Saga atcl-nyanganyi akabidhi ripot kwa waziri!!!

capuchino

Member
Jun 27, 2008
47
0
ATCL wawakilisha sababu za kuharibikiwa
Mwandishi Wetu
Daily News; Friday,December 19, 2008 @21:15

Habari nyingine
ATCL wawakilisha sababu za kuharibikiwa
Mpigapicha wa Channel Ten aagwa
TSN watoa msaada wa kompyuta
‘Zimbabwe isaidiwe kukabili kipindupindu’
Mgonja kula sikukuu uraiani
Basi laua polisi watatu
Bilioni 40 /- za mafisadi zanufaisha wakulima
Bodi ya ATCL matatani
Ujenzi wa barabara mpya Dar waiva
Dhamana ya Mgonja yakamilika

Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), imewasilisha kwa Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu ripoti ya maelezo ya kwa nini kampuni imefika hatua mbaya baada ya kupewa siku saba za kujieleza.

Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Balozi Mustafa Nyang’anyi aliliambia gazeti hili jana kuwa siku saba walizopewa na Waziri Dk. Shukuru Kawambwa zilianza Jumatatu na zinamalizika kesho, lakini walikamilisha kabla na tayari wameiwasilisha kwake.

Dk. Kawambwa juzi katika mkutano na waandishi wa habari, alisema ameipa bodi siku saba ieleze ni kwa nini ATCL imefikia kufungiwa na kuahidi kuwa baada ya maelezo hayo wale wote watakaobainika kuhusika atawawajibisha ipasavyo.

Katika mahojiano na gazeti hili jana kuhusu hali ya kampuni hiyo na matakwa ya wafanyakazi wa ATCL ya kumtaka ajiuzulu pamoja na Menejimenti inayoongozwa na Mkurugenzi, David Mattaka, Balozi Nyang’anyi alisema kujiuzulu kwake si tatizo, anaweza kufanya hivyo, lakini tatizo ni mtaji mdogo wa kuendesha kampuni hiyo.

“Unadhani tatizo ni kujiuzulu? Watu hawajui tulikuwa tukijiendesha vipi kwa kipindi chote cha miaka miwili, tuliomba mtaji kwa serikali wa US dollar milioni sabini na sita (takribani Sh bilioni 91.2) kuendesha kampuni, lakini kutokana na kuwa serikali nayo haina fedha, tumekwama mpaka leo,” alisema Nyang’anyi.

Alisema hata hivyo waliandika maombi ya kupatiwa fedha kwa ajili ya kutafuta na kuchagua wataalamu wa kusaidia uendeshaji wa kampuni wenye ujuzi wa kiwango cha juu, lakini ukosefu wa fedha ulisababisha baadhi ya kampuni ikiwa ni pamoja na yaliokuwa yakiandika nyaraka ya ndege mpya ya Air Bus na DASH8-Q300 kushindwa kuendelea kwani zilihitaji Euro 360,000.

Alisema hata hivyo wanaendelea na juhudi za kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanapata mshahara wa Desemba kwa wakati hata kama kampuni hiyo haizalishi na kwamba viwango vya kukidhi kumaliza dosari zilizoainishwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) vinatarajia kukamilika.

Kuhusu hatua za serikali kuinusuru ATCL kwa kuiongezea mtaji, alisema ni bora na italeta manufaa makubwa endapo ikitekelezeka kwa haraka. Aidha, taarifa zilizopatikana jana kutoka wizarani zilieleza kuwa Waziri Kawambwa alikutana na viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na Uchukuzi, COTWU jana kwa ajili ya kuzungumzia hatua za serikali kwa madai yao na kuhakikishiwa mishahara kwa wakati.
 
Mod naomba tuiache kwa muda tupate maoni ya watu na pengine waio karibu na huko atcl...kujua ukweli halisi....
 
Kwako ndugu nyanganyi,nahisi imefika wakati watu kusema inatosha mzee na kama ulivyosema kujiuzulu sio tatizo nafikiri ni tatizo kubwa sana kwako na management yako...

kwanza kwa hali kama hii kwa nchi za watu tunaanza na waziri husika ,lakini kutokana na uswaiba anakuita ofisini na kuwapa chai ya maziwa ya bure na kukuomba siku saba akujua we ni mwanasiasa msanii uliebobea kwako siku saba zilikuwa kama siku moja ,kama bwana masha alivyoambiwa na mengi akaishia na aibu yake ofisini na kwenye bar.....nasema hivi kwa msaada wa watanzania na wafanyakazi wote wa hapo ATCL..

kabla ya kuondoka nililia sana na kuishia kutishiwa na viongozi wako watanirudisha kijijjini bila kujua mola ndie ajuae wapi tunaelekea,mzee wangu tulionglea yote na kutoa tahadhahari ya yote haya ,....lakini hakuna aliesikia wala kuambiwa na mtu yoyote,,kitu kimoja kabla ya kukujibu napenda kukwambia ATCL kwa bahati mbaya wakati huuu imepata viongozi "

"JEURI-wenye DHARAU na WASIOTAKA KUMISIKIA YOYOTE"

Wakiongozwa na wewe mwenyekiti na kufuatiwa na CEO wako mh DAVID MATTAKA...kama mmngekuwa mnajua umuhimu wa wafanyakazi hapo atcl na kama mngejua bila wafanyakazi nanyie msingekuwepo hapo lah!!!haya yote yasingetokea....nilishamweleza sana hili bw DAViD kabla ya kuondoka nikampa na ushauri ndugu yangu {Dir}....e la hasha dharau ndio zimewaponza na matokeo yake hivi sasa mnaanza kulilia fedhwa kule hazina ili mzitumie vizuri
 
nimesoma hapo juu nakusikitika sana maana hii ndio ulikuwa wimbo wenu kabla ya kuondoka mkapewa fwedha hazina mkazializa kwa safari na kugawana ...sasa limesimamisha naona mnashangilia na kuona huu ndio wakati muafaka wa kulazimisha pesa zitoke mkagawane lala salama vizuri....

Moja

..........Unadhani tatizo ni kujiuzulu? Watu hawajui tulikuwa tukijiendesha vipi kwa kipindi chote cha miaka miwili, tuliomba mtaji kwa serikali wa US dollar milioni sabini na sita (takribani Sh bilioni 91.2) kuendesha kampuni, lakini kutokana na kuwa serikali nayo haina fedha, tumekwama mpaka leo,” alisema Nyang’anyi"

Ans: Mh Nyanganyi...tunajua kwa mida mrefu ATCL ina tatizo la hela ...lakini naomba nikuulize hili shirika mna miaka miwili sasa ..unaweza kuonyesha hata budget ya kampuni kwa kila idara ya kampuni yako???ulikuwa unajua kampuni aina budget planning zaidi ya kusubiri siku mikisikia serikali inatoa hela mnakimbizana kukaa chini na kuandika wizi usiokubalika...na kijana wenu ELIACHAFU...

kitu kimoja napenda kukwambia mzee nyanganyi serikali si wapumbavu si wajinga kuotota pesa..kumbuka enzi za wazungu walikuwa wanatoa million 600 kila mwezi sasa hutumia akili..tatizo mlilolifanya pindi mnaingia mlikuta pesa kidogo serikali wakawaachia kuangalia utendaji wenu.

matokeo yake nitayaonyesha hapo chini..na hivyo kujua kumbe mpo pale kushibisha matumbo yenu na si mko kwa ajili ya kuendeleza kampuni.......kuna mambo matano ukiweza kunisaidia mh nyanganyi nafikiri hata serikali itakuwa na mawazo ya kutoa hela

Hii ni kampuni ya ndege inayojitegemea....je mnawezaje kufanya biashara ya ndege bila kuwa na bussiness plan??Unataarifa hata kweney sub dep za shirika lako ukiwaita wakupatie budget za dep watakuuzia sura zao????

2. Elezea ukweli achana na uswahiba nini kilichoisimamisha kampuni ya atcl..pesa aikuwa tatizo..swlai langu linakuja kama ni pesa ,,iweje mlipoitwa na tcaa mkaomba mpewe siku kumi mtakuwa mmeshamaliza
je hizo pesa mmezipata wapi??Na nijuavyo kama manuals huwa kun watu specific wa kazi hiyo na si kuchukua wau mtaani waje kuandika na kuwakilisha tcaa...watanzania tusidanganywe huyu bw aeleze ukweli...iweje waweze kupeleka hizo docs kwa siku kumi wakati wamepewa toka

Mwezi april wakikumbushiwa wamalizie....lazima watu wawajibishwe
shaka yangu mh nyanganyi ni hivi,,kama nilivyomsikia mkur wa tcaa aikuwa raisi kulisimamisha atcl.ila kulikuja na 2 opt ama tcaa wasimamishwe ama atcl..ndipo kilipoamuliwa kukatwa kichwa cha""yohana mbatizaji""atcl..ukweli utakusaidia zaidi hata kwenye maisha ya ndoa yako mh.....kumbuka unawadanganya watanzania si wafanyakazi wa atcl..laiti ningalikuwapo.....

3. mnasema mnaitaji hela tusaide kidogo kuelimisha umma

MH CEO moaka sasa ametumia zaidi ya shillingi million 100 kwa safari tu nje na ndani wacha anazochukua kila wiki kwa ajili ya mahitaji ya wikiendi ambazo hazingizwi kwenye mahesabu wala kukatwa mshahara wake...na ana mwaka mmoja na nusu je mtu huyu ukimpa miaka mitatu atatumia sh ngapi...unaweza kuiambia jamii tatizo la ATCL ni pesa kama mnatumia ovyo hivi???

MH Dir wa operation alitumia zaidi ya shillingi million 73 kukaa kule elsavador wafanyakazi walipiga sana kelele na ukataarifiwa ukaka kimya mpaka watu walipolifikisha kwa jakaya mkaamua kumtumia ujumbe arudi..wakati yeye akikaa kule kuna engineer alipelekwa kule na Dir wa tech MR FIDELIS TARIMO...huyu injinia mchaga mwenzake anaitwa ringo watu waliandika sana anafanya nini kule hakuna alierespond..amekaa miezi sita mnamlipa doller 350 kila siku ya mungu..

Swali langu mh nyanganyi wakati mnatumia ovyo mlikuwa hamjui ipo siku mafuta yataitaji pesa kulipiwa ili ndege iruke????je ni swala la serikali tena kuwapa mhadi pesa za mafuta ndege iruke hali mnapandisha abiria????

Wakati nakaribia kuondoka kuna kituko kikubwa cha mwaka kilitokea nikalalamika sana sana na vitisho vilipoanza hapo...kuna rubani mmoja alirusha ndege ya atcl...aliyowachukua wachezaji wa taifa kuelekea cameroon.....yule rubani ni dir wa operationakiwa kama dir alilazimisha apewe hela zote yeye then akirudi atwapa kilichobaki...

Serikali walitoa doller 125,750 hakuna hata cent iliobakizwa ama kuingia kwenye acc za tc..aliporudi alibakiza doller 3000 akaulizwa akasema matumiza yalikuwa makubwa ..risiti nilizingangania sana na na uhakika mpaka leo waliopo awajapewa risiti husika....mwenzake akaja kuwapeleka wachezaji wa taifa.....cape verde ikalipwa doller 130,000 usd..akangangania rubani achukue 30,000usd zitawatosha kwenda na kurudi

Wakati wanarudi jamani ilikuwa aibu uko vibosle wakina alex wa taifa stars ndio waliwaokoa marubani...kwa kuwalipia pesa za hotel......

Swali mh nyanganyi siku zote ukienda kukopa lazima ueleze utatumiaje ..ama ulizo kopa umetumiaje..wewe unawadanganya wananchi tatizo la atcl ni pesa ili serikali

wajichanganye kuwagawia muwaonyeshe cha moto....naombautusaidie kujibu haya matumizi ya pesa ovyo hivi yakiendelea hata mkipewa billion 200 unafikiri kutabaki kampuni??

Kuna ubadhirifu wa hali ya juu kwenye ununuzi wa NDEGE YA airbus..ukijaribu kushirikishwa na kushtuliwia na wasamaria wema jamani muendako siko kuna ndege za 260,000usd soko la dunia.kimya ukaziba masikio ukaka kimya na CEO wako..leo hii unajifanya kushangaa kwamba kumbe kungangania kule 360,000usd kuna watu wanapitishiwa pesa kila mwisho wa mwezi malipo yakiingia .....in USD.....

watu wamewajulisha una kampuni ya marubani iitwayo easyway..hii inawatrain marubani

matokeo yake wale RUBANI wasaidizi wanaletwa hapa wakiwa na msaa 250...kitu ambacho hata TCAA tukiwaambia walishiriki hawatakubali...huku kwenye malipo yao kuna

DIR anapokea zaidi ya doller 3000usd kwa mwezi .....sasa hizi pesa za serikali za nini mh??

MWISHO NASHAURI SERIKALI ISITOE PESA MPAKA WATAKAPOONDOKA HAWA VIONGOZI WALIOPO VINGINEVYO KUMEJAA WIZI MTUPU!!!
 
Capucino na Sweetbaby,

Ndugu zangu shukran sana kutufungua macho!..Taarifa zebu zimetulia sana na hakika moja ya ushauri mkuu kwa kiongozi yeyote, husema hivi - Ukitaka kujua ukweli wa mambo, kwanza jitazame mwenyewe!...
Nadhani Nyang'anyi ndicho alichoshindwa kufanya!
 
Tangu siku Mattaka ameteuliwa nilijua ATC itakufa maana alishindwa kuongoza PPF akaachishwa, PPF huhitaji kuwa creative maana tu wakati umelala na kuzila hela. ATC CEO lazima kichwa kiwe kimetulia na safu yako pia.

Haya Nyang'anyi nae tunajua alichofanya akiwa waziri wa mawasiliano na uchukuzi na lord rajipa mpaka akaondolewa. nafasi aloyokuja kupewa ya ubalozi kwa huruma ya mwinyi haihitahi akili na creative ni kula mbele kwa mbele na starehe.

sasa leo watu wa hivyo uwape kuongoza shirika ambalo lilikuwa linakufa watafanya nini cha ajabu zaidi ya kusema asante JK kutupalaji ambao tuliona umuishatutoka na tulisha anza kuusahau.
 
Boma,
Mkuu maneno yako sawa kabisa na ndipo napochoka na Kikwete!.. binafsi nashindwa kuwalaumu watu hawa kwa sababu toka mwanzo wanajulikana kuwa sio viongozi wazuri lakini imekuwaje Kikwete kawachagua?..

Kikwete toka aingie maradakani ni scandal tupu! na ukitazama kwa makini chanzo ni yeye mwenyewe..Kabadilisha watu hadi inatia kinyaa kuona kwamba wanaoteuliwa kushika madaraka wengi wao bado BOMU..I mean hivi kweli Kikwete haoni mapungufu ya watu hawa au anatuchezea kamchezo ka kutafuta wachawi..

Uongozi sio kukaa Ikulu tu isipokuwa ni pamoja na uwezo wa kuchagua ama kuteua wapiganaji, watu ambao una hakika wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi na Uadilifu. Ushindi wa vita haupatikani kwa hesabu ya askari, umri ama elimu ya darasa...
Ikiwa kila mtu anayemchagua ni bomu hivi kweli naweza kumsifia Kikwete na kuwalaumu hao wanao boronga wakati ilifahamika kuwa hawawezi...
 
....waache utapeli wao,kusimama kwa ATCL ni ubovu wa madege yao,walipewa pesa wakaenda kuleta upupu Liberia kwa ajiri ya 10%.....sina hamu na hawa mafisadi hebu waondoeni tuu ili watu wenye uwezo na sio mafisadi waendeshe shirika,i hope Precison na mashirika mengine watasaidia kuleta huduma nzuri na bei chini sio hawa matapeli!
 
ATCL wawakilisha sababu za kuharibikiwa
Mwandishi Wetu
Daily News; Friday,December 19, 2008 @21:15

Habari nyingine
ATCL wawakilisha sababu za kuharibikiwa
Mpigapicha wa Channel Ten aagwa
TSN watoa msaada wa kompyuta
‘Zimbabwe isaidiwe kukabili kipindupindu’
Mgonja kula sikukuu uraiani
Basi laua polisi watatu
Bilioni 40 /- za mafisadi zanufaisha wakulima
Bodi ya ATCL matatani
Ujenzi wa barabara mpya Dar waiva
Dhamana ya Mgonja yakamilika

Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), imewasilisha kwa Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu ripoti ya maelezo ya kwa nini kampuni imefika hatua mbaya baada ya kupewa siku saba za kujieleza.

Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Balozi Mustafa Nyang’anyi aliliambia gazeti hili jana kuwa siku saba walizopewa na Waziri Dk. Shukuru Kawambwa zilianza Jumatatu na zinamalizika kesho, lakini walikamilisha kabla na tayari wameiwasilisha kwake.

Dk. Kawambwa juzi katika mkutano na waandishi wa habari, alisema ameipa bodi siku saba ieleze ni kwa nini ATCL imefikia kufungiwa na kuahidi kuwa baada ya maelezo hayo wale wote watakaobainika kuhusika atawawajibisha ipasavyo.

Katika mahojiano na gazeti hili jana kuhusu hali ya kampuni hiyo na matakwa ya wafanyakazi wa ATCL ya kumtaka ajiuzulu pamoja na Menejimenti inayoongozwa na Mkurugenzi, David Mattaka, Balozi Nyang’anyi alisema kujiuzulu kwake si tatizo, anaweza kufanya hivyo, lakini tatizo ni mtaji mdogo wa kuendesha kampuni hiyo.

“Unadhani tatizo ni kujiuzulu? Watu hawajui tulikuwa tukijiendesha vipi kwa kipindi chote cha miaka miwili, tuliomba mtaji kwa serikali wa US dollar milioni sabini na sita (takribani Sh bilioni 91.2) kuendesha kampuni, lakini kutokana na kuwa serikali nayo haina fedha, tumekwama mpaka leo,” alisema Nyang’anyi.

Ningeishaa sana kama serikali ingetoa fedha hizo kwa Uongozi uliokuwepo sasa hivi. Ingekuwa vizuri kwa wandishi wetu wakatufatutia ni nini hasa hawa wakubwa walikuwa wanataka kukifanya na mamilioni yote hayo. Baada ya kuona kuwa serikali haikutoa fedha hiyo je uongozi haukuona kuwa lilikuwa sababu tosha ya kujiuzulu kwa jinsi ambavyo serikali imeonesha haina imani nao? Je walikuwa wana ngoja nini?


Alisema hata hivyo waliandika maombi ya kupatiwa fedha kwa ajili ya kutafuta na kuchagua wataalamu wa kusaidia uendeshaji wa kampuni wenye ujuzi wa kiwango cha juu, lakini ukosefu wa fedha ulisababisha baadhi ya kampuni ikiwa ni pamoja na yaliokuwa yakiandika nyaraka ya ndege mpya ya Air Bus na DASH8-Q300 kushindwa kuendelea kwani zilihitaji Euro 360,000.

Baada ya Uongozi wa ATCL kushindwa kupata fedha za kuandika nyaraka mpya za Ndege na kwa kujua kwa kuendelea kutokuwa nazo ni kinyume na utaratibu wa uendeshaji wa shughuli za anga, je walichukua hatua gani? Je walijua kuwa wanakiuka taratibu? Waadilifu wangekuwa tayari wamekiri kushindwa.


Alisema hata hivyo wanaendelea na juhudi za kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanapata mshahara wa Desemba kwa wakati hata kama kampuni hiyo haizalishi na kwamba viwango vya kukidhi kumaliza dosari zilizoainishwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) vinatarajia kukamilika.

Kuhusu hatua za serikali kuinusuru ATCL kwa kuiongezea mtaji, alisema ni bora na italeta manufaa makubwa endapo ikitekelezeka kwa haraka.

Aidha, taarifa zilizopatikana jana kutoka wizarani zilieleza kuwa Waziri Kawambwa alikutana na viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na Uchukuzi, COTWU jana kwa ajili ya kuzungumzia hatua za serikali kwa madai yao na kuhakikishiwa mishahara kwa wakati

Suala la viongozi wa wafanyakazi kukutana na serikali ni jambo ambalo nimekuwa nikilisisitiza sana tangu hii saga ilipotokea. Serikali inawajibika kuwaambia wafanyakazi ni hatua gani zitafuata baada ya hapa. Kama serikali itaamua kuja na ATCL ya kichina au vinginevyo, wafanyakazi ni haki yao kufahamishwa hivyo mapema ili na wao waweze kujipanga na kuona ni jinsi gani wanaweza kushirikishwa katika hatua mbalimbali za kuboresha maamuzi ya serikali. Jambo hili ni muhimu ili kuepusha makosa kadhaa ambayo yalifanywa huko nyuma serikali kwa kukosa michango ya wafanyakazi ambao ni moja ya wadau muhimu wa usafiri wa anga. Vilevile ili kuondoa dhana ya kufanya kazi kisiasa ninarudia tena kuwa Waziri ateue ATCL Desk Officer hapo wizarani ambaye atakuwa ni kiungo kati ya ATCL na wizara katika shughuli za kila siku hadi hapo atakapoona inafaa kumuondoa.
.

Mod naomba tuiache kwa muda tupate maoni ya watu na pengine waio karibu na huko atcl...kujua ukweli halisi....

Mwisho ninaishauri Bodi na Menejimenti wajiondoe kwa hiyari zao ili kupisha au kutoa fursa kwa ATCL kuundwa upya.
 
pundamilia 07

Mungu akubariki kwa post zako na wote wenye mapenzi mema na kampuni hii. Kwa kweli inasikirisha..

Embu angalia

Wiki mbili zilizopita, jamani haya si majungu kuna marubani 31 na wafanyakazi wandani ya ndege 32 walikuwa hawajalipwa mishahara yao...lakini bodi ilikaa jumatano wakagawana doller 5500 na alhamisi ya wiki iliopita wakakaa tena wakagawana 5500usd na kupeana bonasi ya sikuku ya xmass na mwaka mpya doller 100usd kila mmoja..huku marubani hawana mishahara .....

Majuzi tu kulikuwa na mkutano wa waziri wa miundo mbinu mpole kawambwa na ma ceo wote waliochini ya wizara yake...jama alikuwa dodoma..nikiwambia hawa mabwana wanadharau kufa mtu ..na ndio inawaondoa sasa hamtaki...akamtuma mkur wa fedhwa anaitwa mr eliachafu...alipofika pale kawambwa akamjibu wapi mattaka akasema amesafiri kikazi...wapi lile jamaa alikuwa na data limeenda tu na jibu amesafiri kikazi..alivyo mjinga hakujua waziri ameshapenyezewa jamaa yuko arusha anakula kuku na kufanya maadalizi kabambe ya harusi ya mwanae.

Baya zaidi kamuni ikikosa mafuta mh mattaka aliamuru ofisi ya arusha atcl wampe sh million 4 kwa ajili ya harusi ya mwanae.....huko sifiki mtajuana atc; wenyewe....baadae akaitwa tena akaambiwa nakuuliza mataka yuko wapi akajibu amesafiri kikazi mkuu...akiwa na wakurugenzi wengine aliulizwa maswali matatu

moja: ukiwa kama kaimu mkurugenzi wa atcl mna plan gani kuhakikisha atcl inaendelea na kuongeza safari zake ndani na nje ya nchi

Pili:kama kaimu mkurugenzi...unaweza kutupa budget raf ya kuonyesha mchanaganuo wa matumizi ya kampuni yenu

tatu:::sisemi aibu....na ndilo lililomfanya mh raisi akamwambia sasa na kwambia nenda mpigie ,muandikie email tever utakachofanya namuitaji mattaka hapa....kabla ya saaa kumi na mbili....ndugu zangu yule bwana aliingia na ndege ya kukodi from arusha...kumi na mbili na nusu...sasa basi mnaweza kuona wapi hili shirika lipo., mikononi.........mwa watu wa aina gani....

Kwenu takukuru:::

tunawaomba hata hawa jamaa wakitolewa ama kuresign lazima wakajibu shutuma na wizi wote kwa jaji mkenjwa...pls tunaomba ..ushaidi wa wizi mnao kama mkiona autoshelezi....tumeni email kwa atclstaff@yahoo.com

matumizi mabovu yanazidi kuongezeka kila siku ...ninachosikia na kuwafurahia hawa jamaa jamani ni kimoja..wanasoma nyakati
wakati pesa zipo wanazunguka kila nchi na kila mkoa na wakisikia unalalamika wanakupa safari na wewe ukale nje ama ndani......na toka jf iwashtue...nasikia wamekuwa na adabu ya fedhwa wacha hili la bodi kuenedelea kukaa kila siku kwenye mikutano na kulazimisha kupewa doller 5500usd wakati kampuni haina hela
 
:sisemi-------------aibu....na ndilo lililomfanya mh raisi

kumradhi mh waziri wa miundo mbinu
 
Mbona huyu Nyang'anyi anazidi kuchemka! Anaacha kutueleza wana mipango gani kuliokoa shirika, yeye anajikita katika kuzungumzia kwa nini limefika hapo. nadhani hiyo ripoti aliyoiwasilisha ilifaa tu kwua background ambayo itaonyesha the way forward.
 
Back
Top Bottom