Sakata la mgomo wa madaktari kuna shinikizo la kisiasa-wasomi

Wasomi mbalimbali wamesema sakata la mgogoro wa Madaktari na serikali linachochewa wanasiasa kutokana na misimamo ya wanasiasa hao walioitoa kwa nyakati tofauti huku wasomi hao wakinena kama ifuatavyo:

1. Uhai haupimwi na kitu chochote, Utaratibu wa Madaktari kugoma umepigwa marufuku katika nchi nyingi duniani-Dk.BENSON BANA
2. Ni tabia mbaya kuona kada moja inajiona ni bora kuliko nyingine-Dk. Bana
3. ANANILEA NKYA kusema kitendo cha Mawaziri wa Afya kushindwa kujiuzulu ni maajabu ni dhahiri suala hili limejaa siasa-SALIM SAID
4. Haki bila nidhamu, wajibu ni sawa na wazimu-Salim Said
5. Kuna njama za kuidhoofisha Serikali kupitia taaluma ya Udaktari-JOSEPH LUGHA
6. Kumpa Rais siku kwa ajili ya kutaka kufanikisha mambo yao ni kinyume na utamaduni wa Watanzania-BANA

Tutafakari

50% ya ulichosema kimesemwa na wasomi kimesemwa na Dr. Bana. Kwa maana nyingine unataka kuaminisha watz kuwa bana anawakilisha 50% ya wasomi hapa tz.

Unatakiwa kufahamu kwamba,

Dr. Bana ni muumini mzuri sana wa siasa na ni wa upande wa CCM. Ni mshabiki mzuri sana wa siasa za upande mmoja na kwa taarifa tu ni kwamba anajipendekeza kwa CCM kwa ajili ya kujiandaa kutwaa madaraka UDSM
 
Bana yuko kazini pale. Subiri kidogo utasikia ni mshauri wa siasa wa JK. Kuna mwenzie alikuwa paple political science nilikutana nae dodoma wakati JK ameenda kuongea na wabunge wa chama. kumbe ni mshauri wake wa siasa. Sasa Bana zamu yake inakaribia. Kaua hata TEMCO hebu we jiulize ile taarifa ya election monitoring waliyopata mamilion toka UNDP iliishia wapi? wanatumika tu na mwenzie Mkandala
 
Dr Bana mara nyingi huwa anahesabiwa kama msomi lakini mimi naona ingekua vema kama angekua anachukuliwa kama kada wa CCM na sio Msomi aliye huru kutoa maoni ya kitaaluma yasiyo kuwa biased.

Imezoeleka kwamba kila challenge inayoenda kwa serikali wanasema siasa imo ndani yake.CHADEMA wamekuwa wahanga na watuhumiwa namba moja katika hili.Serikali na CCM yake wanakimbia matatizo kwa ku justify kwamba ni uchochezi wa siasa za wapinzani.Serikali imekuwa na watu wavivu wasiooweza kutafakari Subject Matter ya Challenge(Kwa sasa mgomo wa madaktari)-Pinda alikaa na madaktari wakakubaliana na kuweka timeline ya utekelezaji,Serikali haijatekeleza according to timeline.Madaktari wana haki ya kusimamia msimamo wao kadri ya makubaliano ya awali.WATANZANIA,Ili kuwa na mabaduiliko ya kweli kuna gharama,kuna gharama kubwa na hata watu kupoteza maisha ili kuwa na ukombozi wa kweli,kwa woga wetu watanzania hatutaweza kwenda mbele,hatutaweza kusimamia serikali zaidi hatutaweza kusimamia rasilimali zetu.

Tunakubaliana kwamba serikali imeoza,NANI ATUTETEE? Sio wakati wa kuwalaumu madaktari,jiulize umefanya nini wewe binafsi kama unakereka na serikali hii.Tuwe watu wa kuthubutu na kuchukua hatua,tuwe watu wa kusimamia tunayoyaamua,tuwe watu wa kutetea tunachoamini,tuwe watu wa kutetea haki zetu.THIS IS THE TIME,TOMORROW WILL NEVER COME.
 
Mtanisamehe wana JF, ila kwa mawazo hawa madaktari wanajaribu tu kuwa difficult bila sababu yeyote ya msingi. Hivi toka wamekubaliana kuingia kwenye meza ya majadiliano na Serikali hao Haji Mponda na Lucy Nkya wameongea kitu gani ambacho kimekua kikwazo kwenye majadiliano yao. Wanachotafuta hao madaktari ni sifa tu ili waonekane wamewaondoa Mawaziri.

Serikali lazima iwe makini kwenye hili na isifanye maamuzi kwa vile tu kundi fulani linataka waziri fulani aondolewe. Kama Mponda na Nkya wataondelewa madarakani kwa vile tu Madaktari wanataka hivyo, then JK ajiandae kwasababu na yeye atakua njiani kuondolewa kwa style hiyo hiyo. Itakuaje leo Walimu nao waseme Waziri wa elimu aondolewe kwa vile wamecheleweshewa kulipwa marupu rupu yao? Itakuaje na mapolisi nao wakitaka waziri wa mambo ya ndani aondolewe kwa vile mishahara yao ni midogo, itakuaje.......

Nchi haiendeshwi hivyo na kuna vyeo serikalini ambavyo unaweza kucheza navyo na kushurutishwa mtu aondolewe madarakani, lakini sio kwenye uwaziri au urais. Hao madaktari kama kweli wanania ya kutatua matatizo yao waendeleze majadiliano na serikali bila kuweka masharti ambayo hayana dira. Tatizo la malipo duni kwa Tanzania sio la Mawaziri wa afya tu, ni la mfumo mzima wa nchi. Inasikitisha sana kuona madaktari wanataka kutumia taaluma zao ambazo ni za muhimu kwa maisha ya binadamu, kuwanyanyasa wananchi wasio na Hatia.
 
Wasomi mbalimbali wamesema sakata la mgogoro wa Madaktari na serikali linachochewa wanasiasa kutokana na misimamo ya wanasiasa hao walioitoa kwa nyakati tofauti huku wasomi hao wakinena kama ifuatavyo:

1. Uhai haupimwi na kitu chochote, Utaratibu wa Madaktari kugoma umepigwa marufuku katika nchi nyingi duniani-
Dk.BENSON BANA
2. Ni tabia mbaya kuona kada moja inajiona ni bora kuliko nyingine-Dk. Bana
3. ANANILEA NKYA kusema kitendo cha Mawaziri wa Afya kushindwa kujiuzulu ni maajabu ni dhahiri suala hili limejaa siasa-SALIM SAID
4. Haki bila nidhamu, wajibu ni sawa na wazimu-Salim Said
5. Kuna njama za kuidhoofisha Serikali kupitia taaluma ya Udaktari-JOSEPH LUGHA
6. Kumpa Rais siku kwa ajili ya kutaka kufanikisha mambo yao ni kinyume na utamaduni wa Watanzania-BANA

Tutafakari
Hivi huyu anaejiita dr Bana ni kweli anaelimu ya kuweza kuitwa dr au ni mwanasiasa, kwani mie simwelewi. Kama serikali aithamini kada ya udaktari kwa vile viongozi wanatibiwa nje. Na kudharau huduma za hospitali zetu kwanini madaktari wasigome kwa maslai ya wananchi. Ukiangalia wanasababu za msingi ni kweli hospitali zetu ni duni na hazina vifaa,ukilinganisha na maofisi za kuanzia kwa wakuu wa wilaya mpaka mawaziri na rais mwenyewe. Hebu tizama fenicha zilizopo katika hizo ofisi na utizame bechi tu za kukalia wagonjwa wanaosubiri huduma au utizame ofisi ya daktari utashangaa. Huyu anayejiita dr Bana angalie picha zilizopigwa katika hospitali inayoitwa ya taifa tanzania(Muhimbili) wakati wa mgomo wa kwanza, vifaa vilivyoko vilivyochaa. Bana achane na siasa za mwaka 47 kuwa rais asiulizwe kitu au kumwambia eti sio utamaduni wa mtanzania. Kwasasa ni wakati wa vitendo rais akikosea anawajibishwa sio wakati wa rais kuwa ikulu kustarehe. Sasa huyu Bana anasema madaktari wanadai madai yao, ukifuatilia madai ya madaktari yanahusu watanzania wote wala sio kwa ajili yao tu. Madaktari wametoa madai yao tangu mwezi uliopita na wakakubaliana serikali haijatekeleza halafu leo hii Bana anatamka maneno ambayo hata mwanafunzi wa darasa la saba hawezi sema. Kwanza vifo vilivyotokea wakati wa mgomo wa kwanza ni tosha kwa waziri wa afya kujiuzulu. Lakini mpaka sasa hajajiuzulu na rais nae wala hajamwajibisha sasa hapa Bana anawalaumu madaktari kwa lipi kama sio huyo rafiki yake rais anaemtetea kashindwa kazi. Kwanza nawashangaa sana wandishi wanaomfuata huyu Bana ili kupata mawazo yake. Hafai hana mawazo ya kuendeleza nchi yeye anamawazo ya kuonewa huruma ili apewe cheo. Kwa upande wangu niko nanyi madaktari endeleeni kudai haki zenu na haki kwa watanzania. Waziri mkuu anasema kuwa waziri wa afya ni mgeni katika wizara na ameyakuta matatizo, huyu waziri kakaa mwaka mzima ameshindwa kuyatatua matatizo aliyoyakuta inamaana uwezo wake ni mdogo. Hivyo waziri mkuu anataka kutuaminisha kuwa tumwachie huyu waziri akae kwa miaka mitano ndio atatatua matatizo ya wizara ya afya. Waziri mkuu nae uwezo wake mdogo ukiangalia kwa makini ni yaleyale ya kulindana sio kufanya kazi. Tizama kwa wenzetu unaweza kuchaguliwa leo kuwa waziri baada ya mwezi moja inatokea matatizo katika wizara yako wa kwanza kuwajibika ni wewe wala haijalishi umekaa muda gani. Inachotakiwa ni utendaji wako wa kazi kuwa kiongozi sio starehe. Bana achana na mawazo ya enzi hizo za mwaka 47 tuko 2012
 
Mimi binafsi huwa nina mashaka makubwa na kauli za huyu Nshomile mwenzangu anazozitoa, kwa mujibu wa katiba yetu anayo haki ya kutoa mawazo lakini kwa usomi wake pia idara anayoiongoza nilitegemea awe anatoa maoni ambayo hayana utata. Kwetu tuna msemo wa kujihadhali na maneno yasiyo na msimamo yatolewayo na watu wanaopewa jina kuwa ni ABALUSHU sijui kama ktk Kiswahili wanaitwa NDUMILA KUWILI. Dr Bana jisimamie wakati unapokuwa unajibu maana mamilioni wanaamini kuwa wewe kama Nshomile usemacho ndio ukweli usiume na kupulizia kaka, kwetu Maruku hatupo hivyo.
 
Kuna matatizo kadhaa katika hili janga la mgomo wa madr! Kuna wanajamvi wanashabikia ili hali wakijua kwamba serikali (kwa maana ya viongozi wanaozozana nao hawaathiriki), wanaojiita wanaharakati pia wanashadadia mgomo sielewi huruma yao ni kwa nani ( wananchi wanaokufa au Drs)! Kwa mtazamo wangu madai ya msingi ni nyongeza ya mshahara, posho na mazingira bora ya kazi, Hili la lazima Waziri na Naibu wake kuondoka ni SIASA tu isiyokuwa na uhusiano na madai yao ya msingi! Guys, think Twice before you support.

My Take: Kosa kubwa lililofanywa na serikali mwanzoni ni kunywea na kuwasimamisha Ms. Nyoni na Dr. Mtasiwa, nilijua atafuata waziri wa afya na naibu wake, wakishaondoka atafuata Waziri Mkuu na baadae Rais! Kisha Ma - Dr ndo watateua hadi baraza la mawaziri.
 
Huyu Bana tumemzoea,yeye anakula na wakubwa kwa hiyo hawezi ona maumivu ya kada za chini kwenye utumishi wa umma.
 
Back
Top Bottom