kazuramimba
Senior Member
- Jun 14, 2011
- 126
- 57
wakuu kama kunge kuwa na Tuzo ya mpambanaji wa mwaka hasa kipindi hiki tunapoenda kumaliza mwaka basi mimi ningependekeza hao hapo juu wa pewe kila mmoja.Nianze na Saed kubenea ni mwandishi mwenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja,mchambuzi wa hali ya juu ambaye kiukweli hana tofauti na wanafalsafa wakubwa kama karl malx.Amefanikiwa kupanga safu ya mashambulizi kwenye gazeti lake la mwanahalisi na kufanya mafisadi wa muogope kila kona.Ni yeye aliye tufumbua macho na kufanya ulimwengu wa jue kuwa Rostam ndie mmliki wa Dowans.Ni yeye alie tufanya tuwajue wanasiasa wanafki kama Zitto kabwe na Samwel Sitta.Ukweli ni kuwa kama asingekuwepo huyu awareness tulio nayo juu ya mwenendo wa nchi yetu isingekuwepo.Pili Godbless lema ameonye njia ya kwamba nidhamu ya woga haina maana tena na ni heri vita inayo leta utu kuliko amani inayo pumbaza.walio bakia nadhani si hitaji kuwaelezea kwakuwa yanajulikana sana waliyo yafanya.Je wewe ungependa nani apigiwe kura kama shujaa wako kwa mwaka huu?