Said Bakhressa aanza kuwasogelea wanasiasa

Buyaka

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
1,643
1,786
IM929.jpg

Bakhressa akimpa Rais ''zawadi"



IM960.jpg


Bakhressa akimsomesha Rais



IM991.jpg


Rais Shein akifungua biashara ya Bakhressa


Wadau, wakati nchi bado ina kumbukumbu za karibu za vifo vya Watanzania kwa kupinduka kwa meli ambapo serikali ilibeba lawama ya kutokusimamia kanuni, taratibu na sheria za uendeshaji wa vyomo vya majini, serikali kupitia Rais wa Zanzibar, imekimbilia kwenda kukata utepe kufungua biashara ya mtu . Nchi za wenzetu ni vigumu sana kumpata Rais kwenda kufungua biashara ya mtu.

Serikali isilale kitanda kimoja na wafanyabiashara, iwakunjie uso wamiliki ili iweze kuwaratibu,
sio kupewa "zawadi" na kuwachekea chekea.

Je ni alama ya kuja kuchafuka kwa the last don of Tanzania business elite, Said Salim Bakhressa?
 
Hawana pa kukwepa!! hao ndiyo wafadhili wa kila kitu mkuu!! serikali imebaki kuomba omba kila kitu hata kile inachoweza kukipata kwa kusimamia kanuni na taratibu, nacho kimeshindikana!!
 
Hivi simbion power ni ya serikali ya marekani. Nafikiri mfanyabiashara mkubwa kama SSB haitaji tu support ya wanasiasa bali wananchi wote wazalendo, kwani licha ya kutoa ajira ndo anatulisha daily.
 
Hivi simbion power ni ya serikali ya marekani. Nafikiri mfanyabiashara mkubwa kama SSB haitaji tu support ya wanasiasa bali wananchi wote wazalendo, kwani licha ya kutoa ajira ndo anatulisha daily.

Pia ifike wakati serikali inapotaka kuingia mikataba na wawekezaji hasa wa nje wawaalike wafanyabiashara wa aina ya S.S.B in negotiations kuliko hawa maofisa wa serikali pekee ambao hata biashara ya kiosk hajawahi wala hawezi kuiendesha
 
Hii ni hulka ya wanasiasa wa Zanzibar, kwani mmesahau aliyemtajirisha huyu jamaa? si Mzee Ruksa
 
popote pale penye ubepari, mfanyabiashara/tajiri anamremote mwanasiasa
 
Hivi simbion power ni ya serikali ya marekani. Nafikiri mfanyabiashara mkubwa kama SSB haitaji tu support ya wanasiasa bali wananchi wote wazalendo, kwani licha ya kutoa ajira ndo anatulisha daily.
Unamaanisha nini hapo kwenye bold mkuu?
 
Pointi yangu ni hii: Kwanza, sipendi kuona wafanyabiashara wanajisogeza kwa wanasiasa, inaleta harufu ya influence peddling and corruption. Bakhressa ameni dissapoint.

Pili, kwa upande wa serikali, si vizuri kwa Rais na serikali kujikita katika kukata tepe za kufungua biashara za watu binafsi. Kwa nini? Kwa sababu serikali inategemewa iwasimamie wafanyabiashara kuhakikisha wanatafa taratibu na sheria. Serikali inapopokea zawadi kutoka kwa mfanyabiashara hii inaleta aina ya mgongano wa kimaslahi. Mtu anakupa zawadi utamwambia nini?

Katika mazingira ambayo kila uchwao vyombo vya kusafiria vinaua raia kama vita vya dunia sitegemei Rais wa Zanzibar mara hii ameshasahau ya kuchunguza ajali ya MV Spice Island anaende kufungua li-meli lingine, mwache Bakhressa mwenyewe afungue meli lake. Wewe simamia taratibu za kisheria katika biashara hiyo, sio akupe zawadi umkatie utepe.

Sasa kwenye hilo kabrasha Rais Shein kafungiwa nini, suti?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom