Ni kweli mkuu, siku zote giza halifukuzi giza ila mwanga ndo huondoa giza, Hata kama Ghadafi kauwa suluhisho sio kuua wanae au kumuua yeye, wamarekani wataifanya Libya kuwa Afghanistan ya Africa, maana wakishamwondoa Ghadaf watataka wachimbe mafuta na baadhi ya walibya wataweka ngumu, hapo ndo watakapoanza kuchinjana na maisha yatakuwa magumu hadi watamkumbuka wanayemwita dikteta sahivi.Me si kwamba nimeumizwa na yeye tu eti kwa kuwa ameuawa. Muda wote sipendi mauaji yoyote. I always say no to war!
Hata kama Gaddafi ni mbaya na muuaji kiasi gani hukumu yake sio kuuwa watoto wake ambao hawana hatia.
Hata kama Gaddafi ni mbaya kiasi gani anapaswa kufikishwa mbele ya sheria , nani dunia hii ameua watu wengi kama George Bush? mbona hawakumvamia ?
Africa wanapaswa kuwa pamoja kwenye hili, kwani huu ni uonevu .
Hivi Gaddafi kapona? mbona hawajasema zaidi ya jana kusema kuwa alikuwa kwenye nyumba hiyo na mpaka sasa haijaelezwa kama yupo hai au naye alikufa na kama hakufa lazima atakuwa aliumia anatibiwa wapi?
Mara baada ya taarika kusema kuwa mtoto wa Gadafi ameuwawa na Nato,wengi wetu wamefurahi
Binafsi nayalaani kama ambavyo nililaani uvamizi wa kihuni,kwa yeyote anayeitakia mema Africa hawezi kushabikia uvamizi na mauaji haya ya mtoto wa Ghadafi na raia wa Libya,kimsingi Nchi za magharibi hazina mapenzi ya kweli na Africa,wanachotaka ni mafuta ya Libya na rasilimali nyingine,kama Ghadafi angeondolewa na nguvu ya umma basi nisingekuwa na neno,hili la kuruhusu uvamizi,na kuuwawa kwa nchi huru kamwe sitalikubali.Historia itatuhukumu
Kwanza hata huyo mtoto wa Gaddafi anaitwa Saif al-Arab siyo Saif al-Africa....Kama kumtetea Gaddafi inabidi iwe ni kwa sababu ya matendo yake na si kwasababu eti ni Mwafrika! Kama matendo yake ni sahihi atatetewa si na waafrika tu bali na wana-waulimwengu wote.
Duh! yaaani wewe ndio unamjua Ghadafi vizuri sio,au chuki inayotokana na stori zenu za katika vijiwe vya kahawa ndio inayokusumbua?Na hakika hata wewe umjui ghadafi.
Napongeza sana NATO!
Hivi mwezi uliopita wakati Gadaffi anauwa watoto wa wenzake ulikuwa hujajiunga JF je ulianzisha thread au topic yeyote kulaani mauaji hayo kwani wale watoto walikuwa hawana wazazi acheni unafiki wenu. Nafikiri haumjui Gadaffi tuulize tuliokwenda Mtukula miaka ya 70 kupigana na waarabu wa Libya wakitaka kuchukua ardhi yetu.Naona watanzania tumeamua kushabikia tu, Toka lini NATO wakawa watetezi wa wanyonge, acha tuonyeshane ujuzi wa kutype tu humu jamiiforums, lakini ukweli NATO wanajua walichokifuata Libya na itadhihirika baada ya kumwondoa Ghadafi ingawa wengi mnajifanya hamuelewi.
Chukua mfano wa Ivory coast watu wangapi wamekufa mbona NATO hawakwenda, Sudan wamekufa wangapi umesikia NATO wako kule, hata Somalia hadi leo haitawaliki watu wanakufa huwezi sikia NATO wameenda.
Watu wengi humu jamvini wanaolaani mauaji ya huyo dogo hawasemi kwamba Ghadafi anapoua ni sawa no, kuua ni kuua iwe Ghadaf kaua au mwanae ameuawa siyo sawa, siku zote haki haitafutwi kwa kuvunja haki nyingine, kama tunaona alichofanya Ghadaf sio sawa kwa nini kitu hicho hicho kikifanywa na NATO kiwe sawa?
Mara baada ya taarika kusema kuwa mtoto wa Gadafi ameuwawa na Nato,wengi wetu wamefurahi
Binafsi nayalaani kama ambavyo nililaani uvamizi wa kihuni,kwa yeyote anayeitakia mema Africa hawezi kushabikia uvamizi na mauaji haya ya mtoto wa Ghadafi na raia wa Libya,kimsingi Nchi za magharibi hazina mapenzi ya kweli na Africa,wanachotaka ni mafuta ya Libya na rasilimali nyingine,kama Ghadafi angeondolewa na nguvu ya umma basi nisingekuwa na neno,hili la kuruhusu uvamizi,na kuuwawa kwa nchi huru kamwe sitalikubali.Historia itatuhukumu
Hivi mwezi uliopita wakati Gadaffi anauwa watoto wa wenzake ulikuwa hujajiunga JF je ulianzisha thread au topic yeyote kulaani mauaji hayo kwani wale watoto walikuwa hawana wazazi acheni unafiki wenu. Nafikiri haumjui Gadaffi tuulize tuliokwenda Mtukula miaka ya 70 kupigana na waarabu wa Libya wakitaka kuchukua ardhi yetu.