashirika ya UMMA ni huu tulionao na uongozi wa NCHI ni huu, Bunge ni hili, acha tu UDA iende inakokwenda. Mashirika ya UMMA yanatafunwa sana. Hayana mwenyewe
Isiondoke kifisadi
 
WildCardJF-Expert Member
#25 Jul 13, 2011
Joined:Apr 22, 2008 7,47217 38
Watanzania uendeshaji wa mashirika ya umma umetushinda siku nyingi. Tulishindwa TBL, tukashindwa TCC, tukashindwa CRDB, THB, NBC, tukashindwa NMC, mashirika ambayo wateja wake sio wa kutafuta. Wanakuja wenyewe. Sasa hivi tumeshindwa TANESCO, tumeshindwa DAWASA/DAWASCO. Acha tu UDA iondoke. Hebu fikiria kituo kama kile cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo kinavyoendeshwa na mapato yanayopatikana pale! Kama mfumo wa uendeshaji mashirika ya UMMA ni huu tulionao na uongozi wa NCHI ni huu, Bunge ni hili, acha tu UDA iende inakokwenda. Mashirika ya UMMA yanatafunwa sana. Hayana mwenyewe
 
Mafuru aliharibu NBC,akapigwa chini,baadaye kikwete akampa kazi hazina,pia tukumbuke uhusiano uliopo Kati ya Familia ya jk na km waziri mkuu
 
Aliyeuza hisa za UDA kwa SGL ni Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na wajumbe wengine watatu akiwemo Mwanasheria wa Jiji, sasa kama Masaburi hakuwa Meya halali wa jiji basi hisa hazikuuzwa kwa kampuni ya SGL,” ameeleza.

Mafuru mbona hajibu hoja za msingi? Quorum ilitimia? Hao wengine ni akina nani?

Huyo Masaburi, ingawa alikuwa Meya, ni mshirika kwenye ufisadi. Ishu sio kama Masaburi hakuwa Meya.


Pili, kwanini hela zingine zikawekwa kwenye akaunti binafsi ya Idd Simba? Alishazirudisha?
 
Waziri Kawambwa mwaka jana akiwassilisha bajeti yake alisema hivi kuhusu UDA
65. Mheshimiwa Spika, kuhusu Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), Serikali imeendelea kuchukua hatua mbali mbali za kuiwezesha UDA kuwa na mtaji wa kujiendesha yenyewe, hii ikiwa ni pamoja na kuwasilisha mapendekezo Serikalini ya kufuta madeni ya muda mrefu ya UDA yenye thamani ya shilingi milioni 612.189 kwa lengo la kuboresha mezania ya Shirika ili iweze kupata fedha kutoka xtaasisi mbali mbali za kifedha. Aidha, kutokana na mapendekezo ya Bodi ya UDA kuhusu hatma ya shirika, Serikali iko katika majadiliano na mwekezaji ambaye amejitokeza kununua hisa za Serikali za aslimia 49.Kupatikana kwa mwekezaji kutawezesha UDA kuongeza uwezo wake wakutoa huduma za usafiri jijini Dar es salaam na kushiriki katika mradi wa mabasi yaendayo kasi.
 
Conflict of interest : JK raisi ndo mwenyekiti wa baraza la mawaziri... mkewe na mwanae wanataka nunua hisa kwenye shirika la Umma ambalo baraza ndo wanatakiwa wapitishe.... do... haya nyerere aliyaweka akijua maraisi wote watakuwa kama yeye.... alijisahau mzee wetu na watu wanapitia hapohapo...
 
Mafuru aliharibu NBC,akapigwa chini,baadaye kikwete akampa kazi hazina,pia tukumbuke uhusiano uliopo Kati ya Familia ya jk na km waziri mkuu

Akileta mambo ya kipuuzi na yule Vasco atumbuliwe tu. Hakuna namna. JPM hawezi kuwa na undumilakuwili.
 
WildCardJF-Expert Member
#25 Jul 13, 2011
Joined:Apr 22, 2008 7,47217 38
Watanzania uendeshaji wa mashirika ya umma umetushinda siku nyingi. Tulishindwa TBL, tukashindwa TCC, tukashindwa CRDB, THB, NBC, tukashindwa NMC, mashirika ambayo wateja wake sio wa kutafuta. Wanakuja wenyewe. Sasa hivi tumeshindwa TANESCO, tumeshindwa DAWASA/DAWASCO. Acha tu UDA iondoke. Hebu fikiria kituo kama kile cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo kinavyoendeshwa na mapato yanayopatikana pale! Kama mfumo wa uendeshaji mashirika ya UMMA ni huu tulionao na uongozi wa NCHI ni huu, Bunge ni hili, acha tu UDA iende inakokwenda. Mashirika ya UMMA yanatafunwa sana. Hayana mwenyewe


Baba umenena
 
Back
Top Bottom