Wana JF sasa sio siri tena, mgombea wa CCM jimbo la Arusha mjini anatoa rushwa bila kificho, wafaidika wa kwanza ni wakina mama wa soko kuu Arusha wanafuatia waendesha pikipiki na waendesha mikokoteni. Anachofanya ni kuwawekea mafuata waendesha pikipiki ya 10,000/= na kuwapa fulana ya CCM, wakina mama na waendesha mikokoteni wanapewa 10,000 na jezi. Pia wenyeviti wa vitongoji ndo wanatumika kwenda nyumba kwa nyumba wakigawa mrungula na Tshirt. Inawezekana nchi nzima ndo mtindo unaotumika tuwe macho.