Mkulima wa Kuku
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 1,270
- 533
Well, kwa waandishi wa habari wanachojaribu kupigia kelele kwa sasa ni kauli ya "mkuki kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu". Ndugu zanguni hakuna binadamu atakayesalimika anapoachia uovu upite naye amekaa kimya kwa sababu yoyote ile. Iwe ni maslahi toka kwa watawala waliopo au iwe ni chuki binafsi dhidi ya anayefanyiwa unyama. Nionacho mimi mkuki huu kule Morogoro alipigwa nguruwe ndiyo maana waandishi hawakupiga kelele kiasi hiki huku wakijua ukweli wa mambo. Lakini kwa Nyololo kapigwa binadamu ndiyo maana kelele ni nyingi. Tumezoea kuona waandishi wakipokea vijibahasha kwenye mikutano (press conference) kisha aidha kunyamazia ukweli fulani au kuupindisha sababu ya vibahasha hivyo. Walidhani watasalimika wakiendelea kukaa kimya. Sasa leo wanyamazishaji wametafuta wa kunyamaziha hawamuoni wamewageukia "washikaji" wa siku zote. Sasa huu ni wito kwa waandishi kutonyamazia ukweli wauonapo bila ya kujali nani anaonewa, vinginevyo tunawaweka waandishi kwenye kundi moja na watawala dhalimu