Sababu za JK kumnyima Samuel Sitta na kumpa Anne Makinda nishani hizi hapa!

Nimeshangazwa na kusikitishwa na Kitendo cha Rais JK kumnyima Nishani aliyekuwa Spika wa Bunge tisa Mhe. Samuel Sitta na Kumpa nishani hiyo Spika wa Sasa Anne Makinda ambaye hana vigezo alivyovitaja Rais. Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu atakubaliana na mimi kuwa hadi sasa, Anne Makinda hamkaribii na wala haoneshi dalili ya kufikia robo ya utendaji wa Samuel Sitta, mbaya zaidi hata mwaka mmoja bado hajamaliza kwenye hicho kiti, huo utendaji uliotukuka kauonyesha lini ilihali hadi sasa ni mauzauza tu???Kama kwa viwango vya Rais, Anne Makinda ni mtendaji bora zaidi ya Sitta, basi ndugu zangu tujue kuwa nchi hii tunajiongoza wenyewe.

Mhe. Samuel Sitta alipoulizwa sababu za kutopata nishani hiyo, alisema kwa sasa asingependa kulizungumzia suala hilo na kusisitiza, "hilo liache kwanza, sitaki kulizungumzia" Aidha, Rais Kikwete aliweka wazi kwamba, nishani hizo zimetolewa kwa Makamu Rais na mawaziri wakuu wastaafu walio hai ama waliokufa, walioondoka madarakani bila kashfa na hata baada ya kuondoka kwao madarakani, wameendelea kuwa na maadili mema na kuishi kwa heshima na maadili ya ofisi yao.

Maoni yangu

Kama Fedha za kuwezesha uwepo wa nishani hizi unatokana kodi zetu, nadiriki kusema fedha zetu zimechezewa kwani baadhi ya waliopewa hawana sifa mbele ya Umma ya kupewa nishani hizo zilizotokana na Kodi zetu kwa mfano, Mkapa. Mzee huyu pamoja na kuliongoza Taifa alijimilikisha kifisadi mgodi wa kiwira kupitia kampuni yake na mkewe tena akiwa bado madarakani. Hiyo heshima anayoisema JK huyu mzee anayo anatoka nayo wapi????Nani atamuheshimu kwa wizi alioufanya???Mzee huyu na mtuhumiwa wa ufisadi - Mramba walituingiza mkenge ktk manunuzi ya Rada na mambo mengine mengi ya hovyo hovyo kwa mtu wa hadhi yake kuyafanya. Spika Anne Makinda mara kadhaa amenukuliwa akitaka Posho za wabunge ziongezwe tena kwa hoja za kitoto kabisa za kupanda kwa gharama za maisha huku akijua kuwa Serikali kiuchumi ipo dhohoflihali. Kimsingi huyu mama hana utu na ni mbinafsi, anajijali yeye na tumbo lake. Anapendelea wazi wazi wabunge wa chama chake. Itoshe tu kusema kuwa huyu mama hana sifa za kuwa Spika ila Jinsia yake ndo ilimbeba kama tulivyoambiwa na waliompitisha kugombea nafasi ya uspika.

Kitendo cha Rais kutompa Nishani Mhe. Samuel Sitta, Spika ambaye kwa asilimia kubwa alionyesha uzalendo wa hali ya juu kwa kuruhusu mijadala ya ufisadi kujadiliwa kwa marefu na mapana yake Bungeni, ni dhahiri kuwa Rais wetu yupo kwa ajili ya mafisadi/wezi wa Rasilimali zetu na sio kwa ajili ya Wananchi. Nlitegemea Rais ampe Sitta nishani kwa moyo wa Uzalendo aliouonyesha akiwa Madarakani. Wataalam wa mambo ya kijamii wanaweza wakahusisha kitendo cha Sitta kunyimwa Nishani, pamoja na kutoteuliwa kugombea Uspika kuwa kinatokana na chuki aliyonayo Rais kwa yale aliyoyafanya Sitta akiwa Spika wa Bunge la Tisa. Kimsingi inaonekana Rais hakupenda yale aliyoyafanya Sitta akiwa Spika.

Kwa kuwaacha watumishi wanaostahili kupata Nishani hizo na kuwapa watu wasio na sifa za kupata nishani hizo. Ni dhahiri kuwa Nishani hizo zimepoteza sifa na kamwe haziwezi kuheshimiwa machoni mwa Watanzania.

Source: Mwananchi 12/12/2011


Ni kweli JK ana matatizo sana katika maamuzi yake. Lakini mara nyingine watu tunaowatetea kwa kweli wanatia mashaka. Samuel Sitta unayemtetea ni yeye ambaye alifunika mjadala wa Richmond ili serikali isishughulikiwe. Sitta alikuwa akifokea wabunge kama watoto wadogo na kurekebisha maswali ya wabunge kwa serikali. Ni kipindi cha Sitta huyo huyo ambapo kwa mara ya kwanza tulishuhudia bunge likipeleka unga wa uchawi kwa Mkemia Mkuu (sasa sijui kama Mkemia Mkuu ana vifaa vya kupima uchawi hatujui).

Tunaweza kuwa hatumpendi Anna Makinda labda kwa kwa sababu ya udhaifu wake lakini hapo hapo kwa mapenzi yetu kwa Sitta tukasahau udhaifu wake. Linganisha Ripoti mbili ile ya Mwakyembe na hii ya Ramo Makani. Utakuta ya Mwakyembe imejaa unafiki na uwongo (na hapa sijamsingizia Mwakyembe maana yeye mwenyewe alikiri kuficha baadhi ya mambo) wakati hii ya Ramo Makani imejitahidi kuwa very objective. Cha kushangaza ya Mwakyembe ilikuwa na mwenyekiti ambaye ana PhD hivi alishindwaje kuoanisha njia za utafiti, matokeo ya utafiti na hitimisho? Tofauti kabisa na Ripoti ya Ramo Makani unaona njia zilizotumika, matokeo na hitimisho. Kwenye Ripoti ya Ramo Makani wahusika wote wakuu waliwekwa kiti moto na hitimisho halikuegemea upande wowote. Nimetoa mfano wa hizo Ripoti mbili kuonyesha kwamba wakati tunalinganisha hao maspika wawili tuweke mizani ya haki na wala siyo mizani ya mapenzi na chuki.
 
ninachofahamu ni wanasayansi wa kenya walimfanyia surgery mtu aliyezaliwa bila miguu mwishowe alishinda medal ya dhahabu ya olimpiki ktk riadha ,,,ila wanasayansi wa TZ wakafunika baada ya mtu mmoja kuzaliwa bila kichwa na kisha wakamuwekea watermelon(tikitimaji) na sasa ni prezidaa
 
Ni kweli JK ana matatizo sana katika maamuzi yake. Lakini mara nyingine watu tunaowatetea kwa kweli wanatia mashaka. Samuel Sitta unayemtetea ni yeye ambaye alifunika mjadala wa Richmond ili serikali isishughulikiwe. Sitta alikuwa akifokea wabunge kama watoto wadogo na kurekebisha maswali ya wabunge kwa serikali. Ni kipindi cha Sitta huyo huyo ambapo kwa mara ya kwanza tulishuhudia bunge likipeleka unga wa uchawi kwa Mkemia Mkuu (sasa sijui kama Mkemia Mkuu ana vifaa vya kupima uchawi hatujui).

Tunaweza kuwa hatumpendi Anna Makinda labda kwa kwa sababu ya udhaifu wake lakini hapo hapo kwa mapenzi yetu kwa Sitta tukasahau udhaifu wake. Linganisha Ripoti mbili ile ya Mwakyembe na hii ya Ramo Makani. Utakuta ya Mwakyembe imejaa unafiki na uwongo (na hapa sijamsingizia Mwakyembe maana yeye mwenyewe alikiri kuficha baadhi ya mambo) wakati hii ya Ramo Makani imejitahidi kuwa very objective. Cha kushangaza ya Mwakyembe ilikuwa na mwenyekiti ambaye ana PhD hivi alishindwaje kuoanisha njia za utafiti, matokeo ya utafiti na hitimisho? Tofauti kabisa na Ripoti ya Ramo Makani unaona njia zilizotumika, matokeo na hitimisho. Kwenye Ripoti ya Ramo Makani wahusika wote wakuu waliwekwa kiti moto na hitimisho halikuegemea upande wowote. Nimetoa mfano wa hizo Ripoti mbili kuonyesha kwamba wakati tunalinganisha hao maspika wawili tuweke mizani ya haki na wala siyo mizani ya mapenzi na chuki.

Imekuwa tabia ya kawaida ya mwanadamu kusahau mema mia moja na kung'ang'ana na baya moja na hata kumchafua mtu kabisa. I understand the point you are trying to make, ila kama Sitta alionekana hafai kwa vigezo hivyo basi nadhan na Anne Makinda ndo hafai kabisa. Kinachoshangaza hapa ni kumuinclude Makinda ktk wapewa nishan tena wastaafu wkt yeye yupo ktk mwaka wake wa kwanza wa Uspika. Ustaafu kaupata wapi??? Lakin pia hadi sasa Mama huyu keshaonesha mapungufu makubwa kama spika hivyo sidhan kama ana sifa za kupewa hizo nishani. Inawezekana kweli Sitta hafai, lakin Makinda ndo hafai zaid. hivyo kumwacha sita na Kumpa Makinda bado kunaraise doubts ktk jamii ya watanzania.
 
Imekuwa tabia ya kawaida ya mwanadamu kusahau mema mia moja na kung'ang'ana na baya moja na hata kumchafua mtu kabisa. I understand the point you are trying to make, ila kama Sitta alionekana hafai kwa vigezo hivyo basi nadhan na Anne Makinda ndo hafai kabisa. Kinachoshangaza hapa ni kumuinclude Makinda ktk wapewa nishan tena wastaafu wkt yeye yupo ktk mwaka wake wa kwanza wa Uspika. Ustaafu kaupata wapi??? Lakin pia hadi sasa Mama huyu keshaonesha mapungufu makubwa kama spika hivyo sidhan kama ana sifa za kupewa hizo nishani. Inawezekana kweli Sitta hafai, lakin Makinda ndo hafai zaid. hivyo kumwacha sita na Kumpa Makinda bado kunaraise doubts ktk jamii ya watanzania.


Mimi nimekupa mifano miwili tu ya uchawi na ripoti za kamati. Nilichotaka kusema ni kwamba hao wote wana matatizo yao kwa hiyo ingekuwa vema kwako kama ungepanga mambo aliyofanya Sitta katika mwaka wake wa kwanza na mambo aliyoyafanya Makinda katika mwaka wake wa kwanza. Ukifanya hivyo itakusaidia hata wewe mwenyewe kujua kweli nani kati ya hao wawili hafai zaidi.
 
kwani lzm mtu apewe nishani,makinda mwanamke wa kwanza kuwa kiongozi wa mhimili wa dola,muda wa kumpa nishani ulikua huu mlitaka apewe miaka hamsini ijayo
 
Mkodoleaji

Sina shaka kuwa observations zako ziko sahihi, lakini ninamashaka na jinsi ambavyo umefanya hitimisho (conclusion) ya observations zako. Kimsingi Mwakyembe ripoti yake sijaujua vema unafiki uliokuwemo, labda kwa kuwa ilikuwa inainvolve significant figure within the government. Lakini pia ifahamike kuwa actions ambazo zililiwa proposed had greater impact on the government in power wakati ule. Yumkini Sitta alihitaji busara za ziada ku-deal na kitu kama hicho, na nina mashaka kama spika wa sasa angeweza kuruhusu hata kusomwa repoti ambayo kwangu naiona ilikuwa so sensitive! Itoshe kusema, kwamba kwa suala la unga ...hakuna aliyekuwa na hakika kama ilikuwa uchawi au sumu..polonium inawekwa kwa viti! Kwa hiyo ili kujiridhisha na kwenda kisayansi ilibidi apewe mkemia mkuu! Hapa si kupima uchawi, bali kuja na uchunguzi wa kisayansi kukubali au kukanusha hisia. Nina imani Sitta na wabunge wote wanajua kuna uchawi, kwa hiyo wangeweza kumtafuta sangoma mmoja na kuja kupunga mapepo hapo Bungeni!!!!

Ninalosema hapa ni kwamba sioni sababu ya kumnyima Sitta kisa ya mapungufu ya richmond na Unga wa uchawi. Hoja ibakie kuwa mbona Makinda kapewa wakati tuzo zilikuwa kwa wastaafu? Huyu mama bado, na ndo kamaliza mwak tuuuuuuuuu
Mimi nimekupa mifano miwili tu ya uchawi na ripoti za kamati. Nilichotaka kusema ni kwamba hao wote wana matatizo yao kwa hiyo ingekuwa vema kwako kama ungepanga mambo aliyofanya Sitta katika mwaka wake wa kwanza na mambo aliyoyafanya Makinda katika mwaka wake wa kwanza. Ukifanya hivyo itakusaidia hata wewe mwenyewe kujua kweli nani kati ya hao wawili hafai zaidi.
 
anajitahidi kuwawezesha wanawake, ila ningefurahi kama wanawake nao wangechangia hii mada kuona wanazungumzaje juu ya hili, kiufupi wale wote waliostahili kupewa nishani hii wamekuwa wakiilalamikia serikali ya awamu ya nne kwa utendaji mbovu labda ndio imepelekea wao kutotunukiwa

sasa yeye alitegemea kila anachofanya aungwe mkono wakati kaboronga zaidi mfano hili sakata la jairo mpaka sasa kakaa kimya kama hakuna kitu kilichotokea sasa mtu kama huyu tutamwelewa je? Au laana za watanzania ndo zinampumbaza hivyo?
 
Taarifa za wapi zinasema Sitta alistahafishwa????Sitta alimaliza muda wake wa miaka mitano bila kashfa yeyote kwa jamii. Alipoapply kuendelea na Uspika wa Bunge la Kumi CCM wakamuengua kwa kigezo cha kutokuwa na jinsia ya kike. Kimsingi vigezo vyote alikuwa navyo, ila kwa vile hakuwa na jinsia ya kike, nywele ndefu na matiti makubwa akapoteza kiti kile. Hakustaafishwa bali alikataliwa kuendelea na Uspika kwa kigezo cha jinsia.


Ubora wa mtendaji au kiongozi sio maneno bali anachosema na kuhubiri kinafaa kitafsiriwe kwa vitendo. Sitta akiwa spika alikuwa na maneno mengi ambayo kimantiki hayakuweza na hayataweza kumwachia legacy. Historia haiwezi kuandikwa kwa kuruhusu mijadala bungeni amabayo ni critical kwa serikali au alleged curruption curprits. No, not all. Kiongozi wa kweli anatakiwa aende zaidi ya hapo kwa kuhakikisha maazimio yanatekelzwa bila chembe ya shaka. Sasa Sitta tunaweza kumpima hivyo? Aliruhusu mjadala wa kashfa ya kampuni ya kufua umeme-Richmond ukaendelea, kamati ikaundwa, ikafanya kazi yake, ikatumia mamilioni ya walipa kodi kusafiri ndani na nje na muda wa kujadili maswala ya maendeleo ukawa haupo wabunge na watu nje ya bunge wakazama kwenye debate ya Richmond. Lakini cha ajabu mtu huyo huyo akaja kuuzima mjadala wa Richmond ktk kipindi ambacho Tiafa lilihitaji majibu ya kina kuwa haupashwi kujadiliwa tena. Sasa huyu ni mpambanaji wa kweli au tumwite tragic hero? Ni sawa na mtu aliyejilemba vizuri kuelekea kwenye sherehe na karibia na lango na shughuli anaamua kujipaka tope. Sitta hapa historia haiwezi kumsifu maana after all kitu ambacho vizazi vijavyo watataka kujua ni baada ya mjadala nini kilifanyika na kama hakikufanyika nini kilifuata? Sasa waandike spika alizima mjadala?


Pili Sitta kuwa mpambanaji wa ufisadi ni quite questionable maana hajawahi kutuambia aliongoka lini? Wakati Dr.Slaa anataka kuanika list of shame bungeni na kashfa ya EPA alinyimwa nafasi hiyo. Na ushahidi wa kile alichotaka kusema bungeni alipompatia spika-Sitta akaenda navyo kwenye kipindi cha maojiano na TBC kikiendeshwa na Simbeye akaonyesha hizo nyarak kwa dharau na akatishia kuzipeleka polisi. Sasa huyu ni mpamnaji anayeshindwa kuheshimu confidential information alipowa na mbunge? Na ilipokuja kudhihirika kuwa kweli watu walikwapua mabilioni toka BOT Sitta akuwahi kuliomba Taifa msamahaa kwa kuukataa ukweli aliokuwa amepelekewa na Dr.

Ujenzi wa nyumba ya bei kubwa kama ofisi ya spika kwenye jimbo lake. Je alifikiri yeye ni pertual speaker.

Haya pamoja na matukio mengine hayampi sitta uhalari wa kuvikwa nishani
 
chama ndicho kinakupa nafasi ya uongozi kama kinaona hujakiwakilisha vema hakina sababu ya kukupa nishani. suala la msingi viongozi hao wanaweza kupewa nishani hata na vyama vya upinzani kama vinaona Siita au Lowassa wanastahili.

Kwa upande wa lowasa nahisi hata yeye mwenyewe anajua hakustahili hofu ni kwa sita, nishani alizotoa Jk zimenifanya nizidi kuamini Jk kaweka baraza lake la mawaziri na timu yake kwa ujumla kwa maslahi yao binafsi na chama kuliko taifa, na nazidi kuamini ktk kashfa mbalimbali zinazojitokeza za ufisadi na mambo mengine Jk nae anahusika kwa 100%
 
Nishani alizotoa mzee wa kaya ni mwanzo wa yeye kupokea nishani yake mara atakapostaafu na taifa hili kuwa na katiba mpya ambayo itawapa wananchi uwezo wa kuhoji utawala uliotangulia
 
Lowassa kafukuzwa uwaziri Mkuu na sitta kafukuzwa uspika leo mnajiuliza kwa nini wamekosa nishani ni fikra mgando hizo wakati suala liko wazi

Mkuu kwa mtazamo wako Anna makinda anastahili kupewa hiyo tuzo kwakuwa spika for less than a year?
 
mimi naona angempa na Dr. Slaa kwa kumkimbiza mchakamchaka kipindi cha uchaguzi na CDM kwa ujumla kwa kuibua mambo ya kizalendo
 
Back
Top Bottom