Safari za viongozi wetu nje ya nchi

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Tumekuwa tukilalamikia safari nyingi za Rais Kikwete nje ya nchi na labda kusahau safari za viongozi wengine. Hizi safari zinazofanywa na viongozi wengi pia tena kwa idadi kubwa kupita kiasi. Kwa mfano kwenye mkutano wa mwaka wa IMF and World Bank huko Uturuki Oktoba 2009, Tanzania iliwakilishwa na jumla ya wajumbe 25 wakati Kenya iliwakilishwa na wajumbe 9, Rwanda 5, Burundi 5 and Uganda 7. Kwa kifupi wakati Tanzania iliwakilishwa na wajumbe 25, nchi za Kenya, Rwanda, Burundi and Uganda kwa pamoja ziliwakilishwa na wajumbe 26 kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini.

Untitled.jpg
 
Mmh! Vidagaa navyo vinagonga tripu za kutosha ila si unajua tena avumae baharini papa.
 
Hapa umenena, hata kwenye hizi mamlaka, taasisi na ofisi za uma kuna safari watu wanaenda ambazo hazina tija na ofisi husiku ni jinsi ya kusaka pesa per diem na kuja baadaye na retirement za uwongo, kuna course za Esami na brah brah kibao watu wanaenda na mwisho wa siku hakuna pontetiality katika ofisi zao, no tija hapo ni mazingira ya kupata hela
 
Kibaya zaidi hakuna tija yoyote inayotokana na ushiriki wao huko zaidi ya kutalii.
 
Kweli inasikitisha sana kuona jinsi ambavyo nchi yetu ina matatizo mengi sekta za afya na elimu lakini kumbe viongozi wetu wanafurahia kupata allowances za safari.
Hebu muwe na huruma na pesa za watanzania -mpunguze hizo safari na idadi ya wawakilishi na muwe na hofu ya mungu .
Hata kwenye mashirika ya umma hili ni tatizo kubwa sana. Watu wanatunga safari nje ya nchi zisizokuwa nalazima nakujipatia hela kibao na safari hizo hazina faida kwa wa mashirika hayo wal kwa watanzania, kuweni na na hofu ya mungu jamani kwa kuacha ubinafsi...............

tumekuwa tukilalamikia safari nyingi za rais kikwete nje ya nchi na labda kusahau safari za viongozi wengine. Hizi safari zinazofanywa na viongozi wengi pia tena kwa idadi kubwa kupita kiasi. Kwa mfano kwenye mkutano wa mwaka wa imf and world bank huko uturuki oktoba 2009, tanzania iliwakilishwa na jumla ya wajumbe 25 wakati kenya iliwakilishwa na wajumbe 9, rwanda 5, burundi 5 and uganda 7. Kwa kifupi wakati tanzania iliwakilishwa na wajumbe 25, nchi za kenya, rwanda, burundi and uganda kwa pamoja ziliwakilishwa na wajumbe 26 kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini.

untitled.jpg
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Inasikitisha kwa kweli kwa jinsi nchi inavyoliwa na hawa watu...
 
Dah kweli ni noma ukijidai kukomaa na fisadi A kumbe kuna mafisadi B,C,D wanakuchek kwa pose wapate mwanya wa kukuingizeni mjini. Kazi tunayo.
 
Hapa umenena, hata kwenye hizi mamlaka, taasisi na ofisi za uma kuna safari watu wanaenda ambazo hazina tija na ofisi husiku ni jinsi ya kusaka pesa per diem na kuja baadaye na retirement za uwongo, kuna course za Esami na brah brah kibao watu wanaenda na mwisho wa siku hakuna pontetiality katika ofisi zao, no tija hapo ni mazingira ya kupata hela

Juzi juzi hapa JF kulikuwa na thread moja inayozungumzia safari ya staff wa EWURA nchi kama kumi hivi kwa wakati mmoja. Geuss what, hawa jamaa walipanda First class kwa ajili ya kutalii nchi hizo. Sasa first class tickets kwa ujumbe wa watu 10 plus per diem ya USD 400 per person per day ni parefu sana kwa hasa ukilinganisha na hali za kwenye hospitals, shule n.k. zilivyo mbaya. Kuna kituko kimoja pia nilikisoma sehemu kwamba nchi wahisani zilikuwa zinakutana Paris kwa ajili ya mkutano wa namna ya kutusaidia. So wajumbe watanzania na jamaa wa ubalozi wa Ufaransa walisafiri ndege moja. Cha kushangaza ujumbe wa Tanzania walisafiri First class na jamaa wa ubalozi wa ufaransa (wafadhiri) walisafiri economy. Mimi nadhani sisi tuna matatizo ya ubongo kidogo si bure jamani.
 
Mwisho wa siku sisi wananchi wenyewe tusiposimama (kidete) sawa sawa haya mambo hayatakwisha, tuangalie mabadiliko yanakujaje hapa umeona mioyo ya wabunge ilivyobadilika baada ya baadhi ya wabunge kuomba posho katika vikao rasmi ziondolewe maana ndo kazi yao watu wamekuja juu wakati huo huku chini mwananchi wa kawaida anumia

Juzi juzi hapa JF kulikuwa na thread moja inayozungumzia safari ya staff wa EWURA nchi kama kumi hivi kwa wakati mmoja. Geuss what, hawa jamaa walipanda First class kwa ajili ya kutalii nchi hizo. Sasa first class tickets kwa ujumbe wa watu 10 plus per diem ya USD 400 per person per day ni parefu sana kwa hasa ukilinganisha na hali za kwenye hospitals, shule n.k. zilivyo mbaya. Kuna kituko kimoja pia nilikisoma sehemu kwamba nchi wahisani zilikuwa zinakutana Paris kwa ajili ya mkutano wa namna ya kutusaidia. So wajumbe watanzania na jamaa wa ubalozi wa Ufaransa walisafiri ndege moja. Cha kushangaza ujumbe wa Tanzania walisafiri First class na jamaa wa ubalozi wa ufaransa (wafadhiri) walisafiri economy. Mimi nadhani sisi tuna matatizo ya ubongo kidogo si bure jamani.
 
Kweli inasikitisha sana kuona jinsi ambavyo nchi yetu ina matatizo mengi sekta za afya na elimu lakini kumbe viongozi wetu wanafurahia kupata allowances za safari.
Hebu muwe na huruma na pesa za watanzania -mpunguze hizo safari na idadi ya wawakilishi na muwe na hofu ya mungu .
Hata kwenye mashirika ya umma hili ni tatizo kubwa sana. Watu wanatunga safari nje ya nchi zisizokuwa nalazima nakujipatia hela kibao na safari hizo hazina faida kwa wa mashirika hayo wal kwa watanzania, kuweni na na hofu ya mungu jamani kwa kuacha ubinafsi...............

Mkuu hili ni tazito kubwa sana sio tuu safari za nje bali pia za ndani. Watu wanajitafutia safari zisizo za lazima kupata hizo posho.
 
Kweli kaka umenena, yaani sijui kama umepitia mashirika ya umma mbali mbali ?. Yaani mtu anatafuta course za nje fupi fupi na kuandaa mazingira ya kukubalika kwa mkubwa wa kazi na mara nyingi huwa wanapatana na wakubwa kisha anakwenda kwa mwaka ukihesabu utashangaa.....
Pesa zinazotumika kama ni kwenda ESAMI wangekwenda wafanyakazi wengi na wangepata ujuzi wengi lakini inafanyika hivyo ili kupata ULAJI.
UBINAFSI, dhambi mbaya sana
 
Back
Top Bottom