Rostam katika tope jipya

Umesema ukweli. Tanzanians we can talk the talk but we can't walk the walk. Siasa za jukwaani tunaweza ila utekelezaji sasa. Ndiyo maana kuna miradi mingi iki tangazwa mpaka mwenyewe utapenda ila ikija kwenye kutekeleza misaada hiyo hakuna chochote. Tatizo Tanzania rushwa kila sehemu. Hata hela zilizo lengwa kusaidia wagonjwa, masikini na watu wenye shida zinaliwa.
Hapa wengi tuta piga kelele ila 2010 matokeo yale yale na ni kwa sababu wenye kuongea tu ni wengi kuliko wanao tenda. Tanzania ufisadi siyo tatizo pekee, hata mentality ya what inatia wasi wasi.
Ndiyo maana Dewji yeye kajiamulia kufadhili zake mpira katulia. Wengi wana lalamika oh tuna wabagua tuna wabagua mbona wakina Dewji hawaja tajwa kama mafisadi papa.
Lakini you can't control others, the best you can do is control yourself & hope others do the same. Tuta jaribu kubadilisha taifa lakini watu wenyewe wasipo taka kubadilika kazi ipo.

You are right,despite the fact kwamba words matter,bila vitendo ni BURE!

Ufanisi wetu na utendaji kazi wetu unapimwa kwa maneno na si vitendo,na ndio maana kiongozi anaweza akatenda mabaya kwa vitendo vyake lakini akamaliza mchezo kwa maneno.

Chukulia mfano tu wa Mh Zitto na hotuba yake huko Busanda. Utabaki ukijiuliza kweli ni mtu gani mwenye akili timamu anayesikiliza maneno yale na bado kuipigia ccm kura?

Hapo ndo utashangazwa na kuona ni kwa jinsi gani Taifa letu lilivyo "Mfu"

Mambo ya ushabiki ushabiki tu,vitendo ni bure,na ndio maana inachosha,kama ni mtu unayependa kuona progress,the you will get pissed off.

Na kwasababu sisi wenyewe kwa wenyewe huwa tuna chuki baina yetu na ndiyo maana ni vigumu kuaminiana,na ndio maana hata wananchi wenye mawazo mbadala hawapati nafasi kwa vigezo kama hatumuamini na nchi itakosa amani...Ni upuuzi Mtupu!

Kama wananchi wanataka amani,basi michezo iendelezwe na mafisadi waombwe kuwa waisaidie michezo hiyo ili amani,upendo na furaha viendelee kudumu. Watanzania hawataki maendeleo na kuwalazimishia ni ukichaa,wapewe kitu roho inataka,wanataka mafisadi,wapewe mafisadi.

Na kujitolea muhanga wasahahu maana watasahaulika mapema mno...Kama bado waandika historia ni wale wale walioko madarakani,then tusahau....Kina Fundikira na Kambona waliota,ndoto zao hazijatimia,nani mwingine mwenye ubavu wa kuota? Jibu silioni,ni mchezo matopeni tu,kama kungekuwa na utaratibu wa kuwaenzi wenye mawazo ya tofauti ya kimaendeleo kwa vitendo,labda ningejaribu kuamini.
 
Hii ingekuwa ni vita ya Risasi, sisi walala hoi tungekuwa karibia kwisha na pengine jeuri yetu kutupwa lupango ioze huko.
Kwa sababu hii bado ni vita ya maneno, ni heri kwetu walala hoi wa ndani na wa ughaibhuni kwa sababu kibano kinazidi kuwaandama Mafisadi kila dakika.
Mafisadi hawawezi kukwepa kibano hiki kwa sababu kila liibukapo jambo kazi kubwa kwao siyo kurekebisha mambo, kazi yao kubwa ni kulinda heshima yao isipinde wala kuingia ukungu kwa gharama ya kuvunja taratibu na kusema uongo pia kulazimisha hoja. Kwa kufanya hivyo tu, kuvunja taratibu, wanajitengenezea kashfa za kesho kiulaini.
Mafisadi walikaa chini pale ikulu kuandaa mikakati ya kuiba na kugawana kisicho chao, hata siku moja hawakuwahi kuota kwamba siku itafika siku ambayo watawajibika kwa wananchi na kutakiwa kutoa maelezo ya kina juu ya wizi uharamia na uuaji wao.
Mafisadi bado wanaamini kwamba Utawala wao ni wa kudumu kwani hawaoni kati yetu nani mwenye uwezo wa kukali viti vyao na makalio yake madogo.
Mafisadi hawana plan yeyote ya maana ya kujikinga na mashambulizi yetu kwa sababu plan hiyo haijawahi kuwekwa mezani kwani haikuwa ni plan ya lazima.
kila liibukapo jambo, kila mmoja hutoka kivyake na kusema mbovu na kuishia kimya kimya.
Ni juzi tu hapa wamesema mengi sana kwa vile tu Kanda mkuu na Bosi wa Idiologi ya CCM MH Rostam Aziz alipakwa tope la usoni.
Ni haki yao kumlinda mtu mwenye IQ kubwa ya kujenga umoja wa Chama kama Rostam Aziz. Huyo ni Juche mshauri mkuu wa MaoTse Tung.

Endelezeni mapambano yenu.
Vita ya maneno nayo ni vita.

Madilu,sikatai kwamba vita ya maneno ni vita,lakini wahenga walibaini kuwa maneno matupu hayavunji mfupa....Kwamfano issue ya RA na Mengi,eti ikageuzwa kuwa ni vita ya wafanyabiashara,ina maana ufanya biashara ni ufisadi? Yani Taifa likiibiwa ni vita kati ya wafanyabiashara,ina maana nchi imegawanywa na kuuzwa kwa wafanyabiashara?Mkuu nakubaliana na vita ya maneno,ila bila vitendo inakuwa ni ngumu kuona matokeo,wananchi wasipobadilika tutakuwa tunapoteza muda,badala yake kwanza labda wapewe elimu kuwa wanacho kabla ya kufikiri kuwa watakifanyia nini kile wasichojua kuwa wanacho...Kwasababu wengi wao si wameaminishwa kuwa sisi ni masikini na kwamba serikali inalinda amani? Zaidi ya hapo watake nini na wanasikia habari za vita kila kukicha kwa majirani. Hiyo ni sababu tosha sana kwa mtanzania wa kizazi hiki kuendelea kuwa masikini....Huku wakimwona mkuu wa nchi akiranda randa kuomba omba kwa wazungu,waasia na waarabu,wa ndani na nje ya nchi,ni kivipi mtawaambia kuwa sisi ni matajiri na wao waamini? Wao wanaona mnawaonea kina RA kwasababu hata wao wenyewe wanaisaidia serikali kwa kupitia chama cha ccm,umesahahu milioni mia nne? Na michezo pia,wacha wabongo wapate wanachostahili,na waliojitolea kwa maneno pia tunawashukuru na Mungu awabariki.
 
Unajua Idd Amin alikuwa na akili nyingi kuliko Nyerere !!! sasa ndiyo nagundua, kumbe Amin aliona mbali sana kuliko Nyerere, hawa magabacholi hawafai hata kwa dawa!!. Nafikiri turudi tena tulikotoka na kuchukua uamuzi wa Idd Amin Dada.
Amin alikuwa na akili kuliko Nyerere? Kuwafukuza wahindi ndizo akili hizo?
Uzawa ni ubaguzi. Nyerere aliuita ni ukaburu mwingine. Nakubali.
 
Mnajua hapa mnamfanya Kubenea kuwa ni Mungu na kila analosema ni kweli,

Hapa unaongelea kina nani hao wanaomfanya Kubenea kuwa kama Mungu. Ninavyoelewa mpaka sasa watu wanajadili alichoandika na sijamwona hata moja anayedai kuwa ni kweli 100%.

mimi nakwambieni kuwa Rostam hajawahi kufanya kazi ya kuuza mahindi,

Duh, hapa ama wewe ni Rostam mwenyewe au mpishi wake, umejuaje hilo ? This appears to be right from the horse's mouth - you seem to know more than you'd care to admit.

tena hio kampuni wala haijapata kuwa na jina lake......

Na hii ni kali zaidi - labda utueleze ni kwenye kampuni zipi jina lake limeonekana. Najaribu sana kujizuia nisihusishe jina lako na Rostam - si unajua tena mahusiano kati ya baba na mwana.

lakini kwa kuwa wamedanganya kuwa ripoti ya CIG imesema hivyo kabla ya kuchangia hapa

Na wewe kwa kuwa unadai kuwa wamedanganya, vipi ukitupa ukweli kabla ya kuchangia hapa - kata mzizi wa fitina wa kwetu !!

wngapi mnaweza kusema mmeiona ripoti hio au mnamsikiliza tu kubenea wenu kilaza namba moja

Sisi wengine tumeona aliyoandika Kilaza wetu namba moja Kubenea, je wewe unamsikiliza nani. Kama nilivyowahi kusema, ujasiri mkubwa unahitajika kuweza kumtetea Fisadi Papa labda uwe Fisadi Mtoto.
 
Mbona katika hiyo repoti hakuna kipengele kinachosema RA anahusika na uchafu huu?. Labda macho yangu yamepitiwa na kushindwa kukiona kipengele hicho.
 
Mbona katika hiyo repoti hakuna kipengele kinachosema RA anahusika na uchafu huu?. Labda macho yangu yamepitiwa na kushindwa kukiona kipengele hicho.
Nenda CCRBT

WANATIBU BURE UGONJWA WAKO
 
KULA CARROT KIDOGO UJARIBU NA HAYA


Tuhuma hizo zinahusu gharama za kutoa bandarini tani 4,677.82 za mahindi kazi iliyofanywa na Rostam Aziz.

Kazi hiyo iligharimu Sh. 894,372,520 bila ya kuwapo mkataba kati ya Rostam na serikali
 
Mbona katika hiyo repoti hakuna kipengele kinachosema RA anahusika na uchafu huu?. Labda macho yangu yamepitiwa na kushindwa kukiona kipengele hicho.

Nenda CCRBT

WANATIBU BURE UGONJWA WAKO

Mkuu huoni kama ingekuwa ni hekima kunionesha kipengele hicho badala ya kunitolea kashfa?. Kupitiwa ni jambo la kawaida.
 
Swadaktaaaa, hiri rijamaaaa kila mahala palipo na feza chafu ukinusa vizuri utalikuta, hebu angalia Caspian inafanya kazi migodini kuchimba udongo lakini ili rikwepe kulipa mshahara kima cha chini wa kwenye migodi (Tsh 350,000/=) basi likaandikisha kuwa Caspian Viwanda na Biashara? halafu anajifanya anapenda wanainchi, Mzurumati mkubwa wa haki za wanainchi, na hao CCM wanazidi kumkumbatia wakati anazidi kuongeza mfarakano ndani ya chama chao kwa kuanza kuwapangia safu ya wabunge wa 2010 kwani tayari kesha anza kufadhili anaowataka yeye , Tusubiri tumbwiritumbwri wakati ukifika tutaona mgawanyiko wa Tarime Tanzania mzima
icon10.gif

Kweli mkuu,
Yaani huyu jamaa alitakiwa apigwe PI aondoke nchini aende huko Canada au Irani. Na mpango wake wa kuweka wabunge wake ni juhudi tu za ili aje awaweke kwenye safu ya uwaziri ikiwa JK ataendelea kuwa rais kwani tunaona jinsi anavyoitawala nchi hii. Na huyu jamaa ni mafia kwelikweli. Wabunge waliokinyume naye ikiwa atafanikiwa kuwaengua kwenye kura za maoni dawa ni wao kuihama CCM na kujiunga na upinzani na watakuwa na hoja nzito za kushawishi wananchi kwa nini wasiichague CCM ha hii kwa hakika itaongeza nguvu ya upinzani bungeni na hatimaye kupata rais toka vyama vya upinzani. MUNGU ana njia zake za kuleta mafanikio kwa watu wake, tuendelee kuomba, saa ya ukombozi i karibu.
 
Mwanakijiji,
Hope wewe una contacts za Kubenea hebu mwulize kwenye hii ripoti tuliyowekewa hapa na Dilunga tusome ukurasa wa ngapi wenye hiyo taarifa maana ripoti yenyewe ni ndefu na wengine tuna kazi nyingi kwa sasa.
 
Last edited:
Mnajua hapa mnamfanya Kubenea kuwa ni Mungu na kila analosema ni kweli,mimi nakwambieni kuwa Rostam hajawahi kufanya kazi ya kuuza mahindi,tena hio kampuni wala haijapata kuwa na jina lake......lakini kwa kuwa wamedanganya kuwa ripoti ya CIG imesema hivyo kabla ya kuchangia hapa wngapi mnaweza kusema mmeiona ripoti hio au mnamsikiliza tu kubenea wenu kilaza namba moja

Taratibu mkubwa. Chunga maneno unayoandika waweza kujipatia laana bure. Huwezi kumweka mwanadamu kwenye nafasi ya Mungu hata siku moja. Mtetee tu mteja wako (Rostam) kwa lugha nzuri. Be careful, ohoooo!
 
Kweli mkuu,
Yaani huyu jamaa alitakiwa apigwe PI aondoke nchini aende huko Canada au Irani. Na mpango wake wa kuweka wabunge wake ni juhudi tu za ili aje awaweke kwenye safu ya uwaziri ikiwa JK ataendelea kuwa rais kwani tunaona jinsi anavyoitawala nchi hii. Na huyu jamaa ni mafia kwelikweli. Wabunge waliokinyume naye ikiwa atafanikiwa kuwaengua kwenye kura za maoni dawa ni wao kuihama CCM na kujiunga na upinzani na watakuwa na hoja nzito za kushawishi wananchi kwa nini wasiichague CCM ha hii kwa hakika itaongeza nguvu ya upinzani bungeni na hatimaye kupata rais toka vyama vya upinzani. MUNGU ana njia zake za kuleta mafanikio kwa watu wake, tuendelee kuomba, saa ya ukombozi i karibu.

Yeeeeeeees mkuu! tuendelee kuomba mipango yake ifanikiwe, awatoe wote na wao wapigie debe upinzani...Amina
Naona mwanga kwa mbaaaaali mtu kama Mwakyembe na ameongozana na wenzie wote
 
Taratibu mkubwa. Chunga maneno unayoandika waweza kujipatia laana bure. Huwezi kumweka mwanadamu kwenye nafasi ya Mungu hata siku moja. Mtetee tu mteja wako (Rostam) kwa lugha nzuri. Be careful, ohoooo!

Mkuu asante kuliona hilo, nilisha sema kwamba mafisadi hawajaishia kufisadi mali zetu, wameenda zaidi hadi kwenye bongo za baadhi yetu, ndiyo maana kwao mwizi ni, ni hero wao, ni muheshimiwa! Hadi wengine wanatamani wangekuwa kama wezi hao, wengine hadi kumpa sifa kwamba ni 'geniasi' n.k, kwahiyo akiguswa wako radhi hata kufanya makufuru!
 
Bubu wenye JF kina nani?...unafikiri bila mimi na wewe n others kutakuwa na JF?

Acha alinacha zako na UPUUZi Hivi unafikiri BAK na wewe wakiamua kuondoka JF basi itakufa!? Ha ha ha ha una alinacha za ajabu kweli kweli! Wanachama zaidi ya 10,000 eti akitoka kilalamishi chuma na BAK hakutakuwa na JF!!!

Tatizo lako upo kama Mwanakjj anaamini kila analofanya yupo Sahihi. Hata kukubali kosa unashindwa...naona nawe ushaanza kupata blind follower...Mwafrika.

Mwanakijiji anaingiaje kwa 'copy and paste' za BAK!? :confused: blind followers hapa JF ndio akina nani hao JF!? Unaweza kufafanua? Sikubali koosa kama si kutenda kosa lolote ambalo linaonekana kwa kilalamishi chuma tu na si kwa mwingine yeyote yule? Hivi uko hapa kufuatilia makosa yanayofanywa na BAK!? :confused: Tafuta la maana la kufanya achana na mimi or just SHUT UP! IF YOU HAVE NOTHING IMPORTANT TO SAY.

Halafu zikijaa thread mnaanzisha thread ya kupongezana...? Kweli kama Huu ndio usomi wenu basi tuna kaz huko mbele ya safari.

Kwani wanaJF wakiamua kupongezana wewe unaathirika vipi mpaka ubwabwaje bila mpango!? Wewe mtu wa ajabu sana hata watu kupongezana kunakukosesha raha! Watu wengine bwana wanajua kucreate matatizo yasiyokuwepo!!! Hata wanaJF wakiamua kupongezana imeshakuwa shida!

Mwafrika elewa kuwa mie na support at any cost Mafisadi wote papa na nyangumi waanikwe. na wale wanaojifunza ufisadi pia waanikwe....Ila wakati tunawalaumu viongozi kufanya recycling ya viongozi nyie mnachofanya n hicho hicho ktk mathread.

Ha ha ha eti unasupport mafisadi waanikwe!!! halafu wakati huo huo watu ambao wako mstari wa mbele katika vita dhidi ya mafisadi kama Mwanakijiji unawakejeli eti wana blind followers hapa JF na pia kufananisha kurecyle viongozi mafisadi Tanzania na kutuma jumbe hapa ukumbini. Ha ha ha mtu mzima HOVYO!
 
Unajua Idd Amin alikuwa na akili nyingi kuliko Nyerere !!! sasa ndiyo nagundua, kumbe Amin aliona mbali sana kuliko Nyerere, hawa magabacholi hawafai hata kwa dawa!!. Nafikiri turudi tena tulikotoka na kuchukua uamuzi wa Idd Amin Dada.

Lets call a spade a spade and not a big spoon. Watanzania tumelala, viongozi wetu ndio kabisaa! Wazungu wanakuja hapa hawana hata mahali pa kulala, na wanaondoka wakiwa mamilionea, kisa ni wazungu. Wahindi pia. Ukienda kwenye ofisi za serikali una ishu zako watakuzungusha sana kwa kuwe wewe ni Mswahili mwenzao, ila akiingia mzungu au mhindi wanampaparikia. Hii ni mental slavery iliyopo wa Watanzani karibu wote, kuanzia walala hoi mpaka viongozi wa juu wa kitaifa.

Sasas swali linakuja, jee ukiwa unakula na kipofu unatakiwa kumshika mkono???? Tuamkeni jamani! Siamini tuna mito na maziwa makubwa halafu kila mwaka kuna baa la njaa kwa ukosefu wa mvua...........!!! Mito na maziwa yetu tunayaimba kwenye nyimbo za kuisifia nchi bila hata kujiuliza yanatusaidiaje!
 
ishalah iko siku yote yataisha na tuone kama pua zao zinaangalia chini au juu. Hivi kweli watanzania weusi tunaweza tukafanya hayo kwo na tukaangaliwa tuu . Inatia kinyaa kwa serikali yetu kuwakumbatia watu hawa. Indi kuna wabunge wangapi waswahili ? Aibu, aibu, aibu.
 
Back
Top Bottom