Ila mkuu nakataa matumizi ya 'mzalendo' kwani wapo watanzania wneye asili ya ki-asia (yaani wahindi) ambao ni wazalendo na wapiganaji mmoja ni Rakesh Rajani - mkurgenzi wa zamani wa HakiElimu. NI jasiri na mpaka leo anaendelea mapigano yake kupita NGO nyingine nimeisahau jina. Rakesh ni mtanzania halisi na hana makuu na anaongea Kiswahili kama sisi tu bila lafudhi. Tuache ubaguzi jamani.
Ila tukirudi kwa hao mafisadi nakubaliana na wewe kuwa wafanyabiashara (waafrika na waasia) wanaogombea kupitia CCM wako hapo kwa ajili ya kusaidia biashara zao na kufuja mali za umma. Ingetakiwa iwekwe wazi kuwa mfanya biashara pindi anapoingia siasa anajiuzulu katika biashara zake... hapo utajua wazalendo kama wapo. Hehehe!
Nawashangaa ndugu zangu wa Babati kwa wahindi kwa asili hawapendi kushirikiana na watu wasio wahindi, sijui walimpitishaje awe mgombea wao? Wahindi tunawafahamu sana, hawachangamani na jamii; hata dini yao hawapendi ujiunge nayo, kumwoa muhindi ni vigumu sana,
Babati mnakosea sana;
Mimi sielewi dini ya wahindi ni ipi? wako wahindi wanaosali makanisani, wapo wahindi wanaoswali misikitini, wapo wahindi wanasali katika mahekalu, dini ya wahindi ni ipi jaman? kuoa ni makubaliano ya muoaji na muolewaji, kwani hakuna wasiokuwa wahindi ambao wameoa wahindi na vice versa? basi chuki zisitufikishe huko jamani,,:mad2::mad2::mad2::mad2:
Nakuabliana na wewe kuhusu Rakesh wa HakiElimu, wengine ambaye ninamkumbuka kwa karibu ni Prof Shifji, tatizo la wahamiaji wengi kutoka India na Pakstani ni kuwa wanawaangusha wahiaji wazalendo kama Rakesh na Shifji. Kama kweli nyuma yake hana dalili za ubabaishaji na ufisadi basi aungwe mkono lakini kama naye ni miongoni mwa wale wengi basi apingwe kwa nguvu zote