Halisi,
I beg to differ just for the sake!
1. Siogopi
2. Siwezi kushabikia 'UASI' sehemu yeyote 'NYETI'
3. Nitaendele Kushabikia huu 'UKOMBOZI' ;hapa tupo pamoja.
Nafikiri tutakubaliana kuwa MMKJJ huwa haji hapa kimbelembele, huwa akipiga mbiu kuna jambo, RA keshapigiwa ramli za aina zote humu JF na hapa nyumbani lakini wapi...kila kitu sasa "Wakombozi" tunadai tunajua, sembuse uraia wake?
Nimeuliza maswali kadha hapo juu(refer to previous post) Where is our Investigative Journalism? Zitabakia kuwa Tetesi tu? Kuvuliwa Uraia kwa sababu gani kuu, sio Raia? Ni Fisadi? Mwirani? Hivi kuna Mtanzania Mtanzania?
Hivi EL anajulikana kama fisadi sio? Atanyanganywa Umasai? Manake kawaaibisha wa Morani wenzake, Wamasai, Watanzania na ndi sisi Watanzania tuanolia tunafisadiwa.AU?
Kwanini Tunamtafutia RA njia rahisi ya kuondoka? ....Haya basi sio Raia wa Tanzania aondoke mara moja...halafu vita vya ufisadi ndio basi?
Ahsante
Nawewe jaribu kuwa mwelewa! Huwezi kulinganisha uraia wa EL na rostam, nadhani hujafikiria kidogo. Huyu rostam ana uraia wa nchi mbili kitu ambacho ni kosa kisheria. Sasa kwa sababu na yeye na fisadi na anaonekana kutudharau basi tutumie njia ya uraia kumfukuza nchini. EL tutamshughulikia taratibu kwa sababu ni morani wa hapa hapa.