Elections 2010 Rostam Apata Mpinzani wa kweli Igunga!

mpuuzi

Member
May 29, 2010
99
17
KIGOGO wa siku nyingi serikalini, Dk Dalaly Peter Kafumu ametangaza nia ya kuwania kiti cha ubunge cha jimbo la Igunga mkoani Tabora ambako atapambana na mbunge wa sasa, Rostam Aziz.

Uamuzi wa Dk Kafumu, ambaye ni kamishna wa madini, kutangaza nia hiyo kinamuweka Rostam, ambaye amekuwa mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 1995, kwenye hali ngumu zaidi baada ya mtalaamu wa tiba asilia, Bakari Nyorabi kutangaza pia nia ya kutaka kiti hicho kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba.


Wote watatu wanawania kiti hicho kwa tiketi ya CCM, hali ambayo itafanya kuwepo kwa mpambano mkali safari hii baada ya mweka hazina huyo wa zamani wa chama tawala kupita bila ya kupingwa mwaka 2005.


Nyorabi aliwaambia waandishi wa habari kuwa ameamua kuwania ubunge wa jimbo hilo baada ya kuona kero nyingi hazijatatuliwa kwa muda mrefu sasa.

Lakini Dk Kafumu alisema jana wakati akitangaza nia hiyo kuwa wakati umefika kwa Rostam kuachia ngazi ili kutoa fursa kwa mawazo mapya kuchangia maendeleo ya wilaya hiyo.


Alisema miaka 15 ya Rostam kuwa mbunge wa jimbo hilo imetosha na sasa anapaswa kuwapisha wengine waleta mawazo mapya.


Dk Kafumu alisema wilaya ya Igunga iko nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na wilaya nyingine zote za mkoa wa Tabora.

Alisema licha ya serikali na wahisani kutoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo kwa miaka kumi iliyopita, maisha ya wafugaji na wakulima yamezidi kudidimia huku wengine wakiikimbia wilaya hiyo kwa ukame kwenda mikoa ya kusini.

Aliongeza kuwa amegundua kuwa tatizo hilo limetokana na pengo kubwa la usimamiaji rasilimali na ubunifu mipango katika kuharakisha kasi ya maendeleo wilayani humo.


Kwa mujibu wa Dk Kafumu, mbali na jitihada za serikali na wahisani kutaka kuisaidia wilaya hiyo kimaendeleo, miradi mingi haitekelezwi kwa faida za wananchi bali kuwanufaisha wajanja wachache.


"Ipo hatari kudhani ubunge ni fursa ya kikundi au mtu fulani tu kama ufalme na kusahau kuwa maendeleo ya kweli huletwa na kila mwanajimbo na mkazi kupitia demokrasia kwa kuunganisha mawazo mapya, nguvu mpya, kasi na ari mpya, chini ya usimamizi na ushirikiano wa chama na serikali kupitia ilani yake na sera za kutokomeza umaskini," alisema Dk Kafumu.


Dk Kafumu aliongeza kuwa Rostam atapata heshima kubwa endapo ataondoka akiwa bado anapendwa na wapigakura wake kuliko kusubiri wamchoke kwa kuwa jimbo la Igunga linahitaji mawazo mapya na mikakati tofauti kabisa katika kujiletea maendeleo.


Dk Kafumu alizaliwa mwaka 1957, katika kijiji cha Itumba wilayani Igunga mkoani Tabora.


Alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi ya Itumba na baadaye kusoma Shule ya Sekondari ya Mirambo na Mkwawa, kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1980 ambako alipata shahada ya kwanza ya sayansi ya jiolojia.

Mwaka 2000, Dk Kafumu alijiunga na Chuo Kikuu cha Free University cha Brussels nchini Ubelgiji ambako alisoma shahada za uzamili na uzamivu katika masomo ya jiolojia.


Alimaliza masomo hayo mwaka 2004 na kurudi nchini ambako kuanzia mwaka 2006, rais alimteua kuwa kamishina wa madini.


Chanzo: Gazeti la Mwananchi
 
Vipi Dr Kafumu ina maana hayukoo kwenye pay roll ya RA?? RA ana uwezo wa kuipanga serikali (akiwemo na dr kafumu kwenye hicho cheo) iweje leo ashindwe ubungee kirahisii??? haijaniingia akilinii badoo...makamba alishampigia debe, Pinda akakolezaa bado JK kumfagiliaaa..
 
Hodi hodi wana JF, Igunga tunaelekea kubakwa kwa staili ya aina yake hivyo JF tusaidiane kuchambua taratibu na tujue kilichomo katika nia ya ndugu yetu Dr kafumu kama ambavyo anajaribu kutuaminisha hapa chini kuwa yeye haji kwa kivuli cha Rostam.....lakini kusikitisha kila nikiingia kwenye google Doctor Kafumu anaonekana kila penye dalili za uchafu na ufisadi wa madini na nafikiri wakati uchafu wote wa mikataba mibovu ikifanyika nafikiri yeye alikuwa Zonal Commisioner Mwanza na kama vile JK alikuwa waziri wa madini na kwa nyuma yao nafikiri thinktank Rostam alikuwa anawaza kumvusha JK 2005, waheshimiwa wa JF hapa tusaidiane kukokotoa mbivu na mbichi
icon3.png


Kigogo wa serikali amvaa Rostam


Tuesday, 15 June 2010 12:26
Herman Meza, Igunga
Rostam Aziz
KIGOGO wa siku nyingi serikalini, Dk Dalaly Peter Kafumu ametangaza nia ya kuwania kiti cha ubunge cha jimbo la Igunga mkoani Tabora ambako atapambana na mbunge wa sasa, Rostam Aziz.

Uamuzi wa Dk Kafumu, ambaye ni kamishna wa madini, kutangaza nia hiyo kinamuweka Rostam, ambaye amekuwa mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 1995, kwenye hali ngumu zaidi baada ya mtalaamu wa tiba asilia, Bakari Nyorabi kutangaza pia nia ya kutaka kiti hicho kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba.

Wote watatu wanawania kiti hicho kwa tiketi ya CCM, hali ambayo itafanya kuwepo kwa mpambano mkali safari hii baada ya mweka hazina huyo wa zamani wa chama tawala kupita bila ya kupingwa mwaka 2005.
Nyorabi aliwaambia waandishi wa habari kuwa ameamua kuwania ubunge wa jimbo hilo baada ya kuona kero nyingi hazijatatuliwa kwa muda mrefu sasa.

Lakini Dk Kafumu alisema jana wakati akitangaza nia hiyo kuwa wakati umefika kwa Rostam kuachia ngazi ili kutoa fursa kwa mawazo mapya kuchangia maendeleo ya wilaya hiyo.

Alisema miaka 15 ya Rostam kuwa mbunge wa jimbo hilo imetosha na sasa anapaswa kuwapisha wengine waleta mawazo mapya.
Dk Kafumu alisema wilaya ya Igunga iko nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na wilaya nyingine zote za mkoa wa Tabora.
Alisema licha ya serikali na wahisani kutoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo kwa miaka kumi iliyopita, maisha ya wafugaji na wakulima yamezidi kudidimia huku wengine wakiikimbia wilaya hiyo kwa ukame kwenda mikoa ya kusini.

Aliongeza kuwa amegundua kuwa tatizo hilo limetokana na pengo kubwa la usimamiaji rasilimali na ubunifu mipango katika kuharakisha kasi ya maendeleo wilayani humo.

Kwa mujibu wa Dk Kafumu, mbali na jitihada za serikali na wahisani kutaka kuisaidia wilaya hiyo kimaendeleo, miradi mingi haitekelezwi kwa faida za wananchi bali kuwanufaisha wajanja wachache.

"Ipo hatari kudhani ubunge ni fursa ya kikundi au mtu fulani tu kama ufalme na kusahau kuwa maendeleo ya kweli huletwa na kila mwanajimbo na mkazi kupitia demokrasia kwa kuunganisha mawazo mapya, nguvu mpya, kasi na ari mpya, chini ya usimamizi na ushirikiano wa chama na serikali kupitia ilani yake na sera za kutokomeza umaskini," alisema Dk Kafumu.

Dk Kafumu aliongeza kuwa Rostam atapata heshima kubwa endapo ataondoka akiwa bado anapendwa na wapigakura wake kuliko kusubiri wamchoke kwa kuwa jimbo la Igunga linahitaji mawazo mapya na mikakati tofauti kabisa katika kujiletea maendeleo.

Dk Kafumu alizaliwa mwaka 1957, katika kijiji cha Itumba wilayani Igunga mkoani Tabora.
Alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi ya Itumba na baadaye kusoma Shule ya Sekondari ya Mirambo na Mkwawa, kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1980 ambako alipata shahada ya kwanza ya sayansi ya jiolojia.

Mwaka 2000, Dk Kafumu alijiunga na Chuo Kikuu cha Free University cha Brussels nchini Ubelgiji ambako alisoma shahada za uzamili na uzamivu katika masomo ya jiolojia.
Alimaliza masomo hayo mwaka 2004 na kurudi nchini ambako kuanzia mwaka 2006, rais alimteua kuwa kamishina wa madini.

Angalia na hapa chini
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/5871-tanzania-one-haina-mkataba-print.html
 
Dr Kafumu ni pandikizi tu - haipendeze RA apite bila kupingwa kwa mara ya pili
 
Kafumu ni mnafiki huyo, hana lolote, yeye ndio mwenyewe alimwachia RA na malipo yake ndio akapewa hicho cheo cha Kamishina wa Madini, na ndio Nguzo kubwa ya Mikataba mibovu ya madini kwani yupo kwenye pay roll ya RA na automatically akawa na Kalamagi na sasa Ngereja, Kwanza inabidi awaombe radhi Watanzania kwani ana Kesi kubwa ya kujibu kwa Watanzania
 
Niliwahi soma article fulani ya Tundu Lissu kuwa Dr Kafumu alishiriki kufukuza wanainchi waliokuwa wakiishi kwenye eneo la mgodi fulani na kuwaambia kuwa hawatalipwa chochote kwani nyumba zao hazina samani nani sawa na choo tu, maneno hayo aliwaambia wasukuma wenzie huko kanda ya ziwa....Hakika anakiburi kama walewale
 
Vipi Dr Kafumu ina maana hayukoo kwenye pay roll ya RA?? RA ana uwezo wa kuipanga serikali (akiwemo na dr kafumu kwenye hicho cheo) iweje leo ashindwe ubungee kirahisii??? haijaniingia akilinii badoo...makamba alishampigia debe, Pinda akakolezaa bado JK kumfagiliaaa..


Mkuu hii ya Dr Kafumu na RA hata mgambo wa jiji anauwezo wa kung'amua nini kimo ndani ya pakacha, hiyo trend uliyoitaja hapo juu inajaribu kutoa picha halisi na sio maneno ya Kafumu kama anavyojaribu kudanganya,
 
labda wamesahau historia.... Kafumu alitaka kurithi kiti cha yule mbunge wa Igunga aliyefariki... na watu walitegemea yeye ndiye angegombea... kutoka kusikojulikana akaja "kijana wetu" Rostam.

Tukirudi siku ile tutajua ni kwanini... ili kumtuliza Peter akapewa ukamishna pale na kutakiwa kutulia... hata sasa hivi sitoshangaa RA asigombee ili ampishe Peter kwani ni salama zaidi hapo..
 
Hivi RA si alisema hagombei tena? Wanasiasa hawaaminiki, huenda kaona cheo kizuri.

Ile sheria ya siasa na biashara naona imekufa kwasasa.
 
labda wamesahau historia.... Kafumu alitaka kurithi kiti cha yule mbunge wa Igunga aliyefariki... na watu walitegemea yeye ndiye angegombea... kutoka kusikojulikana akaja "kijana wetu" Rostam.

Tukirudi siku ile tutajua ni kwanini... ili kumtuliza Peter akapewa ukamishna pale na kutakiwa kutulia... hata sasa hivi sitoshangaa RA asigombee ili ampishe Peter kwani ni salama zaidi hapo..

MMK,Dr Kafumu sio mtu easy au pandikizi kama baadhi ya watu humu wanavyofikiri,ni mtu makini ambaye nafasi anayoishikilia ya Kamishna wa Madini hakupewa kwa upendeleo bali ni kwa sababu ya elimu kubwa aliyonayo na uchapakazi uliotukuka!

MMK;Chukua maneno yangu na ipo siku utakuja kunikumbuka,hapo alipo RA ana wasiwasi sana maana anajua sasa mpinzani wa ukweli kaingia sio hawa geresha wengine waliotangaza kabla ya Dr Kafumu!

Dr Kafumu anaweza kabisa kumbwaga RA kwenye kura za maoni ndani ya CCM hasa baada ya kubadili mfumo wa jinsi ya kuwapigia kura wagombea wao,lkn wasiwasi wangu je kamati kuu itakubali RA mtu wao aende na maji?
 
MMK,Dr Kafumu sio mtu easy au pandikizi kama baadhi ya watu humu wanavyofikiri,ni mtu makini ambaye nafasi anayoishikilia ya Kamishna wa Madini hakupewa kwa upendeleo bali ni kwa sababu ya elimu kubwa aliyonayo na uchapakazi uliotukuka!

MMK;Chukua maneno yangu na ipo siku utakuja kunikumbuka,hapo alipo RA ana wasiwasi sana maana anajua sasa mpinzani wa ukweli kaingia sio hawa geresha wengine waliotangaza kabla ya Dr Kafumu!

Dr Kafumu anaweza kabisa kumbwaga RA kwenye kura za maoni ndani ya CCM hasa baada ya kubadili mfumo wa jinsi ya kuwapigia kura wagombea wao,lkn wasiwasi wangu je kamati kuu itakubali RA mtu wao aende na maji?

Malafyale.. nafahamu kwa uhakika kabisa kuwa ni kweli amebobea katika fani yake na sihoji hata kidogo yeye kuwa katika nafasi hiyo. Lakini haikuja bila compromise. Alikubali kucompromise RA alipogembea mara ya kwanza. Sijui kama unakumbuka...
 
Malafyale.. nafahamu kwa uhakika kabisa kuwa ni kweli amebobea katika fani yake na sihoji hata kidogo yeye kuwa katika nafasi hiyo. Lakini haikuja bila compromise. Alikubali kucompromise RA alipogembea mara ya kwanza. Sijui kama unakumbuka...

Na safari hii pia wamecompromise ili Kafumu apande zaidi kupitia ubunge kwani siku zote RA hutaka kuwa kwenye cover za watu type yake Dr(uwaziri?) halafu kwa kuwa Mkulu alishashauri kutenganisha siasa na biashara basi RA atashuka ulingoni huku akiwa na mtu wake atakayemlindia maslahi yake chamani na serikalini, kama ulivyosema Mkjj tuangalie historia kwa kuanzia pale Mzee kabeho alipofariki kilitokea nini mpaka Dr akajitoa?
 
"Ipo hatari kudhani ubunge ni fursa ya kikundi au mtu fulani tu kama ufalme na kusahau kuwa maendeleo ya kweli huletwa na kila mwanajimbo na mkazi kupitia demokrasia kwa kuunganisha mawazo mapya, nguvu mpya, kasi na ari mpya, chini ya usimamizi na ushirikiano wa chama na serikali kupitia ilani yake na sera za kutokomeza umaskini," alisema Dk Kafumu.

Huyu naye hana jipya, probably, delusional.
 
huyo ni porokwa mwingine au shibuda mwingine. siku chache kabla ya kuchukua fomu atatangaza kuachia ngazi. time will tell. just wait and see.
 
MMK,Dr Kafumu sio mtu easy au pandikizi kama baadhi ya watu humu wanavyofikiri,ni mtu makini ambaye nafasi anayoishikilia ya Kamishna wa Madini hakupewa kwa upendeleo bali ni kwa sababu ya elimu kubwa aliyonayo na uchapakazi uliotukuka!

MMK;Chukua maneno yangu na ipo siku utakuja kunikumbuka,hapo alipo RA ana wasiwasi sana maana anajua sasa mpinzani wa ukweli kaingia sio hawa geresha wengine waliotangaza kabla ya Dr Kafumu!

Dr Kafumu anaweza kabisa kumbwaga RA kwenye kura za maoni ndani ya CCM hasa baada ya kubadili mfumo wa jinsi ya kuwapigia kura wagombea wao,lkn wasiwasi wangu je kamati kuu itakubali RA mtu wao aende na maji?

Hapo kwenye nyekundu sikweli kabisa , hiyo nafasi ya Kamishna wa Madini ilikuwa apewe .Eng Masanja, ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa TMAA (Tanzania Mineral Auditing Agency), lakini zengwe lilikuwa ni kubwa, Amini usiamini kwa asilimia kama 90 RA alihusika kukipanga kikosi cha Wizara ya Nishati na MAdini kwa interest yake, na baada ya Eng Masanja kukosa mwelekeo ilibidi serikali itafute kwa Kumpeleka kwani ilikuwa sio rahisi kwa yeye kuwa na Kafumu Ofisi MojA, na ndipo hicho kitengo cha Ugaguzi wa Dhahabu (By then) kikaanzishwa kuchukua nafasi ya ALex Stewert na masanja ndio akapewa kukiongoza hicho kitengo as kumplease, RA na hii nchi ni zaidi ya tunavyomjua
 
Sishangai hii yote yawezekana kwa nchi zinazoongozwa kwa CARTEL SYSTEM kama TZ
 
MMK,Dr Kafumu sio mtu easy au pandikizi kama baadhi ya watu humu wanavyofikiri,ni mtu makini ambaye nafasi anayoishikilia ya Kamishna wa Madini hakupewa kwa upendeleo bali ni kwa sababu ya elimu kubwa aliyonayo na uchapakazi uliotukuka!

MMK;Chukua maneno yangu na ipo siku utakuja kunikumbuka,hapo alipo RA ana wasiwasi sana maana anajua sasa mpinzani wa ukweli kaingia sio hawa geresha wengine waliotangaza kabla ya Dr Kafumu!

Dr Kafumu anaweza kabisa kumbwaga RA kwenye kura za maoni ndani ya CCM hasa baada ya kubadili mfumo wa jinsi ya kuwapigia kura wagombea wao,lkn wasiwasi wangu je kamati kuu itakubali RA mtu wao aende na maji?

Malafyale Dr Kafumu asilani hawezi kumvaa na kumbwaga RA pale Igunga ila kitakachofanyika ni Rostam kujitoa kabla na kumpigia debe jamaa yake au atajitoa dakika za mwisho na kuhamishia kambi yake kwa Kafumu, bwana wee toka lini kuwadi akamgeuzia kibao bosi wake? Kuhusu ya Kamati kuu ya CCM huko ndio hovyo hovyo kabisa sasa hivi wao ni ngwala kwa ngwala AU jino kwa jino tu & NO formula mpaka uchaguzi upite, umemsikia Anne Kilango kishapeleka malalamiko yake kamati kuu ya CCM na hayajafanyiwa kazi na akina Makamba mpaka sasa anaomba msaada wa M/kiti wao JK, ingawa namie namwona mama kama vile anaelekea kuruka jivu na kukanyaga moto :violin:Mie natoa wito kwa wale wote tunaojuana kutoka Igunga wakati wa kampeni tuwe likizo kusaidia kuepusha balaa linalotaka kutushukia
 
Kwahiyo RA ni mtu makini sana na ana akili sana kuzidi wadanganyika wengi na ndio maana anaweza kupanga Taifa liende vipi hata wana JF wote wanaonekana mbumbumbu kwa huyu jamaa!Ama kweli urofa hatari!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom