Sababu Gani Wakenya Huja Huku JamiiForums?

EngineerLMG

Senior Member
Nov 28, 2013
125
75
Mara kwa mara huwa nasoma mambo kama "Wakenya mmeshindwa kutengeneza JF yenu"... "Tuwachie sisi JF yetu"... "Imetengenezwa na Watanzania"... "Hamna forums zenu"... "Hamna kazi ya kufanya mnakuja huku"...

Mnachosema ni kwamba hamtutaki kwenye forums zenu. Eti tusije. Lakini wacha niwaambie, tutasijaaa! Tena kwa rabsha na sokomoko.

Sababu moja itakayofanya tuzidi kusija JF inaweza kupatwa kwenye video hii hapa ya Coca Cola:


Tanzania ni kama ule mdogo. Na sisi? Si unajua tu.

Hata kama tunawahangaisha, deep down in our hearts, tunawapenda pia. Nyie ni ndugu zetu wa jadi. Na yeyote atakaye jaribu kuwasumbua, mtuambie tu. Tutapambana nao.

Kenya na Tanzania haziwezi kutenganishwa. Mimi kibinafsi, ninazo asili za Kitanzania (robo ya familia yangu iko TZ). Na tumetoka mbali, sisi majirani wawili.


TLDR: Tutaendelea kuja JF, tutaendelea kuwahangaisha, lakini hata hivyo, tunawapenda sana.
 
Tutasijaa! Ha ha ha. Umenikumbusha tukio moja club kati ya "soldier" na mteja mlevi.
Soldier: Toka!
Mteja: Sitoki!
Soldier kwa hasira: Wewe Sitoki? Hilarious ,anyway busara zilitawala all ended well.
 
Ninachopenda kila tukikutana hata nje ya EAC huwa tunaishi kama ndugu wa karibu.

Wakenya wako karibu sana na Watanzania ukilinganisha na nchi zingine za EAC.

Kupigana vijembe na Wakenya ni sehemu ya utamaduni wetu na Wakenya.

By the way, Uhusiano wa Watanzania na Wakenya sio kama ilivyo kwenye hiyo Advert.
 
aah dem za kenya zina guts asee, thats why i luv them.
Wewe uliza mkuu wa kaya wako kwa nn alimpenda msanii wa bongo?Jibu utapata tu,kuwa mabinti za bongo wajanja,wazuri na ukijichanganya wanakusafisha kila kitu mfukoni.Mabinti wa kenya damu zimelala mno.
 
Wakenya humu JF si wengi vile, ni kama ishirini+ hivi-na ndio wanapeleka hao watz wote kwa spidi ya blue subaru!
Sasa wale wakenya wote 700k+ waliokuwa Mashada forums wakija humu....?

Not many Kenyans know about JF, others simply dont care.
 
Wakenya humu JF si wengi vile, ni kama ishirini+ hivi-na ndio wanapeleka hao watz wote kwa spidi ya blue subaru!
Sasa wale wakenya wote 700k+ waliokuwa Mashada forums wakija humu....?

Not many Kenyans know about JF, others simply dont care.
Waiteni wachangamshe ngeli ya genge...si unajua matani ya TZ na Kenya yanatufanya tupasuke mbavu
 
Mara kwa mara huwa nasoma mambo kama "Wakenya mmeshindwa kutengeneza JF yenu"... "Tuwachie sisi JF yetu"... "Imetengenezwa na Watanzania"... "Hamna forums zenu"... "Hamna kazi ya kufanya mnakuja huku"...

Mnachosema ni kwamba hamtutaki kwenye forums zenu. Eti tusije. Lakini wacha niwaambie, tutasijaaa! Tena kwa rabsha na sokomoko.

Sababu moja itakayofanya tuzidi kusija JF inaweza kupatwa kwenye video hii hapa ya Coca Cola:


Tanzania ni kama ule mdogo. Na sisi? Si unajua tu.

Hata kama tunawahangaisha, deep down in our hearts, tunawapenda pia. Nyie ni ndugu zetu wa jadi. Na yeyote atakaye jaribu kuwasumbua, mtuambie tu. Tutapambana nao.

Kenya na Tanzania haziwezi kutenganishwa. Mimi kibinafsi, ninazo asili za Kitanzania (robo ya familia yangu iko TZ). Na tumetoka mbali, sisi majirani wawili.


TLDR: Tutaendelea kuja JF, tutaendelea kuwahangaisha, lakini hata hivyo, tunawapenda sana.

Huu ni mtandao wa kijamii mdau kama ilivyo fb,twitter na mingineyo
 
Hata kama tunawahangaisha, deep down in our hearts, tunawapenda pia. Nyie ni ndugu zetu wa jadi. Na yeyote atakaye jaribu kuwasumbua, mtuambie tu. Tutapambana nao.

Kenya na Tanzania haziwezi kutenganishwa. Mimi kibinafsi, ninazo asili za Kitanzania (robo ya familia yangu iko TZ). Na tumetoka mbali, sisi majirani wawili.
Umenena ukweli, sisi sio majirani tu, bali ni ndugu wa karibu.
 
Back
Top Bottom