jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
Umesema ukweli. Tanzanians we can talk the talk but we can't walk the walk. Siasa za jukwaani tunaweza ila utekelezaji sasa. Ndiyo maana kuna miradi mingi iki tangazwa mpaka mwenyewe utapenda ila ikija kwenye kutekeleza misaada hiyo hakuna chochote. Tatizo Tanzania rushwa kila sehemu. Hata hela zilizo lengwa kusaidia wagonjwa, masikini na watu wenye shida zinaliwa.
Hapa wengi tuta piga kelele ila 2010 matokeo yale yale na ni kwa sababu wenye kuongea tu ni wengi kuliko wanao tenda. Tanzania ufisadi siyo tatizo pekee, hata mentality ya what inatia wasi wasi.
Ndiyo maana Dewji yeye kajiamulia kufadhili zake mpira katulia. Wengi wana lalamika oh tuna wabagua tuna wabagua mbona wakina Dewji hawaja tajwa kama mafisadi papa.
Lakini you can't control others, the best you can do is control yourself & hope others do the same. Tuta jaribu kubadilisha taifa lakini watu wenyewe wasipo taka kubadilika kazi ipo.
You are right,despite the fact kwamba words matter,bila vitendo ni BURE!
Ufanisi wetu na utendaji kazi wetu unapimwa kwa maneno na si vitendo,na ndio maana kiongozi anaweza akatenda mabaya kwa vitendo vyake lakini akamaliza mchezo kwa maneno.
Chukulia mfano tu wa Mh Zitto na hotuba yake huko Busanda. Utabaki ukijiuliza kweli ni mtu gani mwenye akili timamu anayesikiliza maneno yale na bado kuipigia ccm kura?
Hapo ndo utashangazwa na kuona ni kwa jinsi gani Taifa letu lilivyo "Mfu"
Mambo ya ushabiki ushabiki tu,vitendo ni bure,na ndio maana inachosha,kama ni mtu unayependa kuona progress,the you will get pissed off.
Na kwasababu sisi wenyewe kwa wenyewe huwa tuna chuki baina yetu na ndiyo maana ni vigumu kuaminiana,na ndio maana hata wananchi wenye mawazo mbadala hawapati nafasi kwa vigezo kama hatumuamini na nchi itakosa amani...Ni upuuzi Mtupu!
Kama wananchi wanataka amani,basi michezo iendelezwe na mafisadi waombwe kuwa waisaidie michezo hiyo ili amani,upendo na furaha viendelee kudumu. Watanzania hawataki maendeleo na kuwalazimishia ni ukichaa,wapewe kitu roho inataka,wanataka mafisadi,wapewe mafisadi.
Na kujitolea muhanga wasahahu maana watasahaulika mapema mno...Kama bado waandika historia ni wale wale walioko madarakani,then tusahau....Kina Fundikira na Kambona waliota,ndoto zao hazijatimia,nani mwingine mwenye ubavu wa kuota? Jibu silioni,ni mchezo matopeni tu,kama kungekuwa na utaratibu wa kuwaenzi wenye mawazo ya tofauti ya kimaendeleo kwa vitendo,labda ningejaribu kuamini.