mpuuzi
Member
- May 29, 2010
- 99
- 17
KIGOGO wa siku nyingi serikalini, Dk Dalaly Peter Kafumu ametangaza nia ya kuwania kiti cha ubunge cha jimbo la Igunga mkoani Tabora ambako atapambana na mbunge wa sasa, Rostam Aziz.
Uamuzi wa Dk Kafumu, ambaye ni kamishna wa madini, kutangaza nia hiyo kinamuweka Rostam, ambaye amekuwa mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 1995, kwenye hali ngumu zaidi baada ya mtalaamu wa tiba asilia, Bakari Nyorabi kutangaza pia nia ya kutaka kiti hicho kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba.
Wote watatu wanawania kiti hicho kwa tiketi ya CCM, hali ambayo itafanya kuwepo kwa mpambano mkali safari hii baada ya mweka hazina huyo wa zamani wa chama tawala kupita bila ya kupingwa mwaka 2005.
Nyorabi aliwaambia waandishi wa habari kuwa ameamua kuwania ubunge wa jimbo hilo baada ya kuona kero nyingi hazijatatuliwa kwa muda mrefu sasa.
Lakini Dk Kafumu alisema jana wakati akitangaza nia hiyo kuwa wakati umefika kwa Rostam kuachia ngazi ili kutoa fursa kwa mawazo mapya kuchangia maendeleo ya wilaya hiyo.
Alisema miaka 15 ya Rostam kuwa mbunge wa jimbo hilo imetosha na sasa anapaswa kuwapisha wengine waleta mawazo mapya.
Dk Kafumu alisema wilaya ya Igunga iko nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na wilaya nyingine zote za mkoa wa Tabora.
Alisema licha ya serikali na wahisani kutoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo kwa miaka kumi iliyopita, maisha ya wafugaji na wakulima yamezidi kudidimia huku wengine wakiikimbia wilaya hiyo kwa ukame kwenda mikoa ya kusini.
Aliongeza kuwa amegundua kuwa tatizo hilo limetokana na pengo kubwa la usimamiaji rasilimali na ubunifu mipango katika kuharakisha kasi ya maendeleo wilayani humo.
Kwa mujibu wa Dk Kafumu, mbali na jitihada za serikali na wahisani kutaka kuisaidia wilaya hiyo kimaendeleo, miradi mingi haitekelezwi kwa faida za wananchi bali kuwanufaisha wajanja wachache.
"Ipo hatari kudhani ubunge ni fursa ya kikundi au mtu fulani tu kama ufalme na kusahau kuwa maendeleo ya kweli huletwa na kila mwanajimbo na mkazi kupitia demokrasia kwa kuunganisha mawazo mapya, nguvu mpya, kasi na ari mpya, chini ya usimamizi na ushirikiano wa chama na serikali kupitia ilani yake na sera za kutokomeza umaskini," alisema Dk Kafumu.
Dk Kafumu aliongeza kuwa Rostam atapata heshima kubwa endapo ataondoka akiwa bado anapendwa na wapigakura wake kuliko kusubiri wamchoke kwa kuwa jimbo la Igunga linahitaji mawazo mapya na mikakati tofauti kabisa katika kujiletea maendeleo.
Dk Kafumu alizaliwa mwaka 1957, katika kijiji cha Itumba wilayani Igunga mkoani Tabora.
Alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi ya Itumba na baadaye kusoma Shule ya Sekondari ya Mirambo na Mkwawa, kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1980 ambako alipata shahada ya kwanza ya sayansi ya jiolojia.
Mwaka 2000, Dk Kafumu alijiunga na Chuo Kikuu cha Free University cha Brussels nchini Ubelgiji ambako alisoma shahada za uzamili na uzamivu katika masomo ya jiolojia.
Alimaliza masomo hayo mwaka 2004 na kurudi nchini ambako kuanzia mwaka 2006, rais alimteua kuwa kamishina wa madini.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Uamuzi wa Dk Kafumu, ambaye ni kamishna wa madini, kutangaza nia hiyo kinamuweka Rostam, ambaye amekuwa mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 1995, kwenye hali ngumu zaidi baada ya mtalaamu wa tiba asilia, Bakari Nyorabi kutangaza pia nia ya kutaka kiti hicho kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba.
Wote watatu wanawania kiti hicho kwa tiketi ya CCM, hali ambayo itafanya kuwepo kwa mpambano mkali safari hii baada ya mweka hazina huyo wa zamani wa chama tawala kupita bila ya kupingwa mwaka 2005.
Nyorabi aliwaambia waandishi wa habari kuwa ameamua kuwania ubunge wa jimbo hilo baada ya kuona kero nyingi hazijatatuliwa kwa muda mrefu sasa.
Lakini Dk Kafumu alisema jana wakati akitangaza nia hiyo kuwa wakati umefika kwa Rostam kuachia ngazi ili kutoa fursa kwa mawazo mapya kuchangia maendeleo ya wilaya hiyo.
Alisema miaka 15 ya Rostam kuwa mbunge wa jimbo hilo imetosha na sasa anapaswa kuwapisha wengine waleta mawazo mapya.
Dk Kafumu alisema wilaya ya Igunga iko nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na wilaya nyingine zote za mkoa wa Tabora.
Alisema licha ya serikali na wahisani kutoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo kwa miaka kumi iliyopita, maisha ya wafugaji na wakulima yamezidi kudidimia huku wengine wakiikimbia wilaya hiyo kwa ukame kwenda mikoa ya kusini.
Aliongeza kuwa amegundua kuwa tatizo hilo limetokana na pengo kubwa la usimamiaji rasilimali na ubunifu mipango katika kuharakisha kasi ya maendeleo wilayani humo.
Kwa mujibu wa Dk Kafumu, mbali na jitihada za serikali na wahisani kutaka kuisaidia wilaya hiyo kimaendeleo, miradi mingi haitekelezwi kwa faida za wananchi bali kuwanufaisha wajanja wachache.
"Ipo hatari kudhani ubunge ni fursa ya kikundi au mtu fulani tu kama ufalme na kusahau kuwa maendeleo ya kweli huletwa na kila mwanajimbo na mkazi kupitia demokrasia kwa kuunganisha mawazo mapya, nguvu mpya, kasi na ari mpya, chini ya usimamizi na ushirikiano wa chama na serikali kupitia ilani yake na sera za kutokomeza umaskini," alisema Dk Kafumu.
Dk Kafumu aliongeza kuwa Rostam atapata heshima kubwa endapo ataondoka akiwa bado anapendwa na wapigakura wake kuliko kusubiri wamchoke kwa kuwa jimbo la Igunga linahitaji mawazo mapya na mikakati tofauti kabisa katika kujiletea maendeleo.
Dk Kafumu alizaliwa mwaka 1957, katika kijiji cha Itumba wilayani Igunga mkoani Tabora.
Alipata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi ya Itumba na baadaye kusoma Shule ya Sekondari ya Mirambo na Mkwawa, kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1980 ambako alipata shahada ya kwanza ya sayansi ya jiolojia.
Mwaka 2000, Dk Kafumu alijiunga na Chuo Kikuu cha Free University cha Brussels nchini Ubelgiji ambako alisoma shahada za uzamili na uzamivu katika masomo ya jiolojia.
Alimaliza masomo hayo mwaka 2004 na kurudi nchini ambako kuanzia mwaka 2006, rais alimteua kuwa kamishina wa madini.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi