Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Kampuni ya Mwananchi communication iliyokuwa inamilikiwa kwa pamoja kati ya watanzania na wakenya sasa inamilikiwa kwa asilimia 100 na wakenya .
Habari za kuaminika toka kwa watu mbali mbali waliomo ndani ya kampuni hiyo zinasema umiliki ulikamilika wiki iliyopita , umiliki huo kwa sasa uko chini ya National Media Group baada ya kukamilisha malipo ya hisa kutoka kwa wamiliki wazalendo .
Mmiliki mzalendo ambaye pia ni mbunge wa igunga mhe rostam aziz alilipwa kiasi cha shilingi mil 750 wiki iliyopita kuiwezesha national media group inayomilikiwa kwa kiasi Fulani na agha khan foundation kumiliki kampuni hiyo
Mwananchi communication pia imepata piga baada ya kuondokewa na baadhi ya waandishi wake 15 katika kipindi hicho cha wiki moja kutokana na sababu za kimasilahi , waandishi hao wamejiunga na vyombo mbali mbali vya habari jijini dare s salaam .
Baadhi ya maofisa wa serikali wanasema hawakubaliani na uamuzi wa kuwepo umiliki huu lakini haijulikani walikuwa wapi wakati rostam anakabidhi hizo hisa kwa kampuni ya national media au kama kweli wako makini katika kufuatilia umiliki wa kampuni za kigeni hapa nchini , inatia mashaka kuhusu kuwajibika kwao huku .
Kulingana na sheria ya vyombo vya habari , hairuhusiwi chombo chochote kumilikiwa kwa asilimia 100 na kampuni au muwekezaji wowote kutoka nje , umiliki au ubia unatakiwa usizidi asilimia 49 wachambuzi mbali mbali wa mambo wanasema sasa mwananchi imerudi kule kule ilipotoka nyumbani kwao
Na sasa wale wakenya waliofukuzwa kazi wakati ile kwa kufanya kazi na chombo hicho bila vibali vya uhakika wataweza kurudi tena na kuongezwa wengine zaidi
Gazeti la mwananchi ndio gazeti linaloongoza kwa mauzo kwa sasa nchini Tanzania kwa mwagazeti ya Kiswahili na kwa habari za michezo gazeti la mwanaspoti ndio linaongoza kwa mauzo .
Habari za kuaminika toka kwa watu mbali mbali waliomo ndani ya kampuni hiyo zinasema umiliki ulikamilika wiki iliyopita , umiliki huo kwa sasa uko chini ya National Media Group baada ya kukamilisha malipo ya hisa kutoka kwa wamiliki wazalendo .
Mmiliki mzalendo ambaye pia ni mbunge wa igunga mhe rostam aziz alilipwa kiasi cha shilingi mil 750 wiki iliyopita kuiwezesha national media group inayomilikiwa kwa kiasi Fulani na agha khan foundation kumiliki kampuni hiyo
Mwananchi communication pia imepata piga baada ya kuondokewa na baadhi ya waandishi wake 15 katika kipindi hicho cha wiki moja kutokana na sababu za kimasilahi , waandishi hao wamejiunga na vyombo mbali mbali vya habari jijini dare s salaam .
Baadhi ya maofisa wa serikali wanasema hawakubaliani na uamuzi wa kuwepo umiliki huu lakini haijulikani walikuwa wapi wakati rostam anakabidhi hizo hisa kwa kampuni ya national media au kama kweli wako makini katika kufuatilia umiliki wa kampuni za kigeni hapa nchini , inatia mashaka kuhusu kuwajibika kwao huku .
Kulingana na sheria ya vyombo vya habari , hairuhusiwi chombo chochote kumilikiwa kwa asilimia 100 na kampuni au muwekezaji wowote kutoka nje , umiliki au ubia unatakiwa usizidi asilimia 49 wachambuzi mbali mbali wa mambo wanasema sasa mwananchi imerudi kule kule ilipotoka nyumbani kwao
Na sasa wale wakenya waliofukuzwa kazi wakati ile kwa kufanya kazi na chombo hicho bila vibali vya uhakika wataweza kurudi tena na kuongezwa wengine zaidi
Gazeti la mwananchi ndio gazeti linaloongoza kwa mauzo kwa sasa nchini Tanzania kwa mwagazeti ya Kiswahili na kwa habari za michezo gazeti la mwanaspoti ndio linaongoza kwa mauzo .