Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Mwanzoni mwa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM mwaka 2005, wengi walitarajia Dr Salim Ahmed Salim angelichaguliwa kwa kura nyingi kutokana na ukweli kwamba yeye ndiye alikuwa anaonekana kuwa na sifa zote - hakuwa na makundi, hakuwa na kashifa nyuma yake, utendaji kazi wake kwa ujumla ulimuainisha kama Rais mtarajiwa baada ya Benjamin Mkapa.
Hata hivyo, magenge ya majasusi yakiongozwa na Jangili Rostam yalijua kama hilo lingelitokea wangelijikuta ama wanakimbia nchi au wanapata vyumba katika magereza yetu. Hawakutaka vyote viwili na walijua kuwa mtu waliyemtaka achukue Urais hakuwa na sifa za kiutendaji, kwa wengi Kikwete alionekana kama brother man fulani ambaye mahala pake ilikuwa ni vijiwe vya mjini na kwenye kumbi za starehe, haiba yake na utendaji wake wa kazi wa nyuma haukuonyesha kuwa huyu alikuwa rais mtarajiwa.
Wafuasi wake walilitambua hilo vyema na wakabuni mbinu ambazo zingelimuuza huyu kwa wapiga kura (walinunua vyombo vya habari na kuwalipa wanahabari kulifanikisha hili), lakini pia walibuni mbinu za kuwaengua wagombea wengine wote waliokuwa na sifa stahili na ambao walionekana kuwa ni kikwazo kwa mgombea wao. Katika wagombea wote wa kura za maoni, Dr Salmin ndiye alikuwa tishio kubwa na walifanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kuwa wanamchafua ipasavyo.
Wahariri wa magazeti walilipwa kuhakikisha kuwa habari za wagombea zilimsifia mgombea wao, Kikwete, propaganda za chini chini zilipenyezwa na kutuaminisha kuwa Salmin alishiriki kumuua Karume Snr na alikuwa hafai kupewa nchi. Tukaambiwa kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu, akina sisi tulijua tunapotoshwa na tuliwapuuza waliokuwa wakimsifia, lakini walifanikiwa kuwavuna wengi na wakafanikiwa kumuweka Kikwete madarakani kwa kura nyingi.
Kwa sababu Dr Salmin hakujiandaa kwa siasa za kihuni namna hii, aliangushwa vibaya na matokeo yake wote tunayafahamu.
Baada ya kuingia Ikulu walibuni mbinu mbalimbali za kuhakikisha kuwa wanavuna ipasavyo, wakaja na Richmond (baada ya kufanikiwa kuchota za EPA).
UCHAGUZI wa 2010 umeleta changamoto zinazofanana na zile za 2005 lakini sasa wamekuja na mbinu mpya.
Baada ya kuikagua CV ya Mh Slaa wasione mawaa wala dosari yoyote katika utendaji kazi wake wamempata akiishi na mama aliyeolewa na kuachana na mme wake wa awali na kulifanya kuwa mtaji wao mkubwa.
Wamewahamisha watanzania kutoka kwenye mijadala ya muhimu na ya msingi ya kuangalia ni nini wagombea wanataka kuifanyia Tanzania na wanaweza kiasi gani, wametuhamisha kutoka kwenye mijadala ya je haya anayosema Kikwete na CCM watayafanya wanaweza na wanaoutashi wa kuyafanya? Je ni kwa nini hawakuyafanya au hata kuonyesha jitihada za kutaka kuyafanya kwa kipindi walichokuwa madarakani miaka mitano inayomalizika? Wametukosesha fursa ya kutafakari na kujadili ni yupi kati ya wagombea wa upinzani anaweza kuyatekeleza yale anayoyasema? Je Dr Slaa ataweza kulishughulikia suala la ufisadi kwa nguvu zile zile alizolishughulikia akiwa mbunge wa upinzani? Je anao utashi na uwezo kuzitatua kero zilizoishinda serikali ya CCM?
Badala yake wametupeleka kwenye mijadala ya kitoto na isiyotusaidia kupata kiongozi atakaye shughulikia kero zetu, sasa tunajadili ndoa mfu iliyofufuliwa na tamaa ya pesa, ndoa ambayo haitusaidii kupambana na umasikini wa taifa letu, tunajadili mambo yanayojaza kurasa za magazeti ya UDAKU!
Kama taifa tumejishusha na tunajidhalilisha tunapoacha kujadili mstakabali wa uchumi wetu, tunajidhalilisha tunaposhindwa kujadili hoja za wagombea na ilani za vyama vyao, tumekuwa dampo la siasa za maji taka na tunachekelea. Kuna wengi wetu wanafurahia namna ambavyo Dr Slaa amebanwa wasijue kuwa wanaoleta hizi habari wanataka waendelee kutunyonya na kutuibia, tumekuwa kama mazuzu na bado hatujaligundua hili.
Tanzania inasifika nje ya nchi kwa nchi yenye wasomi kuliko majirani zao lakini ikiwa ni nchi iliyo nyuma kuliko wote hao kiuchumi (hata Msumbiji itatupita muda si muda) licha ya kuwa na rasilimali lukuki.
Tunaongoza kwa mataifa yanayopokea misaada katika nchi zinazoendelea na tunajisifu kwa hilo, tunajisifu tunaposema kuwa Wamarekani wameshaizinisha pesa kwa ajiri ya kutatua kero zetu, tunafurahia huku bajeti yetu ikiendelea kutegemea hisani ya wafadhili.
Tumeshindwa hata kuwa na vitu vya kujivunia (Kenya wanajivunia Katiba yao mpya na shirika lao la Kenya Airways) sisi tunajivunia kuyauza mashirika yaliyotuletea heshima kama taifa na tumeridhika, tunataka kuirudisha madarakani serikali hiyo hiyo iliyoshindwa kuzitatua changamoto za taifa hili, tunakubali kutumika kama mifagio ya choo ambayo haiwezi hata kutunzwa sebuleni, sehemu yetu ni huko huko ****** na tunafurahia!
Wakati Rais Clinton akikabiliwa na tuhuma za ufusika akiwa Ikulu, wananchi waliowengi wa Marekani walimuangalia Clinton kama mtendaji mkuu wa nchi na si kama mwanaume aliyeisaliti ndoa yake. Waliangalia ameifanyia nini Marekani kabla ya kuangalia maisha yake ya ndoa. Mwisho wa siku walizipuuza tuhuma zile na kumuunga mkono Rais wao.
Ninawasihi watanzania wote tuzipuuze tuhuma hizi za maisha binafsi ya Slaa na tuangalie utendaji wake wa kazi. Tusijishushe kiasi kile na kuwaruhusu maadui wetu watushinde kwa kututupia pipi, tunastahili zaidi ya hapo!
Hata hivyo, magenge ya majasusi yakiongozwa na Jangili Rostam yalijua kama hilo lingelitokea wangelijikuta ama wanakimbia nchi au wanapata vyumba katika magereza yetu. Hawakutaka vyote viwili na walijua kuwa mtu waliyemtaka achukue Urais hakuwa na sifa za kiutendaji, kwa wengi Kikwete alionekana kama brother man fulani ambaye mahala pake ilikuwa ni vijiwe vya mjini na kwenye kumbi za starehe, haiba yake na utendaji wake wa kazi wa nyuma haukuonyesha kuwa huyu alikuwa rais mtarajiwa.
Wafuasi wake walilitambua hilo vyema na wakabuni mbinu ambazo zingelimuuza huyu kwa wapiga kura (walinunua vyombo vya habari na kuwalipa wanahabari kulifanikisha hili), lakini pia walibuni mbinu za kuwaengua wagombea wengine wote waliokuwa na sifa stahili na ambao walionekana kuwa ni kikwazo kwa mgombea wao. Katika wagombea wote wa kura za maoni, Dr Salmin ndiye alikuwa tishio kubwa na walifanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kuwa wanamchafua ipasavyo.
Wahariri wa magazeti walilipwa kuhakikisha kuwa habari za wagombea zilimsifia mgombea wao, Kikwete, propaganda za chini chini zilipenyezwa na kutuaminisha kuwa Salmin alishiriki kumuua Karume Snr na alikuwa hafai kupewa nchi. Tukaambiwa kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu, akina sisi tulijua tunapotoshwa na tuliwapuuza waliokuwa wakimsifia, lakini walifanikiwa kuwavuna wengi na wakafanikiwa kumuweka Kikwete madarakani kwa kura nyingi.
Kwa sababu Dr Salmin hakujiandaa kwa siasa za kihuni namna hii, aliangushwa vibaya na matokeo yake wote tunayafahamu.
Baada ya kuingia Ikulu walibuni mbinu mbalimbali za kuhakikisha kuwa wanavuna ipasavyo, wakaja na Richmond (baada ya kufanikiwa kuchota za EPA).
UCHAGUZI wa 2010 umeleta changamoto zinazofanana na zile za 2005 lakini sasa wamekuja na mbinu mpya.
Baada ya kuikagua CV ya Mh Slaa wasione mawaa wala dosari yoyote katika utendaji kazi wake wamempata akiishi na mama aliyeolewa na kuachana na mme wake wa awali na kulifanya kuwa mtaji wao mkubwa.
Wamewahamisha watanzania kutoka kwenye mijadala ya muhimu na ya msingi ya kuangalia ni nini wagombea wanataka kuifanyia Tanzania na wanaweza kiasi gani, wametuhamisha kutoka kwenye mijadala ya je haya anayosema Kikwete na CCM watayafanya wanaweza na wanaoutashi wa kuyafanya? Je ni kwa nini hawakuyafanya au hata kuonyesha jitihada za kutaka kuyafanya kwa kipindi walichokuwa madarakani miaka mitano inayomalizika? Wametukosesha fursa ya kutafakari na kujadili ni yupi kati ya wagombea wa upinzani anaweza kuyatekeleza yale anayoyasema? Je Dr Slaa ataweza kulishughulikia suala la ufisadi kwa nguvu zile zile alizolishughulikia akiwa mbunge wa upinzani? Je anao utashi na uwezo kuzitatua kero zilizoishinda serikali ya CCM?
Badala yake wametupeleka kwenye mijadala ya kitoto na isiyotusaidia kupata kiongozi atakaye shughulikia kero zetu, sasa tunajadili ndoa mfu iliyofufuliwa na tamaa ya pesa, ndoa ambayo haitusaidii kupambana na umasikini wa taifa letu, tunajadili mambo yanayojaza kurasa za magazeti ya UDAKU!
Kama taifa tumejishusha na tunajidhalilisha tunapoacha kujadili mstakabali wa uchumi wetu, tunajidhalilisha tunaposhindwa kujadili hoja za wagombea na ilani za vyama vyao, tumekuwa dampo la siasa za maji taka na tunachekelea. Kuna wengi wetu wanafurahia namna ambavyo Dr Slaa amebanwa wasijue kuwa wanaoleta hizi habari wanataka waendelee kutunyonya na kutuibia, tumekuwa kama mazuzu na bado hatujaligundua hili.
Tanzania inasifika nje ya nchi kwa nchi yenye wasomi kuliko majirani zao lakini ikiwa ni nchi iliyo nyuma kuliko wote hao kiuchumi (hata Msumbiji itatupita muda si muda) licha ya kuwa na rasilimali lukuki.
Tunaongoza kwa mataifa yanayopokea misaada katika nchi zinazoendelea na tunajisifu kwa hilo, tunajisifu tunaposema kuwa Wamarekani wameshaizinisha pesa kwa ajiri ya kutatua kero zetu, tunafurahia huku bajeti yetu ikiendelea kutegemea hisani ya wafadhili.
Tumeshindwa hata kuwa na vitu vya kujivunia (Kenya wanajivunia Katiba yao mpya na shirika lao la Kenya Airways) sisi tunajivunia kuyauza mashirika yaliyotuletea heshima kama taifa na tumeridhika, tunataka kuirudisha madarakani serikali hiyo hiyo iliyoshindwa kuzitatua changamoto za taifa hili, tunakubali kutumika kama mifagio ya choo ambayo haiwezi hata kutunzwa sebuleni, sehemu yetu ni huko huko ****** na tunafurahia!
Wakati Rais Clinton akikabiliwa na tuhuma za ufusika akiwa Ikulu, wananchi waliowengi wa Marekani walimuangalia Clinton kama mtendaji mkuu wa nchi na si kama mwanaume aliyeisaliti ndoa yake. Waliangalia ameifanyia nini Marekani kabla ya kuangalia maisha yake ya ndoa. Mwisho wa siku walizipuuza tuhuma zile na kumuunga mkono Rais wao.
Ninawasihi watanzania wote tuzipuuze tuhuma hizi za maisha binafsi ya Slaa na tuangalie utendaji wake wa kazi. Tusijishushe kiasi kile na kuwaruhusu maadui wetu watushinde kwa kututupia pipi, tunastahili zaidi ya hapo!