Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Katika Gazeti la MwanaHALISI, tr 11-17/11/2009 inasemekana mbunge wa Nzega, mh Lucas Selelii wakati wa Kikao cha CCM Dodoma alieleza sababu tatu (3) zifuatazo kwamba Richmond (Development Company LLC) ni mali ya Rostam Aziz: 1. Alitafuta nyumba kwa ajili ya matumizi ya ofisi ya Richmond (Development Company LLC) na alilipia pango la nyumba hiyo! 2. Jopo la Waandishi wa Habari mashuhuri kwa ajili ya kuisafisha Richmond (Develpment Company LLC) baada ya vyombo vya habari kuanza kueleza utata wa mkataba lilitafutwa na Rostam Aziz ili kupoza makali! "Tumezungumza na waandishi wa habari hawa mmoja baada ya mwingine na wote wametuthibitishia hili," alisema Selelii. Majina ya waandishi hao ni Gideon Shoo, Jimmy Mdoe na Salva Rweyemamu ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais! 3. Fedha za Dowans (ambayo iliirithi Richmond Develpment Company LLC kwa shinikizo toka Wizara ya Nishati na Madini chini ya Karamagi) zilihamishiwa katika akaunti ya Caspian (ya Rostam Aziz), Rostam Aziz alikuwa akifuatilia mwenyewe fedha hizo hazina! Source: MwanaHALISI, tr 11-17/11/2009, uk. 2.