Sakata la kujivua gamba CCM Zitto adai Serikali imejitia kitanzi

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
*Zitto adai Serikali imejitia kitanzi

NA Waandishi Wetu, jijini Habari Leo

MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameibuka na kusema kitendo kinachofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa watendaji wake
kutakiwa kujivua gamba kinaweza kuathiri utendaji wa Serikali.

Zitto amesema CHADEMA haioni kuwa kitendo hicho kinaweza kukisaidia chama hicho kuwa na wanachama wasafi.

“Sidhani kama huo utaratibu unaweza kuwaondoa mafisadi bali kunaweza kuathiri utendaji wa Serikali kwa kuwaondoa viongozi wasio na makosa,” amesema Zitto.

Amesema kwa kuwa wapinzani wakubwa wa CHADEMA ni CCM, wamedhamiria kukaa pembeni na kuangalia ni kitu gani kitafuatia.

Zitto amesema suala la ufisadi ni jukumu la mtu binafsi kuamua kuachana na suala hilo na si la kushinikizwa.

“Hivi sasa CHADEMA inaangalia mechi hiyo ili kuweza kufahamu itakwishaje na ndio maana tumekaa pembeni kuwaangalia hawa wapinzani wetu wakubwa,” amesema Zitto.

Zitto amesema chama chake kitaendelea kuwa mstari wa mbele kwa kuhakikisha kuwa suala la ufisadi linakomeshwa nchini.

Amesema bado suala hilo linahitaji nguvu zaidi kwa kuwa baadhi ya maeneo kumejengeka mizizi ambayo inahitaji kung'olewa.

“Hii mizizi inahitaji kung'olewa hivyo kama wananchi wataamua kufanya hivyo itawalazimu kwanza kukubaliana na CHADEMA kwa kukipa nguvu zaidi katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu,” amesema Zitto.
 
Hii mechi itakuwa kama ile ya Real Madrid na Barcelona. There will be plenty of divers lakini hawataonyeshwa red card.
 
Mizizi imetanda hawawezi kuikata kiusalama; CC na NEC yote ina matajiri Uchwara
 
*Zitto adai Serikali imejitia kitanzi

NA Waandishi Wetu, jijini Habari Leo

MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameibuka na kusema kitendo kinachofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa watendaji wake
kutakiwa kujivua gamba kinaweza kuathiri utendaji wa Serikali.

Zitto amesema CHADEMA haioni kuwa kitendo hicho kinaweza kukisaidia chama hicho kuwa na wanachama wasafi.

“Sidhani kama huo utaratibu unaweza kuwaondoa mafisadi bali kunaweza kuathiri utendaji wa Serikali kwa kuwaondoa viongozi wasio na makosa,” amesema Zitto.

Amesema kwa kuwa wapinzani wakubwa wa CHADEMA ni CCM, wamedhamiria kukaa pembeni na kuangalia ni kitu gani kitafuatia.

Zitto amesema suala la ufisadi ni jukumu la mtu binafsi kuamua kuachana na suala hilo na si la kushinikizwa.

“Hivi sasa CHADEMA inaangalia mechi hiyo ili kuweza kufahamu itakwishaje na ndio maana tumekaa pembeni kuwaangalia hawa wapinzani wetu wakubwa,” amesema Zitto.

Zitto amesema chama chake kitaendelea kuwa mstari wa mbele kwa kuhakikisha kuwa suala la ufisadi linakomeshwa nchini.

Amesema bado suala hilo linahitaji nguvu zaidi kwa kuwa baadhi ya maeneo kumejengeka mizizi ambayo inahitaji kung'olewa.

“Hii mizizi inahitaji kung'olewa hivyo kama wananchi wataamua kufanya hivyo itawalazimu kwanza kukubaliana na CHADEMA kwa kukipa nguvu zaidi katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu,” amesema Zitto.

unafiki mtupu
 
Hakuna chama cha wababaishaji kama ccm ilikuwa siku 90 sasa wamesema chama kimekuwa imara baada ya kuvua MAGAMBA ngoja wajimalize wenyewe kwa kucheza na uozo
 
MHESHIMIWA ZITTO NAKUOMBEA KWA MUNGU AKUJALIE TENA ULE UJASIRI WA ZAMANI WA KUNYOOSHA KAULI JUU YA MASUALA NYETI NA YENYE MASLAHI YA UMMA KITAIFA

Zitto Zuberi Kabwe,

Naomba sana tukubaliane kutofautiana kidogo katika baadhi ya kauli ulizozitoa humu.

Kwanza, endapo kilichoandikwa ni maneno yako kweli basi nikatae hapa kwamba JANGA LA UFISADI (kauli ya kwanza hapo chini) si suala la Mtu binafsi na kwamba akaachwe tu kule kujipima mwenyewe na kuhiari njia gani akajipitie.

Sababu yangu kuamini hivyo ni kwamba kodi zinazosadikiwa kukwapuliwa na watuhumiwa wa UFISADI ulikua ni mali ya Umma kwa ujumla wetu hivyo kufanya suala zima hapa kuwa na Maslahi ya Jamii nzima ya Tanzania.

Hivyo watuhumiwa wa ndani ya CCM na serikali yake wakimaliza KUBEMBELEZANA KUJIUZULU huko katika kifindi cha siku 90 basi sisi Nguvu ya Umma tutalazimika kuchukua hiyo kesi kuja kwenye mahakama yetu ili kama waathirika wa janga hilo, ukwapwaji wa kila mara ya kodi zetu na kudidimiziwa maendeleo, ili tukalitolee maamuzi sahihi na ya kudumu.

Pili, kwa kuzingatia ukweli kwamba zao 'Pamba' kamwe haiwezi kufifia hata kidogo ueupe wake endapo wakati wote halikukutana na uchafu wowote popote pale, basi hata watumishi wetu serikalini uliowataja kama 'Wasio na Makosa' nao kamwe hawawezi kupigwa dhoruba yoyote ile ya fagio la chuma kuondoa ufisadi kwenye mfumo wetu kama hawakuwahi kushiriki UFISADI au kusaidia jambo hilo kutokea.

Kwa msingi huo, aheri tubaki na watumishi wawili waaminifu katika kila idadi 1000 ili nafasi hizo 998 zikatangazwe kwa utaratibu mpya, kuzingatia miiko ya uongozi ndani ya Azimio la Arusha na sheria na vyombo vya usimamizi kuimarishwa maradufu kuzuia kabisa hali hiyo. Endapo mtapenda kujua 'njia zipi zitumike mara baada ya hapo' basi mkatuulize hapa JF - tutatoa mkakati kiboko ambayo hakuna atakayeamini wengine tumeikalia tu kimya hapa kwa kuwa hata siku moja hatupewi nafasi tu.

Tatu, yeyote atakayekua amesoma na kutafakari vema kauli yako namba moja na mbili bila shaka atakua amebaki ameduazwa bila kuelewa kama aliyetoa na kauli ya tatu na ya nne bado ni mtu yule yule AU NI NAFSI YA KUTOKEA wakati zile kauli mbili za mwazo zilitoka kwa NAFSI YA KUSHINDIA ndani mwake mtu yule yule mmoja.

Hiyo hali ya mkanganyiko unatokana na ukweli kwamba tayari umetoa Judgment kwamba Mtanzania yeyote ni ruksa tu kuwaibia wenzake ilmradi tu kipenyo kinapatikana kwaki kama kiongozi wa ngazi fulani hivi ila pale suala la kuwajibika kubeba mshahara wa dhambi hiyo basi sasa Wa-Tanzania wenye kuibiwa kamwe hawana nafasi kumtaka MKWAPWAJI YEYOTE kubeba msalaba wake mpaka jambazi huyo tu akiamka vizuri ndio akajionelee kama ni vema akaturejeshee kilichoibwa au ajiuzulu au asijishughulishe kabisa na lolote lile.

Mhe Zitto, hili nalipinga hata kama Mwalimu Nyerere ninayemuamini saana ndio ngekua ametoa kuli kama hii. Ingawaje utakua umesaidia sana kuwafariji wahusika kiaina ila kiama cha mfumo mzima wa kifisadi uko pale pale hivyo hata kama kiongozi wangu wa CHADEMA (wewe mwenyewe ukiwemo) atathibitika kuwa ni sehemu ya ukwapaji huo basi itakua ndio hivyo tena ...!!!

Mwisho, kama kuna kitu kinachonifanya siku zote kuwapenda viongozi weengi sana ndani ya CHADEMA basi ni kule kuwa na ujasiri wa kutoa KAULI NYOOFU usiopinda pinda kiasi cha kuweza kuzalisha maana zaidi ya moja juu ya mada ile ile au kule kutafuta kufurahisha pande zote tatu za sarafu.

*Zitto adai Serikali imejitia kitanzi

NA Waandishi Wetu, jijini Habari Leo

MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameibuka na kusema kitendo kinachofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa watendaji wake
kutakiwa kujivua gamba kinaweza kuathiri utendaji wa Serikali.

Zitto amesema CHADEMA haioni kuwa kitendo hicho kinaweza kukisaidia chama hicho kuwa na wanachama wasafi.

“Sidhani kama huo utaratibu unaweza kuwaondoa mafisadi bali (1) kunaweza kuathiri utendaji wa Serikali kwa kuwaondoa viongozi wasio na makosa,” amesema Zitto.

Amesema kwa kuwa wapinzani wakubwa wa CHADEMA ni CCM, wamedhamiria kukaa pembeni na kuangalia ni kitu gani kitafuatia.

Zitto amesema (2) suala la ufisadi ni jukumu la mtu binafsi kuamua kuachana na suala hilo na si la kushinikizwa.

“Hivi sasa CHADEMA inaangalia mechi hiyo ili kuweza kufahamu itakwishaje na ndio maana tumekaa pembeni kuwaangalia hawa wapinzani wetu wakubwa,” amesema Zitto.

Zitto amesema (3) chama chake kitaendelea kuwa mstari wa mbele kwa kuhakikisha kuwa suala la ufisadi linakomeshwa nchini.

Amesema bado (4) suala hilo linahitaji nguvu zaidi kwa kuwa baadhi ya maeneo kumejengeka mizizi ambayo inahitaji kung'olewa.

“Hii mizizi inahitaji kung'olewa hivyo kama wananchi wataamua kufanya hivyo itawalazimu kwanza kukubaliana na CHADEMA kwa kukipa nguvu zaidi katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu,” amesema Zitto.
 
MHESHIMIWA ZITTO NAKUOMBEA KWA MUNGU AKUJALIE TENA ULE UJASIRI WA ZAMANI WA KUNYOOSHA KAULI JUU YA MASUALA NYETI NA YENYE MASLAHI YA UMMA KITAIFA

Zitto Zuberi Kabwe,

Naomba sana tukubaliane kutofautiana kidogo katika baadhi ya kauli ulizozitoa humu.

Kwanza, endapo kilichoandikwa ni maneno yako kweli basi nikatae hapa kwamba JANGA LA UFISADI (kauli ya kwanza hapo chini) si suala la Mtu binafsi na kwamba akaachwe tu kule kujipima mwenyewe na kuhiari njia gani akajipitie.

Sababu yangu kuamini hivyo ni kwamba kodi zinazosadikiwa kukwapuliwa na watuhumiwa wa UFISADI ulikua ni mali ya Umma kwa ujumla wetu hivyo kufanya suala zima hapa kuwa na Maslahi ya Jamii nzima ya Tanzania.

Hivyo watuhumiwa wa ndani ya CCM na serikali yake wakimaliza KUBEMBELEZANA KUJIUZULU huko katika kifindi cha siku 90 basi sisi Nguvu ya Umma tutalazimika kuchukua hiyo kesi kuja kwenye mahakama yetu ili kama waathirika wa janga hilo, ukwapwaji wa kila mara ya kodi zetu na kudidimiziwa maendeleo, ili tukalitolee maamuzi sahihi na ya kudumu.

Pili, kwa kuzingatia ukweli kwamba zao 'Pamba' kamwe haiwezi kufifia hata kidogo ueupe wake endapo wakati wote halikukutana na uchafu wowote popote pale, basi hata watumishi wetu serikalini uliowataja kama 'Wasio na Makosa' nao kamwe hawawezi kupigwa dhoruba yoyote ile ya fagio la chuma kuondoa ufisadi kwenye mfumo wetu kama hawakuwahi kushiriki UFISADI au kusaidia jambo hilo kutokea.

Kwa msingi huo, aheri tubaki na watumishi wawili waaminifu katika kila idadi 1000 ili nafasi hizo 998 zikatangazwe kwa utaratibu mpya, kuzingatia miiko ya uongozi ndani ya Azimio la Arusha na sheria na vyombo vya usimamizi kuimarishwa maradufu kuzuia kabisa hali hiyo. Endapo mtapenda kujua 'njia zipi zitumike mara baada ya hapo' basi mkatuulize hapa JF - tutatoa mkakati kiboko ambayo hakuna atakayeamini wengine tumeikalia tu kimya hapa kwa kuwa hata siku moja hatupewi nafasi tu.

Tatu, yeyote atakayekua amesoma na kutafakari vema kauli yako namba moja na mbili bila shaka atakua amebaki ameduazwa bila kuelewa kama aliyetoa na kauli ya tatu na ya nne bado ni mtu yule yule AU NI NAFSI YA KUTOKEA wakati zile kauli mbili za mwazo zilitoka kwa NAFSI YA KUSHINDIA ndani mwake mtu yule yule mmoja.

Hiyo hali ya mkanganyiko unatokana na ukweli kwamba tayari umetoa Judgment kwamba Mtanzania yeyote ni ruksa tu kuwaibia wenzake ilmradi tu kipenyo kinapatikana kwaki kama kiongozi wa ngazi fulani hivi ila pale suala la kuwajibika kubeba mshahara wa dhambi hiyo basi sasa Wa-Tanzania wenye kuibiwa kamwe hawana nafasi kumtaka MKWAPWAJI YEYOTE kubeba msalaba wake mpaka jambazi huyo tu akiamka vizuri ndio akajionelee kama ni vema akaturejeshee kilichoibwa au ajiuzulu au asijishughulishe kabisa na lolote lile.

Mhe Zitto, hili nalipinga hata kama Mwalimu Nyerere ninayemuamini saana ndio ngekua ametoa kuli kama hii. Ingawaje utakua umesaidia sana kuwafariji wahusika kiaina ila kiama cha mfumo mzima wa kifisadi uko pale pale hivyo hata kama kiongozi wangu wa CHADEMA (wewe mwenyewe ukiwemo) atathibitika kuwa ni sehemu ya ukwapaji huo basi itakua ndio hivyo tena ...!!!

Mwisho, kama kuna kitu kinachonifanya siku zote kuwapenda viongozi weengi sana ndani ya CHADEMA basi ni kule kuwa na ujasiri wa kutoa KAULI NYOOFU usiopinda pinda kiasi cha kuweza kuzalisha maana zaidi ya moja juu ya mada ile ile au kule kutafuta kufurahisha pande zote tatu za sarafu.
Ni uchambuzi makini (Great thinker)
 
*Zitto adai Serikali imejitia kitanzi

NA Waandishi Wetu, jijini Habari Leo

MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameibuka na kusema kitendo kinachofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa watendaji wake
kutakiwa kujivua gamba kinaweza kuathiri utendaji wa Serikali.

Zitto amesema CHADEMA haioni kuwa kitendo hicho kinaweza kukisaidia chama hicho kuwa na wanachama wasafi.

“Sidhani kama huo utaratibu unaweza kuwaondoa mafisadi bali kunaweza kuathiri utendaji wa Serikali kwa kuwaondoa viongozi wasio na makosa,” amesema Zitto.

Amesema kwa kuwa wapinzani wakubwa wa CHADEMA ni CCM, wamedhamiria kukaa pembeni na kuangalia ni kitu gani kitafuatia.

Zitto amesema suala la ufisadi ni jukumu la mtu binafsi kuamua kuachana na suala hilo na si la kushinikizwa.

“Hivi sasa CHADEMA inaangalia mechi hiyo ili kuweza kufahamu itakwishaje na ndio maana tumekaa pembeni kuwaangalia hawa wapinzani wetu wakubwa,” amesema Zitto.

Zitto amesema chama chake kitaendelea kuwa mstari wa mbele kwa kuhakikisha kuwa suala la ufisadi linakomeshwa nchini.

Amesema bado suala hilo linahitaji nguvu zaidi kwa kuwa baadhi ya maeneo kumejengeka mizizi ambayo inahitaji kung'olewa.

“Hii mizizi inahitaji kung'olewa hivyo kama wananchi wataamua kufanya hivyo itawalazimu kwanza kukubaliana na CHADEMA kwa kukipa nguvu zaidi katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu,” amesema Zitto.
.


Sidhani kama CCM haina uwezo wa kuwadhibiti hawa,tatizo ni uthubutu tu.Chama hiki kimewahi kufanya maamuzi mazito tena kwa kiongozi wa ngazi ya Urais mwaka 1984 mbona Serikali,chama wala nchi haikuyumba,vivyo hivyo mwaka 1988.

Hakuna mwenye nguvu zaidi ya serikali na umma.Lowassa kama ndio anaonekana tishio kumuondoa basi hiki chama kitakuwa ni dhaifu na hivyo Kikwete nae itabidi ajiandae kusafiri kama alivyofanywa Thabo Mbyelwa Mbeki na bado ANC ika survive na wala si Kwa Zulu Inkhata.

Zitto nadhani aachane na fikra za staki nataka,kwani hakutoa suluhisho la nini kifanyike juu ya hawa Mafisadi.Any way kufa kwa CCM kwake na chama chake ni sherehe.
 
Back
Top Bottom