Elections 2010 Ruzuku ya Chadema

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Kwa vile Chadema kimejitokeza kuwa chama kikuu cha upinzani (a Government-in-Waiting), na kimetokea kuaminiwa na watanzania wengi, kitumie kipindi hiki cha kabla ya uchaguzi wa 2015 kujijenga kimuundo zaidi ndani na nje ya chama. Nitazungumzia muundo wa nje ya chama kwa vile muundo wa ndani umekamilika.

Tunajua ruzuku ya chama itaongezeka, ni wito wangu kwa viongozi kwa vile watanzania wameanza kuwaamini(kwa kuwapa kura za kutosha ofcourse) badala ya sehemu kubwa ya ruzuku kutumika kwenye mambo ya administrations itumike kujenga miundombinu ya chama.

Chadema inaweza kuanza kwa kupata ofisi za kudumu za mikoa, inawezekana kabisa kutenga kiasi fulani cha ruzuku kila baada ya miezi miwili na kujenga au kukodi ofisi moja ya mkoa. Wakifanya hivi kwa muda wa miaka miwili wanaweza kuwa wamekamilisha mikoa yote ya Tanzania.

Chadema ni chama cha kudumu viongozi wake wawe na mitazamo (vision) ya muda mrefu hata kuanza kufikiria kujenga makao makuu ya kudumu, ofisi wanazotumia leo zinaweza kuwa ofisi ndogo za chama au ofisi za wilaya ya Kinondoni, mbona CUF waliweza kununua jengo la ghorofa moja/mbili kwa ruzuku ya muda mfupi. Inawezekana kinachotakiwa ni commitment.

Vilevile wajaribu kuzipatia ofisi za wilaya uwezo kama usafiri wa uhakika na mawasiliano kuwezesha smooth running kati ya makao makuu na wilayani waliko wapiga kura. Kama tumeamua kuijenga nchi kupitia Chadema inawezekana tuache tamaa.

Nawasilisha.

Luteni is a True Revolutionist
 
Kwa vile Chadema kimejitokeza kuwa chama kikuu cha upinzani (a Government-in-Waiting), na kimetokea kuaminiwa na watanzania wengi, kitumie kipindi hiki cha kabla ya uchaguzi wa 2015 kujijenga kimuundo zaidi ndani na nje ya chama. Nitazungumzia muundo wa nje ya chama kwa vile muundo wa ndani umekamilika.

Tunajua ruzuku ya chama itaongezeka, ni wito wangu kwa viongozi kwa vile watanzania wameanza kuwaamini(kwa kuwapa kura za kutosha ofcourse) badala ya sehemu kubwa ya ruzuku kutumika kwenye mambo ya administrations itumike kujenga miundombinu ya chama.

Chadema inaweza kuanza kwa kupata ofisi za kudumu za mikoa, inawezekana kabisa kutenga kiasi fulani cha ruzuku kila baada ya miezi miwili na kujenga au kukodi ofisi moja ya mkoa. Wakifanya hivi kwa muda wa miaka miwili wanaweza kuwa wamekamilisha mikoa yote ya Tanzania.

Chadema ni chama cha kudumu viongozi wake wawe na mitazamo (vision) ya muda mrefu hata kuanza kufikiria kujenga makao makuu ya kudumu, ofisi wanazotumia leo zinaweza kuwa ofisi ndogo za chama au ofisi za wilaya ya Kinondoni, mbona CUF waliweza kununua jengo la ghorofa moja/mbili kwa ruzuku ya muda mfupi. Inawezekana kinachotakiwa ni commitment.

Vilevile wajaribu kuzipatia ofisi za wilaya uwezo kama usafiri wa uhakika na mawasiliano kuwezesha smooth running kati ya makao makuu na wilayani waliko wapiga kura. Kama tumeamua kuijenga nchi kupitia Chadema inawezekana tuache tamaa.

Nawasilisha.

Luteni is a True Revolutionist



Asante sana Luteni, hilo ni jambo la msingi sana kwa CHADEMA. CHADEMA wanatakiwa wawe na matawi nchi nzima.
Nakumbuka katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika 2009 wagombea wa CHADEMA walinyimwa kugombea kutokana na masharti yaliyowekwa na tume ya uchaguzi kwamba wagombea ni lazima wadhaminiwe na viongozi wa chama wa ngazi ya chini.
 
Ulichosema ni kweli kabisa,Lazima kama kweli Chadema kinahitaji kuaminika kianze mkakati kabambe wa kujiimarisha kuanzia ngazi ya chini kabisa ya mitaa na vitongoji na hili litafanikiwa tu kwa viongozi wa juu Kutoa Dira nakuhakikisha ngazi za Wilaya wanapatikana viongozi makini na mahiri,wenye uwezo wanaokipenda Chama na Nchi yetu ili waimarishe Chama ngazi za Chini kwa kuhakikisha watu wanapata elimu ya uraia, wanaijua katiba ya Chama nakuweka Transparency juu ya Matumizi ya fedha za ruzuku kuanzia ngazi ya juu kwakufanya hivyo watu tutakuwaradhi hata kuchanga fedha zetu kwaajili ya maendeleo ya Chama.
 
naam limefika tutalitendea kazi mkuu! nitalifikisha kwa waheshimiwa wa chadema pasipo kuchakachua mawazo yako luteni!
 
ofisi za mikoa zinahitajika lakini sio magari wilayani.
hata ofisi ya makao makuu haiitaji kuwa kubwa sana, ya wastani inatosha
 
mimi nilishasema Chadema lazima washiriki chaguzi za mitaa kwa nguvu zote maana ndiko ushindi wa uchaguzi mkuu huanzia. CCM wameshinda kwa sababu walikuwa na watu huko chini wakawa wanawafatilia wale mbumbu mitaani na vijijini. Tunahitaji kuwa na viongozi kila kijiji/mtaa na angalau tuwe na wanachama. Chadema sasa hivi ni hot cake kila mtu anataka kuwa mwanachama ila hawajuwi wapate wapi maelekezo au ofisi ya chama.

Wazo la kuwa na ofsi ni lazima. Dr. Slaa nadhani ni mwanaume wa shoka jambo hili atalifanyia kazi maana ndiye mtendaji mkuu wa chama.

Napendekeza hata yawekwe mahema na wawepo mawakala wa kuandikisha wanachama, sijuiwi kama hili lina tatizo kisheria. likifanyika zoezi kama hili japo kwa muda wa miezi miwili tunaweza kupata watu wengi sana.
 
Luteni uko very right.

Watu tupo tayari kusaidia kwenye kuimarisha ofisi za CHADEMA kuanzia kwenye mikoa,wilaya,kata mpaka vitongoji.
Napenda kunukuu maneno ya Naibu K/Mkuu Zitto Kabwe kuwa CHADEMA ni chama mbadala kinachotegemea kuchukua madaraka baada ya CCM.
 
Na kikubwa zaidi, kuonekana kwa matunda ya ruzuku hiyo kutawajengea imani kwa wananchi kwamba wako makini katika mipango na matumizi ya fedha. Wasisahau kwamba karata yao ya turufu ni vita dhidi ya ufisadi. Hivyo wabaya wao wanafuatilia kwa ukaribu sana jinsi wanavyotumia ruzuku wanayopata.
 
Tunajua ruzuku ya chama itaongezeka, ni wito wangu kwa viongozi kwa vile watanzania wameanza kuwaamini(kwa kuwapa kura za kutosha ofcourse) badala ya sehemu kubwa ya ruzuku kutumika kwenye mambo ya administrations itumike kujenga miundombinu ya chama.

Kuna anayefahamu hesabu za kukokotoa ruzuku inavyotolewa?
 
kwa vile chadema kimejitokeza kuwa chama kikuu cha upinzani (a government-in-waiting), na kimetokea kuaminiwa na watanzania wengi, kitumie kipindi hiki cha kabla ya uchaguzi wa 2015 kujijenga kimuundo zaidi ndani na nje ya chama. Nitazungumzia muundo wa nje ya chama kwa vile muundo wa ndani umekamilika.

Tunajua ruzuku ya chama itaongezeka, ni wito wangu kwa viongozi kwa vile watanzania wameanza kuwaamini(kwa kuwapa kura za kutosha ofcourse) badala ya sehemu kubwa ya ruzuku kutumika kwenye mambo ya administrations itumike kujenga miundombinu ya chama.

Chadema inaweza kuanza kwa kupata ofisi za kudumu za mikoa, inawezekana kabisa kutenga kiasi fulani cha ruzuku kila baada ya miezi miwili na kujenga au kukodi ofisi moja ya mkoa. Wakifanya hivi kwa muda wa miaka miwili wanaweza kuwa wamekamilisha mikoa yote ya tanzania.

Chadema ni chama cha kudumu viongozi wake wawe na mitazamo (vision) ya muda mrefu hata kuanza kufikiria kujenga makao makuu ya kudumu, ofisi wanazotumia leo zinaweza kuwa ofisi ndogo za chama au ofisi za wilaya ya kinondoni, mbona cuf waliweza kununua jengo la ghorofa moja/mbili kwa ruzuku ya muda mfupi. Inawezekana kinachotakiwa ni commitment.

Vilevile wajaribu kuzipatia ofisi za wilaya uwezo kama usafiri wa uhakika na mawasiliano kuwezesha smooth running kati ya makao makuu na wilayani waliko wapiga kura. Kama tumeamua kuijenga nchi kupitia chadema inawezekana tuache tamaa.

Nawasilisha.

luteni is a true revolutionist

asante sana luteni hayo ni mawazo mazuri sana tu, tena sana
 
Kwa vile Chadema kimejitokeza kuwa chama kikuu cha upinzani (a Government-in-Waiting), na kimetokea kuaminiwa na watanzania wengi, kitumie kipindi hiki cha kabla ya uchaguzi wa 2015 kujijenga kimuundo zaidi ndani na nje ya chama. Nitazungumzia muundo wa nje ya chama kwa vile muundo wa ndani umekamilika.

Tunajua ruzuku ya chama itaongezeka, ni wito wangu kwa viongozi kwa vile watanzania wameanza kuwaamini(kwa kuwapa kura za kutosha ofcourse) badala ya sehemu kubwa ya ruzuku kutumika kwenye mambo ya administrations itumike kujenga miundombinu ya chama.

Chadema inaweza kuanza kwa kupata ofisi za kudumu za mikoa, inawezekana kabisa kutenga kiasi fulani cha ruzuku kila baada ya miezi miwili na kujenga au kukodi ofisi moja ya mkoa. Wakifanya hivi kwa muda wa miaka miwili wanaweza kuwa wamekamilisha mikoa yote ya Tanzania.

Chadema ni chama cha kudumu viongozi wake wawe na mitazamo (vision) ya muda mrefu hata kuanza kufikiria kujenga makao makuu ya kudumu, ofisi wanazotumia leo zinaweza kuwa ofisi ndogo za chama au ofisi za wilaya ya Kinondoni, mbona CUF waliweza kununua jengo la ghorofa moja/mbili kwa ruzuku ya muda mfupi. Inawezekana kinachotakiwa ni commitment.

Vilevile wajaribu kuzipatia ofisi za wilaya uwezo kama usafiri wa uhakika na mawasiliano kuwezesha smooth running kati ya makao makuu na wilayani waliko wapiga kura. Kama tumeamua kuijenga nchi kupitia Chadema inawezekana tuache tamaa.

Nawasilisha.

Luteni is a True Revolutionist

Pamoja na mawazo mazuri ya kuijenga CHADEMA, bado naamini ruzuku peke yake haitoshi kukijenga chama, kwani hata CCM wanaopata mabilioni kwa mwezi haziwatoshi. Pia ukizingatia kwamba CCM wanatumia pia miundombinu nyingine ambayo ni mali ya umma kwa vile ilipatikakana wakati kikiwa ni chama dola. Kwa hiyo mimi nashauri wale wote ambao tuna moyo wa kuipenda nchi hii (HAPA SIONGELEI KUKIPENDA CHADEMA KAMA CHAMA) basi tuendeleze wimbi tulilolianzisha wakati wa uchaguzi la kukipa uwezo chama hiki ili baadaye kiweze kuwa imara sana na kushika dola ndani ya muda mfupi ujao. Kwa upande wa viongozi, wanatakiwa wasitumie imani ya wananchi vibaya. Hilo likitokea basi itatuchukua miango zaidi ya 2 kurudisha moyo wa wananchi kwa chama kingine cha upinzani. Kwani baada ya NCCR-Mageuzi ku-abuse confidence ya supporters wake, utaona kuwa imetuchukua zaidi ya miaka 10 sasa kuweza kuwavuta tena wananchi katika mkondo wa kudai na kuipigania demokrasia.
 
mimi nilishasema Chadema lazima washiriki chaguzi za mitaa kwa nguvu zote maana ndiko ushindi wa uchaguzi mkuu huanzia. CCM wameshinda kwa sababu walikuwa na watu huko chini wakawa wanawafatilia wale mbumbu mitaani na vijijini. Tunahitaji kuwa na viongozi kila kijiji/mtaa na angalau tuwe na wanachama. Chadema sasa hivi ni hot cake kila mtu anataka kuwa mwanachama ila hawajuwi wapate wapi maelekezo au ofisi ya chama.

Wazo la kuwa na ofsi ni lazima. Dr. Slaa nadhani ni mwanaume wa shoka jambo hili atalifanyia kazi maana ndiye mtendaji mkuu wa chama.

Napendekeza hata yawekwe mahema na wawepo mawakala wa kuandikisha wanachama, sijuiwi kama hili lina tatizo kisheria. likifanyika zoezi kama hili japo kwa muda wa miezi miwili tunaweza kupata watu wengi sana.
Asante Ngonini

Umesema jambo la maana sana Serikali za Mitaa ni mtaji ambao CCM huwa inautumia kwenye uchaguzi mkuu, namwamini Katibu wa Chadema Dr.Slaa(PhD) lazima atakuwa na mikakati kuhusu maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa.

Tusiwalaumu watu wa vijijini kuwa kwanini wakipata matatizo mtu wa kwanza kumwendea ni balozi wa nyumba kumi lakini waende wapi kama ndiye aliyepo karibu. Chadema wasifanye mchezo wautumie huu mtaji watu walioupata kwenye uchaguzi huu kabla haujapotea kwa kufungua ofisi na matawi sehemu mbaimbali.

Nitafurahi sana siku moja kusikia au kuona kwenye TV Dr. Slaa au Mh. Mbowe akifungua ofisi ya chama ya wilaya au Mkoa wa Mtwara mfano, hiyo itaongeza uaminifu wa watu kwao lakini watu wakianza kusikia viongozi wamepigania ruzuku watu hawakawii kuifananisha Chadema na NCCR ilivyokuwa.

Lakini naamini Chadema ina viongozi walio determined ndiyo maana wengi tunatumia muda wetu mwingi kuishauri vinginevyo what is the use kama hawasikilizi kwa nini tusiendelee kuishauri CCM tuliyoizoea. We need Operation Sangara Part. 2.

Luteni is a True Revolutionist
 
Pamoja na mawazo mazuri ya kuijenga CHADEMA, bado naamini ruzuku peke yake haitoshi kukijenga chama, kwani hata CCM wanaopata mabilioni kwa mwezi haziwatoshi. Pia ukizingatia kwamba CCM wanatumia pia miundombinu nyingine ambayo ni mali ya umma kwa vile ilipatikakana wakati kikiwa ni chama dola. Kwa hiyo mimi nashauri wale wote ambao tuna moyo wa kuipenda nchi hii (HAPA SIONGELEI KUKIPENDA CHADEMA KAMA CHAMA) basi tuendeleze wimbi tulilolianzisha wakati wa uchaguzi la kukipa uwezo chama hiki ili baadaye kiweze kuwa imara sana na kushika dola ndani ya muda mfupi ujao. Kwa upande wa viongozi, wanatakiwa wasitumie imani ya wananchi vibaya. Hilo likitokea basi itatuchukua miango zaidi ya 2 kurudisha moyo wa wananchi kwa chama kingine cha upinzani. Kwani baada ya NCCR-Mageuzi ku-abuse confidence ya supporters wake, utaona kuwa imetuchukua zaidi ya miaka 10 sasa kuweza kuwavuta tena wananchi katika mkondo wa kudai na kuipigania demokrasia.
DC

Ni kweli ruzuku peke yake haitoshi lakini kupanga ni kuchagua, hakuna siku mtu atasema hela imetosha hela huwa haijai mfukoni, ila ukitaka zijae zipangilie uwe na priorities. CCM wao matumizi yao yanajulikana tunajua zinapoishia ndiyo maana leo tunawashauri Chadema wasifanye hayo madudu. Niliwahi kusikia choo kimoja chenye matundu sijui matano kinajengwa kwa Mil. 700(ni mfano tu), kama matunizi yenyewe ndiyo ya aina hiyo hata upewe ruzuku ya bil.10 kwa mwezi haziwezi kutosha.
 
kuna wakati chadema walizindua kampeni ya chadema ni tawi hivi iliishia wapi au ilikwamishwa na nini?
 
Hodi hodi wana bodi! Naomba mnipokee ndiyo mara yangu ya kwanza nachangia.
Ibra Mo, pamoja na yote ulioyasema ambayo na mazuri ya kufanyiwa kazi na Chadema, pia waanze kuanzia sasa kuwa na orodha yote ya vituo vilivyopigia kura mwaka huu ili iwasadie kuwa na idadi ya mawakala wa 2015 watayarishe bajeti kuanzia sasa. Itakpofika hiyo 2015 watakuwa wamejiweka mahali pazuri kwa kushindana bila ya kuwa na wasiwasi wa fedha ya kuwalipa wakala.Mimi naliona hili lilkuwa ni tatizo kwa vyama vingi VYA UPINZANI. Haya ni maoni yangu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom