EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Tumekuwa tukilalamikia safari nyingi za Rais Kikwete nje ya nchi na labda kusahau safari za viongozi wengine. Hizi safari zinazofanywa na viongozi wengi pia tena kwa idadi kubwa kupita kiasi. Kwa mfano kwenye mkutano wa mwaka wa IMF and World Bank huko Uturuki Oktoba 2009, Tanzania iliwakilishwa na jumla ya wajumbe 25 wakati Kenya iliwakilishwa na wajumbe 9, Rwanda 5, Burundi 5 and Uganda 7. Kwa kifupi wakati Tanzania iliwakilishwa na wajumbe 25, nchi za Kenya, Rwanda, Burundi and Uganda kwa pamoja ziliwakilishwa na wajumbe 26 kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini.