MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Kuna sababu nyingi naona ni heri serikali ya chama cha mapinduzi kuliko serikali ya chama chochote cha upinzani tulionao. Hii ni kwa sababu hata kama CCM kime tupa baadhi ya sababu ya kuto kichagua bado naamini upinzani haujatupa sababu ya kuwa chagua na hilo ndilo la muhimu kuliko yote.
1.Upinzani mara nyingi umebaki kusema nini CCM haijafanya badala ya kukazania kutuambia nini wao wata fanya tofauti. Ni vigumu sana kuwa sikia wapinzani pale kunapo kuwa hamna maneno dhidi ya upinzani. Upinzani wetu upo REACTIVE badala ya kuwa PROACTIVE!
2.Vyama vyetu vya upinzani ni vyama vya uchaguzi tu. Ni vyama vichache na mara chache sana vinavyo jinadi kabla ya uchaguzi.
3.Wengi wa wapinzani walio kuwaga CCM na serikalini hawana track record nzuri na wengi wao inaelekea siyo wapinzani wa kweli bali wali hama kambi baada ya kuona hawana masilahi CCM.
4.Japo vyama vya upinzani havipo madarakni lakini bado kuna baadhi ya vitu wangeweza kufanya kusukuma gurudumu la maendeleo nchini. Sija sikia chama chochote cha upinzani kikiwa na program zozote za kijamii. Sijawahi(I could be wrong) kusikia chama chochote cha upinzani kikichangia aidha hali au mali wakati maafa yanapo tokea. Kumbuka kutoa ni moyo si utajiri.
5.Hata upinzani kuna baadhi ya watu ni mafisadi. Tumesikia wengine ambao wame pata utajiri wao kwa biashara zisizo halali au hata kuiba fedha za vyama vyao. Je hawa wakipewa serikali hawata endeleza ufisadi huo huo tena katika njia kubwa zaidi?
Baada ya kutafakari kwa muda mimi naona bado CCM ni chama "bora" kuliko chochote cha upinzani. Naamini kabisa kwamba bila baadhi ya watu wanao ichafua CCM bado kingekua chama imara. Nadhani baada ya enzi za Nyerere kuisha kule kupokezana kwa madaraka kulienda kwa kundi bovu badala ya kundi imara na kundi hilo ndiyo lime set precedent ya mambo yote yanayo tokea sasa. Bado sijaona upinzani wa kweli Tanzania. Ni mtazamo wangu tu.
1.Upinzani mara nyingi umebaki kusema nini CCM haijafanya badala ya kukazania kutuambia nini wao wata fanya tofauti. Ni vigumu sana kuwa sikia wapinzani pale kunapo kuwa hamna maneno dhidi ya upinzani. Upinzani wetu upo REACTIVE badala ya kuwa PROACTIVE!
2.Vyama vyetu vya upinzani ni vyama vya uchaguzi tu. Ni vyama vichache na mara chache sana vinavyo jinadi kabla ya uchaguzi.
3.Wengi wa wapinzani walio kuwaga CCM na serikalini hawana track record nzuri na wengi wao inaelekea siyo wapinzani wa kweli bali wali hama kambi baada ya kuona hawana masilahi CCM.
4.Japo vyama vya upinzani havipo madarakni lakini bado kuna baadhi ya vitu wangeweza kufanya kusukuma gurudumu la maendeleo nchini. Sija sikia chama chochote cha upinzani kikiwa na program zozote za kijamii. Sijawahi(I could be wrong) kusikia chama chochote cha upinzani kikichangia aidha hali au mali wakati maafa yanapo tokea. Kumbuka kutoa ni moyo si utajiri.
5.Hata upinzani kuna baadhi ya watu ni mafisadi. Tumesikia wengine ambao wame pata utajiri wao kwa biashara zisizo halali au hata kuiba fedha za vyama vyao. Je hawa wakipewa serikali hawata endeleza ufisadi huo huo tena katika njia kubwa zaidi?
Baada ya kutafakari kwa muda mimi naona bado CCM ni chama "bora" kuliko chochote cha upinzani. Naamini kabisa kwamba bila baadhi ya watu wanao ichafua CCM bado kingekua chama imara. Nadhani baada ya enzi za Nyerere kuisha kule kupokezana kwa madaraka kulienda kwa kundi bovu badala ya kundi imara na kundi hilo ndiyo lime set precedent ya mambo yote yanayo tokea sasa. Bado sijaona upinzani wa kweli Tanzania. Ni mtazamo wangu tu.