Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
hata kama ameamua kurudisha fedha zetu, kwa nini arudishe 'kiaina' kama anavyosema kana ka nsungu! na nani hapa anastahili kuombewa, nchi au watu wa aina yake?
Kama ni hivyo asilimia 99% hatutakiwi kutuoa zaka kanisani
Kama sikosei makanisa ya kikristu hayatambui ufisadi mdogo ama mkubwa kwa namna nyingine msema uongo,mchonganishi,mzinzi mwivi kama RA hukumu ni ileile.
mpinga ngono ama fisadi hukumu ni ile ile SASA kipimo unachompimia mwezako ndicho hichohicho nawe utamiwa.
AZIZI ni FISADI wasema zaka yake ikataliwe je WEWE MZINZI,MLAFI,MWONGO zaka yako ikibaliwe.
NA tena ULE WENU ni Kheri uwe baridi ama moto kuliko yule wa vuguvugu.
Kanisa lishinikizwe lirudishe hizo pesa za fisadi haraka sana, juzi juzi tu makanisa yalikuwa yanakemea mafisadi na ufisadi na kutaka JK awashughulike mafisadi. Leo wanatizama pembeni na kuchukua pesa kutoka kwa fisadi. Viongozi wa Kanisa hilo waache unafiki na kuzirudisha pesa hizo haraka sana au wazipeleke kwenye vituo vya watoto yatima.
ewaaa mama, labda tuestablish kwani yeye dini gani kwanza? Huenda ni muumini wa KKKT?
Kuna Mwenye Simu Ya Askofu Dr Malasusa! Huyu Askofu Anachukia Sana Ufisadi, Na Kama Zimetolewa Kkkt Manake Ni Kwenye Himaya Yake. Tumpigie Tumpe Live Kuwa Hili Halikubaliki
Labda ni mshahara wake je? au ndio tumefikia mahali kwa kuwatenga kabisa katika jamii? basi na huduma zake au za kampuni/shirika nazo zikataliwe katika jamii.
Kama wewe pia unafanya ufisadi basi hustahili kutoa zaka kanisani. Wengine vipato vyetu vinatokana na shughuli ambazo ni za kihalali hatumwibii wala kumdhulumu mtu yeyote, ndiyo maana tunapata jeuri ya kutaka kanisa liache unafiki na kurudisha pesa hizo za fisadi Rostam Aziz.
Sioni sababu yoyote ya wewe kumtetea huyu fisadi, ambaye ufisadi aliofanya unawaathiri Watanzania wengi kwa namna moja au nyingine.
Mnakumbuka A Bible Story, Wakati Akina Mitume Walipokuwa Wanatoa Mapepo Na Kukemea Mashetani, Akatoka Mtu Mmoja Akataka Kununua Kipaji Hicho Kwa Pesa? Rostam Anatak Kulinunua Kanisa, Kama Alivyowanunua Akina Makamba, Chitaliko, Serukamba, Jk, Mamvi N.k
Kamwe Aiachwe Akaikebehi Madhabahu Ya Bwana Wa Majeshi, Kwa Visenti Vyake Vya Ufisadi
Kama wewe pia unafanya ufisadi basi hustahili kutoa zaka kanisani. Wengine vipato vyetu vinatokana na shughuli ambazo ni za kihalali hatumwibii wala kumdhulumu mtu yeyote, ndiyo maana tunapata jeuri ya kutaka kanisa liache unafiki na kurudisha pesa hizo za fisadi Rostam Aziz.
Sioni sababu yoyote ya wewe kumtetea huyu fisadi, ambaye ufisadi aliofanya unawaathiri Watanzania wengi kwa namna moja au nyingine.
naogopa kuingia kwenye udini, kwi kwi kwi.....by the way si unajua ni rafiki yake wakuvanga?labda alishahamishia majeshi huko KKKT? au anataka kudilute effect ya udini kwenye CCM na kuamua kuwa mpendwa?
Exactly mfano wa YESU.
Bwana mmoja alienda kuomba hekaluni akisema tazama bwana mimi mtiifu ,napata kipato kihalali ,tazama nakutolea Zaka kubwa kila wiki.
Na mwingine aliyehesabiwa haki aliomba Tazama bwana mimi nimkosefu mzinzi ,mtu wa dhuluma,muaji mfanya mabaya yote naomba Nirehemu
Yesu alisema hakika nawaambieni huyu jambazi wa pili kahesabiwa haki mbinguni.
Exactly mfano wa YESU.
Bwana mmoja alienda kuomba hekaluni akisema tazama bwana mimi mtiifu ,napata kipato kihalali ,tazama nakutolea Zaka kubwa kila wiki.
Na mwingine aliyehesabiwa haki aliomba Tazama bwana mimi nimkosefu mzinzi ,mtu wa dhuluma,muaji mfanya mabaya yote naomba Nirehemu
Yesu alisema hakika nawaambieni huyu jambazi wa pili kahesabiwa haki mbinguni.
Somo la Yesu limepinda au umelipindisha.
Kwa nini yule mtiifu, mtoa zaka, alizozipata kihalali asihesabiwe haki mbinguni zaidi ya Jambazi aliyetubu?
Tuache udanganyika! Kanisa limekosea hapa na lazima kanisa tulifahamishe hivyo, kwamba hamuwezi kumkemea mtenda dhambi ambaye dhambi alizozifanya zimewaathiri Watanzania wengi wakiwemo waumini wa kanisa hilo. Halafu kanisa linageuka na kuchukua pesa kutoka kwa huyo huyo mtenda dhambi. Ni unafiki na undumila kuwili wa hali ya juu.
Ni lile anaposali Spika Samwel Sitta... (KKKT Kinondoni).
Aichangia kwaya Tshs Milioni 7...Amalizia na kuwaomba waumini kuiombea nchi kwani iko kwenye kipindi kibaya cha watu kutafutana uchawi na kuonesha hali si shwari nchini.
Zaidi tusubiri kutoka vyombo vya nyumbani kwani walikuwepo wengi. Wasipoandika tutaandika!