Kiwi
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 1,054
- 990
tulipiga kelele sana kuwa mradi wa mabasi hauwezekani UMEWEZEKANA.......sasa tunapiga kelele kuwa hilo la treni haliwezekani MWAKYEMBE na timu yake WANAANZA KUONYESHA WANAWEZA
Sisi TUNAONGEA wao WANAFANYA........mwisho wa siku tutasema wameiba kura kwa sababu mikutano yao haijazi watu....KUMBE WENZETU HAWAONGEI KWA MIDOMO BALI VITENDO
Mradi wa mabasi 'yaendayo kasi' umewezekana??? Nimeona bomoa bomoa maeneo kadhaa na harakati za kujenga njia (lane) za kupitisha mabasi hayo, lakini sijaona utekelezaji wake.
Kupanua au kujenga barabara ni moja tu kati ya changamoto za mradi wa mabasi. Changamoto zingine kama taa za barabarani kufanya kazi, na usimamizi wa kuhakikisha ya kuwa hizo njia (lanes) zilizowekwa kweli zitatumika kwa mabasi tu na kuzuia magari madogo, mikokoteni, bajaj, bodaboda, baiskeli za guta n.k kutumia njia hizo bado zipo. Askari wetu waliozoea kitu kidogo tutawabadilishaje mtazamo wao wasichukue pesa na kufumba macho watakapoona magari ya walio tayari kutoa rushwa yanatumia njia hizo? Na magari ya 'vigogo' wakikwama kwenye foleni wakaamua kupita njia za mabasi kuna atakayekuwa tayari kuwadhibiti, hali anajua kibarua chake kinaweza kuota nyasi?
Hayo yatakapowezekana, mabasi 'yaendayo kasi' yatakapoanza kutembea mijini na daladala, bajaj, bodaboda, mikokoteni, guta n.k zitakapoondoka kwenye barabara zetu; na pale mgao wa giza unaoathiri taa za kuongozea magari utakapokwisha ndiyo tuanze kutoa pongezi.
Kuhusu reli... makadirio yote hayo kuhusu watu wangapi watanufaika tujuzane nauli itakuwa shilingi ngapi? Na bei ya mafuta (dizeli) inayozidi kupanda kila kukicha? Tusije kupewa majibu kama ya watu wa Kigamboni walioambiwa asiyeweza nauli mpya apige mbizi!!!
Taarifa kwenye makaratasi na mbele ya TV inapendeza, lakini inawezekana?