nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
*Zitto adai Serikali imejitia kitanzi
NA Waandishi Wetu, jijini Habari Leo
MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameibuka na kusema kitendo kinachofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa watendaji wake
kutakiwa kujivua gamba kinaweza kuathiri utendaji wa Serikali.
Zitto amesema CHADEMA haioni kuwa kitendo hicho kinaweza kukisaidia chama hicho kuwa na wanachama wasafi.
Sidhani kama huo utaratibu unaweza kuwaondoa mafisadi bali kunaweza kuathiri utendaji wa Serikali kwa kuwaondoa viongozi wasio na makosa, amesema Zitto.
Amesema kwa kuwa wapinzani wakubwa wa CHADEMA ni CCM, wamedhamiria kukaa pembeni na kuangalia ni kitu gani kitafuatia.
Zitto amesema suala la ufisadi ni jukumu la mtu binafsi kuamua kuachana na suala hilo na si la kushinikizwa.
Hivi sasa CHADEMA inaangalia mechi hiyo ili kuweza kufahamu itakwishaje na ndio maana tumekaa pembeni kuwaangalia hawa wapinzani wetu wakubwa, amesema Zitto.
Zitto amesema chama chake kitaendelea kuwa mstari wa mbele kwa kuhakikisha kuwa suala la ufisadi linakomeshwa nchini.
Amesema bado suala hilo linahitaji nguvu zaidi kwa kuwa baadhi ya maeneo kumejengeka mizizi ambayo inahitaji kung'olewa.
Hii mizizi inahitaji kung'olewa hivyo kama wananchi wataamua kufanya hivyo itawalazimu kwanza kukubaliana na CHADEMA kwa kukipa nguvu zaidi katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu, amesema Zitto.
NA Waandishi Wetu, jijini Habari Leo
MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameibuka na kusema kitendo kinachofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa watendaji wake
kutakiwa kujivua gamba kinaweza kuathiri utendaji wa Serikali.
Zitto amesema CHADEMA haioni kuwa kitendo hicho kinaweza kukisaidia chama hicho kuwa na wanachama wasafi.
Sidhani kama huo utaratibu unaweza kuwaondoa mafisadi bali kunaweza kuathiri utendaji wa Serikali kwa kuwaondoa viongozi wasio na makosa, amesema Zitto.
Amesema kwa kuwa wapinzani wakubwa wa CHADEMA ni CCM, wamedhamiria kukaa pembeni na kuangalia ni kitu gani kitafuatia.
Zitto amesema suala la ufisadi ni jukumu la mtu binafsi kuamua kuachana na suala hilo na si la kushinikizwa.
Hivi sasa CHADEMA inaangalia mechi hiyo ili kuweza kufahamu itakwishaje na ndio maana tumekaa pembeni kuwaangalia hawa wapinzani wetu wakubwa, amesema Zitto.
Zitto amesema chama chake kitaendelea kuwa mstari wa mbele kwa kuhakikisha kuwa suala la ufisadi linakomeshwa nchini.
Amesema bado suala hilo linahitaji nguvu zaidi kwa kuwa baadhi ya maeneo kumejengeka mizizi ambayo inahitaji kung'olewa.
Hii mizizi inahitaji kung'olewa hivyo kama wananchi wataamua kufanya hivyo itawalazimu kwanza kukubaliana na CHADEMA kwa kukipa nguvu zaidi katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu, amesema Zitto.