Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,119
- 9,049
Sabasaba ndio inakwenda kwenda mwishoni. Naamini kwa wale waliobahatika kutembelea mabanda ya maonyesho watakuwa wameona na kujifunza mambo mengi tofauti. Kwa mtazamo wangu, bado tuna safari ndefu ya kuimarisha viwanda vyetu vya ndani ili tuweze kuwa na uzalishaji wa kutosha. Bidhaa za ndani zilikuwa chache kuliko toka nje ambazo zililenga kupata masoko ya uhakika.
Katika mabanda yote, banda la JKT lilinifurahisha kwa kuwa na vitu vilivyotengenezwa hapa hapa tena kwa ustadi mkubwa.
Na lile la wakubwa zao au kaka zao, JWTZ, nalo lilikuwa zuri maana lilionyesha mambo mengi yanayofanywa na Jeshi katika kipindi cha amani.Lilinikumbusha geshi lile ambalo tulilizoe enzi tuko katika vikundi vya "komsomol" miaka michache iliyopita.
Katika mabanda yote, banda la JKT lilinifurahisha kwa kuwa na vitu vilivyotengenezwa hapa hapa tena kwa ustadi mkubwa.
Na lile la wakubwa zao au kaka zao, JWTZ, nalo lilikuwa zuri maana lilionyesha mambo mengi yanayofanywa na Jeshi katika kipindi cha amani.Lilinikumbusha geshi lile ambalo tulilizoe enzi tuko katika vikundi vya "komsomol" miaka michache iliyopita.