Mwanakilimo
Member
- Oct 25, 2011
- 12
- 4
Mimi naishi mjini, wala si mkulima kwa practice, bali kwa taaluma.
Mwaka jana kuna mbolea ya ruzuku 'ilikuja' mtaani kwetu nami nikajipati mfuko mmoja UREA na miwili ya DPP. Nilichukua nikaweke kwenye maua yangu.
Ukweli ni kwamba mpango wa serikali wa ruzuku ya pembejeo ni total failure. Sina uhakika kama serikali iliamua kwa makusudi kuplan na ku-implement mpango mbovu kiasi hicho, lakini nachojua ni kuwa kama objective yake ilikuwa kuongeza tija katika kilimo, then haijafanikiwa hata 20%. Kama objective ilikuwa siasa, then hapo sina comment...
Kwa ushauri tu wa mwanzo kwa serikali, kama kweli wanataka kusaidia kilimo na kumsaidia mkulima nchi hii, then wanatakiwa wawe na majibu ya ndiyo katika maswali yafuatayo...
1. Je, serikali ina orodha (register) ya wakulima wa mahindi, wa mtama, wa mihogo, wa kahawa, wa korosho, wa chai, wa tumbaku, wa pamba, wa kunde, wa viazi, wa ufuta, wa alizeti, wa pareto, wa vanila, wa ndizi, wa nyanya, wa vitunguu, wa mchicha, wa tikiti, wa mazao yote yanayolimwa hapa nchini?
2. je, serikali inajua mkulima x mwaka jana alilima mahindi ekari ngapi, alivuna ekari ngapi, mwaka huu kalima ngapi na mwaka ujao atalima ngapi?
3. Je, serikali inajua mkulima x ana ekari ngapi za ardhi ya kilimo cha mvua, na ngapi za ardhi ya kilimo cha umwagiliaji, anaweza kulima ngapi kwa mwaka, na ni kwa nini hawezi kulima ngapi?
Lengo la maswali yangu ni kutaka kuipa serikali ujumbe kuwa inatakiwa kuratibu kwanza shughuli za kilimo nchini, ili iweze kusaidia na kukuza kilimo. Serikali inatakiwa iwe na register ya wakulima wote nchini, mahali walipo, mazao wanayolima, ukubwa wa ardhi yao na aina ya kilimo wanachofanya. Kwa utaratibu huu ina maana kama kuna mtu anayelima mahindi, anatakiwa ajiorodheshe serikalini, aseme analima akari ngapi, ni shamba lake au la kukodisha n.k...
Serikali inatakiwa iratibu idadi ya ekari za zao fulani zilizolimwa mwaka husika, zililimwa wapi na mazao yalikuwaje... Serikali inatakiwa ifahamu mathalani mkuliwa y ana miti mingapi ya kahawa, au ya korosho na inahitaji mbolea ipi na kiasi gani, na uzalishaji wake ukoje...
Mtu unaweza kudhani ni kazi ngumu kwa serikali kufanya mambo haya lakini wka maendeleo ya teknolojia tuliyo nayo kwa sasa ni kazi rahisi mno. Serikali inaweza kuwa na majina yote ya wakulima wake, na pale itakapoamua kugawa mbolea ya ruzuku wka mfano, then wanajua mbolea kiasi fulani imeenda kwa fulani, na wanaweza ku crosscheck kwa kuwasiliana kwa simu na wakulima kadhaa (siku hizi asilimia kubwa ya wakulima wana simu), na kama ikionekana kuna tatizo eneo fulani, then mtendaji aliyekuwa responsible eneo hilo anafuatiliwa...
nina mengi sana na naamini wanajamvi pia mna mengi ya kuishauri serikali katika kuboresha kilimo Tanzania...
Mwaka jana kuna mbolea ya ruzuku 'ilikuja' mtaani kwetu nami nikajipati mfuko mmoja UREA na miwili ya DPP. Nilichukua nikaweke kwenye maua yangu.
Ukweli ni kwamba mpango wa serikali wa ruzuku ya pembejeo ni total failure. Sina uhakika kama serikali iliamua kwa makusudi kuplan na ku-implement mpango mbovu kiasi hicho, lakini nachojua ni kuwa kama objective yake ilikuwa kuongeza tija katika kilimo, then haijafanikiwa hata 20%. Kama objective ilikuwa siasa, then hapo sina comment...
Kwa ushauri tu wa mwanzo kwa serikali, kama kweli wanataka kusaidia kilimo na kumsaidia mkulima nchi hii, then wanatakiwa wawe na majibu ya ndiyo katika maswali yafuatayo...
1. Je, serikali ina orodha (register) ya wakulima wa mahindi, wa mtama, wa mihogo, wa kahawa, wa korosho, wa chai, wa tumbaku, wa pamba, wa kunde, wa viazi, wa ufuta, wa alizeti, wa pareto, wa vanila, wa ndizi, wa nyanya, wa vitunguu, wa mchicha, wa tikiti, wa mazao yote yanayolimwa hapa nchini?
2. je, serikali inajua mkulima x mwaka jana alilima mahindi ekari ngapi, alivuna ekari ngapi, mwaka huu kalima ngapi na mwaka ujao atalima ngapi?
3. Je, serikali inajua mkulima x ana ekari ngapi za ardhi ya kilimo cha mvua, na ngapi za ardhi ya kilimo cha umwagiliaji, anaweza kulima ngapi kwa mwaka, na ni kwa nini hawezi kulima ngapi?
Lengo la maswali yangu ni kutaka kuipa serikali ujumbe kuwa inatakiwa kuratibu kwanza shughuli za kilimo nchini, ili iweze kusaidia na kukuza kilimo. Serikali inatakiwa iwe na register ya wakulima wote nchini, mahali walipo, mazao wanayolima, ukubwa wa ardhi yao na aina ya kilimo wanachofanya. Kwa utaratibu huu ina maana kama kuna mtu anayelima mahindi, anatakiwa ajiorodheshe serikalini, aseme analima akari ngapi, ni shamba lake au la kukodisha n.k...
Serikali inatakiwa iratibu idadi ya ekari za zao fulani zilizolimwa mwaka husika, zililimwa wapi na mazao yalikuwaje... Serikali inatakiwa ifahamu mathalani mkuliwa y ana miti mingapi ya kahawa, au ya korosho na inahitaji mbolea ipi na kiasi gani, na uzalishaji wake ukoje...
Mtu unaweza kudhani ni kazi ngumu kwa serikali kufanya mambo haya lakini wka maendeleo ya teknolojia tuliyo nayo kwa sasa ni kazi rahisi mno. Serikali inaweza kuwa na majina yote ya wakulima wake, na pale itakapoamua kugawa mbolea ya ruzuku wka mfano, then wanajua mbolea kiasi fulani imeenda kwa fulani, na wanaweza ku crosscheck kwa kuwasiliana kwa simu na wakulima kadhaa (siku hizi asilimia kubwa ya wakulima wana simu), na kama ikionekana kuna tatizo eneo fulani, then mtendaji aliyekuwa responsible eneo hilo anafuatiliwa...
nina mengi sana na naamini wanajamvi pia mna mengi ya kuishauri serikali katika kuboresha kilimo Tanzania...