Sababu kuu za wabunge kudai nyongeza za posho kila kukicha ni hizi hapa;
Wabunge hulazimika kudai posho kubwa ili sehemu ya fedha hizo zisaidie kutatua baadhi ya matatizo binafsi yanayowakabili wananchi kama ada za shule, kughalimia matibabu, chakula n.k.
Lawama wanazopata wabunge wengi kuwa hawajafanya lolote katika maeneo yao ni matokeo ya serikali kushindwa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi wake. Lawama inaweza kuwa kwetu sisi wenyewe wananchi kushindwa kutengeneza serikali madhubuti. Nakaribisha michango zaidi sio matusi.
- Kwanza ni uelewa mdogo wa wananchi juu ya kazi za mbunge, pamoja na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuianisha wazi kazi za mbunge, watanzania wengi hawazijui kazi za mbunge. Wantazania wengi hufananisha kazi za mbunge na zile za serikali au wafadhiri, hii hupelekea kumubebesha mbunge kazi za serikali na wafadhiri. Ukosefu wa huduma za afya maji, elimu, barabara, umeme n.k hudhani hutokana na kuwapo mbunge dhaifu katika eneo husika.
- Kuwapo kwa serikali dhaifu sana, kuwapo kwa serikali isiyoleta maendeleo husababisha wabunge kupata lawama kubwa kutoka kwa wananchi wake. Serikali kushindwa kuleta huduma nzuri iwe katika afya, elimu n.k husababisha wananchi kuwabebesha wabunge lawama sana.
- Tatu ni wananchi kukabiliwa na umaskini ulikithiri, hii husababisha watu kukabiliwa na matatizo mbalimbali ya kifedha. Ili kujikwamua na matatizo hayo huhitaji ufadhiri kutoka kwa watu mbalimbali.
Wabunge hulazimika kudai posho kubwa ili sehemu ya fedha hizo zisaidie kutatua baadhi ya matatizo binafsi yanayowakabili wananchi kama ada za shule, kughalimia matibabu, chakula n.k.
Lawama wanazopata wabunge wengi kuwa hawajafanya lolote katika maeneo yao ni matokeo ya serikali kushindwa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi wake. Lawama inaweza kuwa kwetu sisi wenyewe wananchi kushindwa kutengeneza serikali madhubuti. Nakaribisha michango zaidi sio matusi.