Elections 2010 Safari ndefu ya ukombozi imeanza Chadema yagonga rasmi milango ya NEC

naona wewe umetumwa padri aoneshe huruma kwa wanaodai haki.!nyie wanufaika na uozo na mafisadi siku yenu inakuja
 
Mwanasheria wa CHADEMA, Mabere Marando amewasilisha rasmi NEC barua ya kupinga matokeo.

Hatua zilizochukuliwa/tutakazochukua ni:

1. Kwenda NEC - (barua imewasilishwa jana)
2. Tunakwenda kueleza Nchi wahisani ambazo zimefadhili shughuli za Uchaguzi
3. Tunakwenda kuwaeleza wananchi kilichotokea kwa kuwaonyesha ushahidi kamili.
4. Dk. Slaa amepanga kuwakilisha ushahidi MZITO unaoonyesha uchakachuaji mkubwa wa kura za Urais ulivyofanyika. Ushahidi huo ni pamoja na matokeo halisi ya vituoni yenye saini za mawakala ambayo yanapishana na yale ya NEC.

Marando alisema hadi juzi Jumatatu matokeo ambayo tayari walikuwa wamekusanya kutoka katika maeneo mbalimbali ya Nchi, yanaonyesha Mgombea Urais wa CHADEMA Dk. Willibrod Slaa anaongoza kwa wastani wa asilimia 61.6%.

My take; Mahakamani je?

Source ya hii topic yako iko wapi?
 

Chama chochote kina uhuru wa kukataa ama kukubali matokeo kulingana na maslahi inayopata. Hivi sasa ccm inaitumia cuf kukandamiz haki za watu wa tanzania bara. Hebu fikiria tokea kinana alipokurupuka kutangaza idadi ya viti vya ubunge hakuna mkurugenzi aliyethubutu kuruhusu matokeo yanaoonyesha chadema kushinda viti zaidi vya ubunge. Hizo ni njama za kuhakikisha kuwa cuf inakuwa kambi ya upinzani katika bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania kwa kupata viti 24 vya ubunge ambapo 22 kati ya hivyo nji vya pemba; na kuizidi chadema yenye viti 21 vya watanzania bara.
.
OH NOW I SEE, kaka umenifungua macho
 
Lengo la kupinga si kwa uchaguzi huu tu bali mpango mzima wa chaguzi zijazo pia, bila kurekebishwa sasa mambo yatajirudia uchaguzi ujao.

Ni sawa kabisa kwa unalo lisema kwa Mtu anayea Fuatilia siasa za TZ kwa umakini, Fina hupenda Democrasia ya kweli awe ni CUF,CCM,CHADEMA,NCCR,TLP etc atakubaliana na hoja yako ya msingi kabisa.

Mkuu umeona mbali sana sasa sijui hawa vioongozi wetu wachanga sijui wanaweza ona hizo alama za nyakati?

Nasikia waangalizi wa Chaguzi hizi wamehoji kwanini Wajumbe wa NEC walichaguliwa na RAIS, na kwanini ni wazeee badala ya Vijana?
Na mfumo mzima wa Technology waliyo itumia ulikuwa hajakamilika vyema mapema ili uweze kufanya kazi kwa haraka na kutoa majibu ya kura mapema na mwishowe ukachochea vurugu na kutokuwa na imani na matokeo ya kura zinazo somwa sasa.

 
NEC wanatimiza matakwa ya CCM ya kushinda kwa zaidi ya 80%.
Tunawashukuru CHADEMA kwa kuwasilisha barua yao ya malalamiko NEC kwa kutangaza matokeo ambayo hayakubandikwa vituoni kwa kumuongezea JK kura.
Tunaomba Jumuiya za kimataifa (UN, AU, SADC, UNDP) walijue hilo na CHADEMA wawapelekee nakala ya barua waliyoipeleka NEC ili wapate taarifa rasmi.
Kwa sasa CCM imekuwa mafia hata pale inaposhindwa siku zote inafanya mabadiliko na kujitangaza kushinda.
Tangu tuanze siasa za vyama vingi CCM haijawahi kushinda Zanzibar na imekuwa ikibadili matokeo na kujitangaza imeshinda.
Na uchaguzi wa mwaka huu hawatangazi kura zilizopatikana vituoni bali wanazichakachua na kumtangaza JK kashinda.

Sisi Watanzania wapenda AMANI tunataka mshindi wa Urais atangazwe kwa kura zake alizopata na kuhesabiwa vituoni sio UCHAKACHUWAJI HUU UNAOFANYWA NA NEC KWA AMRI YA CCM. Tupo tayari kukubali kama matokeo ya vituoni ndiyo yakitangazwa !!!!!

CHADEMA wasikate tamaa waendelee kuomba HAKI YAO na sisi Wanachama na washabiki na watanzania wote wapenda amani na wanaojua dhamani ya kura zao tuko nyuma yao mpaka kieleweke

PEOPLE 'zzzzzzzzz POWER ...........................
(HAKUNA MTU YEYOTE ANAYEWEZA KUZUIA NGUVU YA WANANCHI KWANI HII HUWA NI NGUVU YENYE MAMLAKA KUTOKA JUU)
:sad::sad::sad::sad::sad::sad::sad::sad:
 
Back
Top Bottom