Sabodo awataka mafisadi warejeshe fedha,achangia kuchimba visima 1000

mashingo

Member
Nov 12, 2010
5
0
Source:
Gazeti la mwananchi,Saturday, 01 January 2011 11:37
by Festo Polea

MFANYABIASHARA maarufu wa jijini Dar es Salaam, Mustafa Sabodo, amesema kama viongozi wanaotuhumiwa kuhusika katika ufisadi wa namna yoyote nchini wanataka kusamehewa na Mungu na wananchi katika mwaka huu, lazima watoe fedha walizoibia nchi ili zielekezwe katika kusaidia wananchi.

Sabodo alitoa kauli hiyo jana ofisini kwake jijini Dar es salaam, wakati akitangaza kuchimba visima 1,000 katika wilaya zote nchini, isipokuwa katika Mkoa wa Dar es Salaam.


Katika hotuba yake, Sabodo aliitaka serikali isiingilie matumizi visima hivyo vyenye lengo la kuwasaidia wananchi kupata huduma za maji bila masharti.


Alisema ni jambo la ajabu kwa viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi, kuendelea kuhodhi fedha nyingi na kushindwa kuisaidia jamii inayowazunguka.

"Mimi ni tajiri na nina fedha nyingi kwa sasa na si fisadi, lakini nasaidia wananchi wa aina yote kwa kuwa naipenda Tanzania na watu wake. Kwa upande wao, mafisadi wanakumbatia fedha nyingi za kuiba lakini wagumu kuzitoa, halafu wanataka kusamehewa, hawatasamehewa kamwe," alisema Sabodo.

Mfanyabiashara huyo ambaye ni muumini wa falsafa za Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Nyerere, alisisitiza kuwa mwaka huu ni mwaka wa viongozi mafisadi kujisafisha kama wanahitaji kweli wanataka msamaha wa Mwenyezi Mungu na wananchi wa Tanzania.

"Mafisadi katika nchi hii ni kero, wana fedha nyingi, wameiba fedha na kuzificha halafu wanataka Mungu na Watanzania wawasamehe, hakika wakitaka kusamehewa watoe fedha walizoiba," alisisitiza
Kuhusu visima 1,000 atakavyovijenga katika wila zote nchini, Sabodo alisema kila kisima kitagharimu zaidi ya Sh5 milioni na ujenzi wake utakamilika Julai mwaka huu.

"Visima hivyo ninavyosaidia katika wilaya hizo sitapenda serikali iingilie kwa chochote kwa kuwa matengenezo madogo madogo yatafanywa na wananchi wenyewe. Hakuna yeyote atakayelipia katika kutumia visima hivyo," alisema.


Sabodo alisema visima hivyo vitachimbwa kulingana na mahitaji wa wananchi na wingi wao katika wilaya.
 
Source:
Gazeti la mwananchi,Saturday, 01 January 2011 11:37
by Festo Polea

MFANYABIASHARA maarufu wa jijini Dar es Salaam, Mustafa Sabodo, amesema kama viongozi wanaotuhumiwa kuhusika katika ufisadi wa namna yoyote nchini wanataka kusamehewa na Mungu na wananchi katika mwaka huu, lazima watoe fedha walizoibia nchi ili zielekezwe katika kusaidia wananchi.

Sabodo alitoa kauli hiyo jana ofisini kwake jijini Dar es salaam, wakati akitangaza kuchimba visima 1,000 katika wilaya zote nchini, isipokuwa katika Mkoa wa Dar es Salaam.


Katika hotuba yake, Sabodo aliitaka serikali isiingilie matumizi visima hivyo vyenye lengo la kuwasaidia wananchi kupata huduma za maji bila masharti.


Alisema ni jambo la ajabu kwa viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi, kuendelea kuhodhi fedha nyingi na kushindwa kuisaidia jamii inayowazunguka.

"Mimi ni tajiri na nina fedha nyingi kwa sasa na si fisadi, lakini nasaidia wananchi wa aina yote kwa kuwa naipenda Tanzania na watu wake. Kwa upande wao, mafisadi wanakumbatia fedha nyingi za kuiba lakini wagumu kuzitoa, halafu wanataka kusamehewa, hawatasamehewa kamwe," alisema Sabodo.

Mfanyabiashara huyo ambaye ni muumini wa falsafa za Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Nyerere, alisisitiza kuwa mwaka huu ni mwaka wa viongozi mafisadi kujisafisha kama wanahitaji kweli wanataka msamaha wa Mwenyezi Mungu na wananchi wa Tanzania.

"Mafisadi katika nchi hii ni kero, wana fedha nyingi, wameiba fedha na kuzificha halafu wanataka Mungu na Watanzania wawasamehe, hakika wakitaka kusamehewa watoe fedha walizoiba," alisisitiza
Kuhusu visima 1,000 atakavyovijenga katika wila zote nchini, Sabodo alisema kila kisima kitagharimu zaidi ya Sh5 milioni na ujenzi wake utakamilika Julai mwaka huu.

"Visima hivyo ninavyosaidia katika wilaya hizo sitapenda serikali iingilie kwa chochote kwa kuwa matengenezo madogo madogo yatafanywa na wananchi wenyewe. Hakuna yeyote atakayelipia katika kutumia visima hivyo," alisema.


Sabodo alisema visima hivyo vitachimbwa kulingana na mahitaji wa wananchi na wingi wao katika wilaya.


Bila shaka Mzee Sabodo hapa alimlenga Lowassa.
 
Back
Top Bottom