EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Ripoti ya Uchaguzi Chadema
Ripoti ya Kamati iliyondwa na Chadema kuchunguza maridhiano ya madiwani wake ,CCM na TLP Arusha Mjini, imesema hakuna tuhuma za rushwa katika mchakato huo kama ilivyoeleza na baadhi ya viongozi wa chama hicho akiwemo Lema.
Dk Slaa awaandikia barua madiwani
Kamati Kuu ya Chadema imewataka madiwani wake kuomba radhi kama sehemu ya utawala bora. Barua hiyo ya kuwataka waombe radhi madiwani wote inakuja zikiwa ni siku chache tu mara baada ya madiwani wanane kuitunishia misuli Chadema iliyowataka wajiuzulu nyadhifa zao walizozipata katika mwafaka wakidai hawawezi kujiuzulu.
Kwa mujibu wa taarifa za uhakika zinadai ya kuwa barua za kuwataka madiwani hao waombe radhi zimetua mkoani Arusha, jana mnamo saa 4;30, ambapo zilisambazwa kwa madiwani wote.
Barua hiyo (Mwananchi ina nakala yake) yenye KUMB c/hq/m/ar/01/157 na kichwa cha habari kisemacho,
"YAH;KUTAKIWA KUOMBA KWA USHIRIKI WENU KATIKA KURIDHIA MWAFAKA /MARIDHIANO BATILI"
iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willlibrod Slaa, inawaagiza madiwani hao kuwa ni imani yao watafuata agizo la kuomba radhi kwa kutumia busara zao na utawala bora.
"Chadema toka mwanzo ilipinga uchaguzi wa meya, jambo lililopelekea "maandamano makubwa tarehe 5 Januari 2011 kutokana na kukiukwa kwa sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi kitendo cha maridhiano /mwafaka wa 15,4,2011 na uchaguzi uliofuatia wa naibu meya nao unakiuka sheria ,kanuni na taratibu maradufu kuliko hata uchaguzi wa meya mwenyewe"
Katibu wa Chadema, Dk Slaa alipoulizwa na gazeti hili alikiri chama chao kuwaandikia barua madiwani hao huku akisisitiza, yeye hataki kujibishana na madiwani hao, lakini watapambana na sheria hadi kufikia leo majira ya saa 7.02 mchana.
"Mimi sihitaji kujibishana na madiwani wetu, lakini nasubiri hadi kesho (leo) saa 7:02 mchana tujue, wao watapamba na sheria kama kuna mtu anaweza kupambana na sheria tutaona,"alisema Slaa.
My Take:
Naomba kufahamishwa iikiwa barua za kutakiwa kujiuzulu nyadhifa zao bado ziko pale pale au zilitolewa kimakosa, au zimeambatana na barua za kuomba Radhi. Kuna mkanganyiko, habari inasema barua za kuomba Radhi zimetumwa baada ta Madiwani kutunisha misuli barua za kujiuzulu.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/49-uchaguzi-mkuu/13854-ccm-chadema-wavutana-bungeni
Source: Gazeti la Mwananchi
Ripoti ya Kamati iliyondwa na Chadema kuchunguza maridhiano ya madiwani wake ,CCM na TLP Arusha Mjini, imesema hakuna tuhuma za rushwa katika mchakato huo kama ilivyoeleza na baadhi ya viongozi wa chama hicho akiwemo Lema.
Dk Slaa awaandikia barua madiwani
Kamati Kuu ya Chadema imewataka madiwani wake kuomba radhi kama sehemu ya utawala bora. Barua hiyo ya kuwataka waombe radhi madiwani wote inakuja zikiwa ni siku chache tu mara baada ya madiwani wanane kuitunishia misuli Chadema iliyowataka wajiuzulu nyadhifa zao walizozipata katika mwafaka wakidai hawawezi kujiuzulu.
Kwa mujibu wa taarifa za uhakika zinadai ya kuwa barua za kuwataka madiwani hao waombe radhi zimetua mkoani Arusha, jana mnamo saa 4;30, ambapo zilisambazwa kwa madiwani wote.
Barua hiyo (Mwananchi ina nakala yake) yenye KUMB c/hq/m/ar/01/157 na kichwa cha habari kisemacho,
"YAH;KUTAKIWA KUOMBA KWA USHIRIKI WENU KATIKA KURIDHIA MWAFAKA /MARIDHIANO BATILI"
iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willlibrod Slaa, inawaagiza madiwani hao kuwa ni imani yao watafuata agizo la kuomba radhi kwa kutumia busara zao na utawala bora.
"Chadema toka mwanzo ilipinga uchaguzi wa meya, jambo lililopelekea "maandamano makubwa tarehe 5 Januari 2011 kutokana na kukiukwa kwa sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi kitendo cha maridhiano /mwafaka wa 15,4,2011 na uchaguzi uliofuatia wa naibu meya nao unakiuka sheria ,kanuni na taratibu maradufu kuliko hata uchaguzi wa meya mwenyewe"
Katibu wa Chadema, Dk Slaa alipoulizwa na gazeti hili alikiri chama chao kuwaandikia barua madiwani hao huku akisisitiza, yeye hataki kujibishana na madiwani hao, lakini watapambana na sheria hadi kufikia leo majira ya saa 7.02 mchana.
"Mimi sihitaji kujibishana na madiwani wetu, lakini nasubiri hadi kesho (leo) saa 7:02 mchana tujue, wao watapamba na sheria kama kuna mtu anaweza kupambana na sheria tutaona,"alisema Slaa.
My Take:
Naomba kufahamishwa iikiwa barua za kutakiwa kujiuzulu nyadhifa zao bado ziko pale pale au zilitolewa kimakosa, au zimeambatana na barua za kuomba Radhi. Kuna mkanganyiko, habari inasema barua za kuomba Radhi zimetumwa baada ta Madiwani kutunisha misuli barua za kujiuzulu.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/49-uchaguzi-mkuu/13854-ccm-chadema-wavutana-bungeni
Source: Gazeti la Mwananchi