Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
*Wasema Hoja zake zimezingatia sheria si porojo za siasa
*Wakerwa na wasomi wanafunzi kubeza maoni yake
Na Mwandishi Wetu
SIKU moja baada ya waliojiita wanafunzi wa kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, Profesa Mwesiga Baregu kupinga maoni ya aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Mark Bomani kuhusu malipo ya Kampuni ya Dowans, wanasheria kadhaa jijini Dar es Salaam wamemuunga mkono na kusisitiza kuwa maoni hayo ni sahihi kwani yamezingatia mtazamo wa kisheria.
Wakizungumza na gazeti hili kwa sharti la majina yao kutoandikwa, wanasheria hao kwa nyakati tofauti jana walisema kwa mujibu wa sheria, kauli ya Jaji Bomani katika mahojiano maalum na gazeti hili juzi ni sahihi na kwamba alitumia uzoefu wake kisheria na huo ndio ukweli kuhusu malipo hayo.Ukiangalia ukweli wa kisheria hoja zote alizozungumza
Jaji Bomani kuhusu uhalali wa malipo ya Dowans na madhara yanayoweza kuikumba nchi endapo itakataa kulipa ni sahihi. Mimi kama mwanasheria mzoefu namuunga mkono, hawa wanaojaribu kupinga hoja zake
naamini bado wachanga kisheria.
Malipo ya Dowans kwa vigezo alivyotoa Jaji Bomani hayakwepeki japo waliohusika katika mkataba lazima wachukuliwe hatua,alisisitiza mwanasheria mmoja wa kujitegemea jijini Dar es Salaam.
Alisisitiza kuwa iwapo hukumu ya kesi dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi ya Migogoro ya Kibiashara (ICC) ilitolewa na watu wenye sifa, Tanzania haiwezi kukwepa kuilipa Dowans kwa kutumia mabavu.
Alishauri Watanzania kuacha ushabiki na kupoteza muda katika suala hilo badala yake watafute ufumbuzi wa tatizo la umeme kwani umeme si suala la kisiasa bali linagusa uchumi na maendeleo ya nchi.
Kumshambulia Jaji Bomani si sahihi, hoja alizotoa ni za kitaalamu zenye mtazamo wa kisheria. Maoni ya Jaji Bomani yanapaswa kuheshimiwa kwani kama mtaalamu na mkongwe wa fani ya sheria ana haki kutoa maoni yake kwa kuzingatia uzoefu wake, huyu ni mwanasheria anazungumza kwa kuitazama sheria si porojo za kisiasa, alisema wakili mwingine jijini Dar es Salaam na kusisitiza kuwa sheria ni utaalamu si ushabiki.
Aliwashambulia waliojiita wanafunzi wa sheria mwaka wa tatu kwa kauli zao dhidi ya Jaji Bomani na kueleza kuwa wamekosa hoja kwani walipaswa kujibu kwa misingi ya hoja alizotoa Jaji Bomani badala ya kutoa majibu yasiyo na mantiki hatua inayoshusha hadhi na usomi wao.
Naye Jaji Bomani akizungumza na gazeti hili jana, alieleza kusikitishwa na watu wanaomshambulia katika maoni yake kwa kutanguliza ushabiki bila kuzingatia ukweli na mantiki
ya kisheria.
Mimi nilitoa maoni yangu kama mwanasheria mzoefu, Jaji na Mwanasheria Mkuu mstaafu wa Serikali kwa kuzingatia sheria za nchi na za kimataifa na kwa maslahi ya heshima ya nchi katika jumuiya ya kimataifa. Sikutoa maoni hayo kisiasa kama wengi wanavyofanya. Inasikitisha kuwa tumefikia mahali hata mtu hawezi kutoa maoni yake bila kupachikwa maneno ya ovyo ovyo. Mimi ni mwanasheria ninayeheshimika haijawahi na haitatokea kurubuniwa na mtu yeyote. Inasikitisha sana, alisema Jaji Bomani.
Hivi karibuni katika mahojiano yake na gazeti hili, Jaji Bomani alisema kisheria malipo ya Dowans hayakwepeki kinyume na hapo taifa litaingia kwenye matatizo makubwa zaidi.Akaeleza kuwa ni vigumu Mahakama Kuu kutengua hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC Court) kama hakukuwa na kasoro zozote katika utoaji hukumu hiyo.
Kwa kesi za usuluhishi kama hii hukumu hii inaweza kutenguliwa tu kama hao wapatanishi hawakuwa na sifa za kuwa wapatanishi kitu ambacho hapa hakiwezi kutumiwa kwa kuwa katika suala hili, hawa walikubaliwa na pande zote, alikaririwa akisema Jaji Bomani na kuongeza;
Hukumu hii inaweza kutenguliwa tu kama ikidhihirika kwamba wamepewa rushwa kwa kutoa hukumu ya namna hiyo. Vinginevyo Mahakama Kuu haijihusishi na kuingilia kesi yenyewe. Mimi kwa upande wangu kama nilivyokwisha kusema siku za nyuma jambo hili liishe ili mitambo hiyo itumike hapa nchini kuzalisha umeme tuondokane na hali ya mgawo na upungufu wa umeme na hilo ndilo jambo muhimu kwa uchumi wa nchi.
Jaji Bomani aliyetumikia nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kati ya mwaka 1965- 1976 akirithi wadhifa huo kutoka kwa mwingereza Bw. Roland Brown,alisisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, haoni sababu za kukwepa kulipa fidia hiyo na kushauri kuwa kilichopo sasa ni kuzungumza na hao wanaodai ili kufikia muafaka wa namna ya malipo hayo.
Alishauri kuwa kukataa kulipa kimabavu si sahihi hivyo serikali inapaswa kutafakari kwa makini jambo hilo kabla ya kufikia maamuzi.
Alionya kwamba endapo serikali itatumia mabavu kugoma kulipa na Dowans ikasajili hukumu ya kesi hiyo nje ya Tanzania, kisheria kampuni hiyo inaweza kupewa uwezo kukamata mali za serikali huko ziliko.
Novemba 15 mwaka jana,Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara ilipitisha hukumu dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuilipa Dowans fidia ya sh. bilioni 94 kutokana na kuvunja mkataba.
*Wakerwa na wasomi wanafunzi kubeza maoni yake
Na Mwandishi Wetu
SIKU moja baada ya waliojiita wanafunzi wa kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, Profesa Mwesiga Baregu kupinga maoni ya aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Mark Bomani kuhusu malipo ya Kampuni ya Dowans, wanasheria kadhaa jijini Dar es Salaam wamemuunga mkono na kusisitiza kuwa maoni hayo ni sahihi kwani yamezingatia mtazamo wa kisheria.
Wakizungumza na gazeti hili kwa sharti la majina yao kutoandikwa, wanasheria hao kwa nyakati tofauti jana walisema kwa mujibu wa sheria, kauli ya Jaji Bomani katika mahojiano maalum na gazeti hili juzi ni sahihi na kwamba alitumia uzoefu wake kisheria na huo ndio ukweli kuhusu malipo hayo.Ukiangalia ukweli wa kisheria hoja zote alizozungumza
Jaji Bomani kuhusu uhalali wa malipo ya Dowans na madhara yanayoweza kuikumba nchi endapo itakataa kulipa ni sahihi. Mimi kama mwanasheria mzoefu namuunga mkono, hawa wanaojaribu kupinga hoja zake
naamini bado wachanga kisheria.
Malipo ya Dowans kwa vigezo alivyotoa Jaji Bomani hayakwepeki japo waliohusika katika mkataba lazima wachukuliwe hatua,alisisitiza mwanasheria mmoja wa kujitegemea jijini Dar es Salaam.
Alisisitiza kuwa iwapo hukumu ya kesi dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi ya Migogoro ya Kibiashara (ICC) ilitolewa na watu wenye sifa, Tanzania haiwezi kukwepa kuilipa Dowans kwa kutumia mabavu.
Alishauri Watanzania kuacha ushabiki na kupoteza muda katika suala hilo badala yake watafute ufumbuzi wa tatizo la umeme kwani umeme si suala la kisiasa bali linagusa uchumi na maendeleo ya nchi.
Kumshambulia Jaji Bomani si sahihi, hoja alizotoa ni za kitaalamu zenye mtazamo wa kisheria. Maoni ya Jaji Bomani yanapaswa kuheshimiwa kwani kama mtaalamu na mkongwe wa fani ya sheria ana haki kutoa maoni yake kwa kuzingatia uzoefu wake, huyu ni mwanasheria anazungumza kwa kuitazama sheria si porojo za kisiasa, alisema wakili mwingine jijini Dar es Salaam na kusisitiza kuwa sheria ni utaalamu si ushabiki.
Aliwashambulia waliojiita wanafunzi wa sheria mwaka wa tatu kwa kauli zao dhidi ya Jaji Bomani na kueleza kuwa wamekosa hoja kwani walipaswa kujibu kwa misingi ya hoja alizotoa Jaji Bomani badala ya kutoa majibu yasiyo na mantiki hatua inayoshusha hadhi na usomi wao.
Naye Jaji Bomani akizungumza na gazeti hili jana, alieleza kusikitishwa na watu wanaomshambulia katika maoni yake kwa kutanguliza ushabiki bila kuzingatia ukweli na mantiki
ya kisheria.
Mimi nilitoa maoni yangu kama mwanasheria mzoefu, Jaji na Mwanasheria Mkuu mstaafu wa Serikali kwa kuzingatia sheria za nchi na za kimataifa na kwa maslahi ya heshima ya nchi katika jumuiya ya kimataifa. Sikutoa maoni hayo kisiasa kama wengi wanavyofanya. Inasikitisha kuwa tumefikia mahali hata mtu hawezi kutoa maoni yake bila kupachikwa maneno ya ovyo ovyo. Mimi ni mwanasheria ninayeheshimika haijawahi na haitatokea kurubuniwa na mtu yeyote. Inasikitisha sana, alisema Jaji Bomani.
Hivi karibuni katika mahojiano yake na gazeti hili, Jaji Bomani alisema kisheria malipo ya Dowans hayakwepeki kinyume na hapo taifa litaingia kwenye matatizo makubwa zaidi.Akaeleza kuwa ni vigumu Mahakama Kuu kutengua hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC Court) kama hakukuwa na kasoro zozote katika utoaji hukumu hiyo.
Kwa kesi za usuluhishi kama hii hukumu hii inaweza kutenguliwa tu kama hao wapatanishi hawakuwa na sifa za kuwa wapatanishi kitu ambacho hapa hakiwezi kutumiwa kwa kuwa katika suala hili, hawa walikubaliwa na pande zote, alikaririwa akisema Jaji Bomani na kuongeza;
Hukumu hii inaweza kutenguliwa tu kama ikidhihirika kwamba wamepewa rushwa kwa kutoa hukumu ya namna hiyo. Vinginevyo Mahakama Kuu haijihusishi na kuingilia kesi yenyewe. Mimi kwa upande wangu kama nilivyokwisha kusema siku za nyuma jambo hili liishe ili mitambo hiyo itumike hapa nchini kuzalisha umeme tuondokane na hali ya mgawo na upungufu wa umeme na hilo ndilo jambo muhimu kwa uchumi wa nchi.
Jaji Bomani aliyetumikia nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kati ya mwaka 1965- 1976 akirithi wadhifa huo kutoka kwa mwingereza Bw. Roland Brown,alisisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, haoni sababu za kukwepa kulipa fidia hiyo na kushauri kuwa kilichopo sasa ni kuzungumza na hao wanaodai ili kufikia muafaka wa namna ya malipo hayo.
Alishauri kuwa kukataa kulipa kimabavu si sahihi hivyo serikali inapaswa kutafakari kwa makini jambo hilo kabla ya kufikia maamuzi.
Alionya kwamba endapo serikali itatumia mabavu kugoma kulipa na Dowans ikasajili hukumu ya kesi hiyo nje ya Tanzania, kisheria kampuni hiyo inaweza kupewa uwezo kukamata mali za serikali huko ziliko.
Novemba 15 mwaka jana,Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara ilipitisha hukumu dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuilipa Dowans fidia ya sh. bilioni 94 kutokana na kuvunja mkataba.