Brightman Jr
JF-Expert Member
- Mar 22, 2009
- 1,225
- 232
Waheshimiwa habari zenyu. Mie niko safari natokea Mz to Dar. Nimepanda bac moja (jina tunalihifadhi). Kinachonishangaza humt ndani wamejaa si kawaida yaani mpaka wengine wamesimama. Cha ajabu kila tunapofika kwa wale wanaohusika na barabara konda anawaambia waliosimama wachuchumae chini ili tupite lindo. Bahati nzuri tumefika lindo moja hapa jamaa wa lindo imebidi aingie ndani na kuwakuta watu wamechuchumaa. Nashangaa bac imeruhusiwa na tunaendelea na safari! Wakuu hivi siku hizi level seat ilishafutwa? Au ni ule mtindo wa ''The beutyful ones are not yet born....!'' kaaazi kwelikweli.