Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Ule msimu wa kuchipua hatimaye umeanza kwa wabeba maboksi. Hivyo jua limeanza kutoka na kuifanya hali ya hewa isiwe ya baridi. Mabinti nao wameanza kuvaa nguo fupi kupita kiasi. Ukiwaona mitaani utadhani hawakuwepo wakati wa msimu wa kipupwe. Swali la kujiuliza ni nini hasa saikolojia inayofanya wanawake wa rangi zote wavae nguo fupi kiasi hiki? Je, ni fasheni? Au ni kwa ajili ya kuvutia macho ya wanaume? Pengine ni raha na uhuru mwili ukiwa wazi?