Sakata la muro;mkuu wa upelelezi;kamishna wa polisi aibu tupu;mwema tuifwaitilie hili

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,921
22,073
Wapendwa
kwa wlaioona jana taarifa ya habari ya tbc kesi ya jerrymuro imezaa kesi nyingine juu yake baada ya mshitakiwa aitwae deogratias kusema aliitwa mbele ya mkuu wa upelelezi kanda ya dar es salaam na kamishna wa polisi kbw kasala na kuletewa karatasi ambayo ilikuwa juu yake imewekwa karatasi nyingine na kuambiwa asaini..alipokataa bw huyu aliambiwa asiposaini watamakesure wamemfunga akauliza kwa nini akaambiwa na mkuu wa upelelezi bw CHARLES MKUMBO sisi mtu wetu ni jerry muro amelizalilisha sana jeshi la polisi na niachokwambia hii saini ndio itakayokutoa ..na hii amri sio mmimi ni jkutoka makao makuu

JAMANI WATANZANIA NIMEANGALIA MWILI UKASISIMKA NIKASEMA KUMBE SEGEREA/KEKO NA MAGEREZA MENGINE YAMEJAA WAFUNGWA WENGI WASIO NA HATIA ..EMBU ANGALIA KAMA HILI ANAAMBIWA AMRI IMETOKA JUU JAMANI WATANZANIA TUWATAFUTE HAO WA JUU WATUELEZE WANATAKA NINI???HII KESI WENGI WALIONGEA MWEMA AKASEMA ATAISEMEA MPAKA LEO HII...ANYWAY TUSUBIRI UKWELI JAMAA WAMEITWA WAJE KUELEZA
 
Wapendwa
kwa wlaioona jana taarifa ya habari ya tbc kesi ya jerrymuro imezaa kesi nyingine juu yake baada ya mshitakiwa aitwae deogratias kusema aliitwa mbele ya mkuu wa upelelezi kanda ya dar es salaam na kamishna wa polisi kbw kasala na kuletewa karatasi ambayo ilikuwa juu yake imewekwa karatasi nyingine na kuambiwa asaini..alipokataa bw huyu aliambiwa asiposaini watamakesure wamemfunga akauliza kwa nini akaambiwa na mkuu wa upelelezi bw CHARLES MKUMBO sisi mtu wetu ni jerry muro amelizalilisha sana jeshi la polisi na niachokwambia hii saini ndio itakayokutoa ..na hii amri sio mmimi ni jkutoka makao makuu

JAMANI WATANZANIA NIMEANGALIA MWILI UKASISIMKA NIKASEMA KUMBE SEGEREA/KEKO NA MAGEREZA MENGINE YAMEJAA WAFUNGWA WENGI WASIO NA HATIA ..EMBU ANGALIA KAMA HILI ANAAMBIWA AMRI IMETOKA JUU JAMANI WATANZANIA TUWATAFUTE HAO WA JUU WATUELEZE WANATAKA NINI???HII KESI WENGI WALIONGEA MWEMA AKASEMA ATAISEMEA MPAKA LEO HII...ANYWAY TUSUBIRI UKWELI JAMAA WAMEITWA WAJE KUELEZA
Mwili umekusisimuka kwa sababu hujui kinachoendelea. Muro mla rushwa ataenda jela safari hii
 
kesi ndani ya kesi..hapatoshi ila kwa kweli tuna kazi kupambana na matukio ya namna hii. polisi hii ni kashfa wanayo miaka kibao kwa kisingiziom cha upelelezi ila uonevu huu yahitaji miujiza kuutokomeza coz wengi wanaofanyiwa hawajui sheria na hawana utetezi so hukaa kimya kuogopa wasijiingize matatizoni na WAKUBWA..
 
polisi wengi ni aina ya zombe, wezi, warafi na kazi yao ni kubambikiza kesi tu na kutafuta utajiri hata kama jeryy alitaka rushwa lakini ukweli uliopo ni kuwa jeshi la polisi lilikuwa linamtafuta kiaina ili kumkamata baada ya kuwaumbua kwa rushwa wanazokula
 
Muro alijisahau sana akaona yuko juu ya sheria na wale wajinga wachache waliokuwa wanamtuma kwa manufaa yao ndio wamemmaliza, kesi hii haruki lazima akanyee ndoo.
 
dont know whether i will ever stop wondering of zis country's issues!
 
muro alijisahau sana akaona yuko juu ya sheria na wale wajinga wachache waliokuwa wanamtuma kwa manufaa yao ndio wamemmaliza, kesi hii haruki lazima akanyee ndoo.

innocent until proven guilty
 
Mwili umekusisimuka kwa sababu hujui kinachoendelea. Muro mla rushwa ataenda jela safari hii
Wewe lazima uwe fisadi tena siyo mdogo,
Nadahani wewe ndo hujui kinachoendelea, Polisi hawa ni kama ni bora ya mbwa ambaye akiamrishwa kwa mtu asiyehatia hawezi kumng'ata tu ila kumshtua.

Jerry hana kosa lile ila Polisi waliona aibu na wameamua kumkomoa, Lakini Mungu siku zote huwa anaona, Na ukitaka kufaya Dhuluma lazima akupige changa la macho upofuke.

Hao wakubwa miaka yao ni michache maana wanawaacha wala rushwa wakubwa na kuwatia hatiani wapiganaji.
Kwani Kubenea ilikuwaje, na wapiganaji kibao.
jamani hawa watu pamoja na nyie washabiki wake mtatupeleka shimoni.
Lazima wajue kukomoana siyo utendaji mzuri, walisubiri atoboe ile rushwa ya polisi ndo wamtolee hilo?
Nakwambia lazima wataingia upofu kutoka kwa Mungu!!!
 
Jerry kakomolewa na na kesi ya kupikwa! Kama kweli hakimu atakuwa na haki, kina Jerry watatoka salama.
 
Polisi wa nchi hii wanafanya kazi ngumu sana, ila wachache wanaharibu utendaji wao, Kova anaharibu sana kazi ya polisi, huyu ni mpenda sifa , ujiko na mtu wa kariba ya makamba na tabwe hiza.
anafanya kazi ili aonekane, hii kesi itataliabisha JESHI letu la polisi, kwa upuuzi wa wawachache.
 
Huu ni ukweli lakini kimazingira tu hata mimi nisyekuwa mwanasheria najua. Andrew Chenge ni guilty. Huyu Jery Muro mazingira yanamfunga. Alikuwa msanii.

Hii siyo kweli, He is not Guilty hata kama watachora vema mipango yao lakini Itakuwa bure, mnachopaswa kujua ni kwamba waliamua kumdhalilisha kwa kazi aliyofanya

Kwani yeye si alikuwa anaonesha LIVE bila ya kutafutiza,
Ona sasa wao wanavyohangaika kutafuta ushaidi, Kwani Kamera za CCTV si zingetosha?
Mbona hawatokei mahakamani wanachora nini na wao ni wapelelezi wasomi, wakati mwenzao alikuwa anachukua kamera na kuweka tu runingani na kila mtu akaona.

Tungeni wee na mkitumia nguvu zenu mshinde, Mungu atawagonga ngooooo! mtatia aibu maana bado hawajaacha.
 
Jerry kakomolewa na na kesi ya kupikwa! Kama kweli hakimu atakuwa na haki, kina Jerry watatoka salama.

Tena wamepika vibaya, wanapikia uji kwenye mkaa,
Ni nguvu zao tu ndo zinawalinda, Kwakweli wamezoea kupika kesi ili wawanyamazishe watu.
 
Jerry alifanya kazi nzuri lakini nayeye msanii tu/ sasa amekutana na wasanii wenzake kazi kweli kweli
 
Muro alijisahau sana akaona yuko juu ya sheria na wale wajinga wachache waliokuwa wanamtuma kwa manufaa yao ndio wamemmaliza, kesi hii haruki lazima akanyee ndoo.

Hatanyea ndoo kabisa, Kuwa chini ya sheria nu Kuficha maovu, au Kuwa juu ya sheria ni kuyalipua maovu ya watu wanaotakiwa kutoa huduma kwa watu na kuaamua kushibisha matumbo yao bila aibu?

Yeye alisahau tu kuwa polisi wameshika mpini naye makali. Na alipaswa kuwa Muoga kama watanzania wengine tulivyo.
Hakujua kuwa wana kila aina ya kutwisha mtu kesi hata iwe kubwa vipi.
 
Jerry kakomolewa na na kesi ya kupikwa! Kama kweli hakimu atakuwa na haki, kina Jerry watatoka salama.
.
Wapenzi wa Jerry na wote mnaikubali kazi yake, msiwe na wasiwasi, Jerry atashinda kesi, polisi wana very weak case agaist him, kesi zote za rushwa zinahitaji strong evedence to make conviction, vitu ambavyo havipo.

Sisi hatuna Cybe law hapa kwetu, na Electronic evidence ya video kupitia CCTV camera is in-addmisable evidence, hivyo hakuna kesi hapo, ni kuchafuliana tuu majina na kupotezeana muda.

Tatizo ninaloliona, hata kama Jerry atashinda hii kesi, he will never be the same Jerry again. Ndivyo yaliyomkuta O.J. Simpson, hata kama alishinda kesi, he was never the same again.

Ushauri wangu kwa Jerry, kesi ikiisha, arudi shule akapige Masters ya kitu alichosomea pale UDSM.
 
Jeshi la Polisi ni uozo mtupu. Nilitarajia mengi kutoka kwa Mwema lakini kwa kuwa kazungukwa na wala rushwa, wasio jua kazi na wenye shule kidogo inakuwa vigumu sana kubadilika kwa jeshi hilo. Kuna matukio mengi sana yanayothibitisha kuwa Jeshi la Polisi uwezo wake ni mdogo sana tena haswa kikosi cha upelelezi. Inafikia hatua tunajiuliza wanacho peleleza ni nini? Mbona maovu kibao yanafanyika kila siku ndani ya bongo na hakuna kinachofanyika. Wengi wao wamechoka kwa pombe za ofa na ndo hizo zinazoharibu utendaji wa kazi zao. Mie nina imani kuwa Jerry alikuwa anawindwa ili anamalizwe kwa kazi zake nzuri alizokuwa anafanya. Na huenda muajiri wake wa zamani anahusika katika mkakati huo.
 
Back
Top Bottom