Ronald Baraka Shelukindo: Nitalichukua jimbo la Bumbuli 2015

attachment.php

Mtoto wa aliyekuwa mbunge wa Bumbuli Bwana Shekukindo yuko kwenye hatua za awali za kujiandaa kulichukua jimbo hilo kwenye uchaguzi ujao wa 2015

Ronald Baraka Shelukindo ambaye ni maarufu kama afisa mwandamizi wa DSTV amesema kuwa anayo nia, uwezo na pia mitazamo mibadala kwa ajili ya jimbu hili.

Tatizo kubwa ambalo wachunguzi wa masuala ya siasa za Bumbuli wanasema linaweza kumkabili Ndugu Baraka ni kutojulikana jimboni ambako kijana January amejizatiti vilivyo kwenye ngazi zote.

Lakini hilo linaonekana haliwezi kumtatiza huyu kijana msomi na mcheshi bwana Baraka kwani tayari kashaanza michakato ya kuandaa mpago kambambe wa kuliendeleza jimbo la Bumbuli

Kwa maoni yangu nadhani vizuri kujitokeza lakini ninachouliza kama January anafanya kazi nzuri kwa nini Baraka Shelukindo asipewe ukuu wa wilaya ili wafanye kazi kama timu ya pamoja?

Imagine Baraka Shelukindo + January Makamba for Bumbuli

hamuoni kama ni dream team na wakaaachana na siasa za bufu za wazee wao?

Mkuu naona umejaribu kutumia akili kujipigia kampeni hapa..ila tatizo ni kuwa m.kwere huwa hasomi hizi thread..mwandikie barua ya maombi ya huo ukuu wa wilaya kabisa..kwani dstv vipi hakulipi??
 
so far makamba keshafanya mengi. Huyu another son aache ubinafsi na chuki kisa tu baba yake alipigwa chini. Nafasi na majukumu aliyo nayo makamba serikalini, bungeni na jimboni huyu dogo wa shelukindo hawezi. Cha msingi aungane tu na 'kaka' yake wawatumikie wana Bumbuli
 
Naona watu mnawaka bure tu hapa........wengine mmefikia hata kunitusi........nashukuru.....mimi nimetoa angalizo kuwa aangalie huu uamuzi wake wa kugombea.....ni kweli kila mtu ana haki ya kugombea wadhifa popote katika nchi hii lakini ila dhana ya ''kujulikana'' kwenu bado ipo......huwezi kutoka Mtera na ukenda kukombea Marangu UKAJIAMINISHA KUSHINDA......mimi hii familia yake naujua vizuri...namjua marehemu mama yake alikuwa nani kule Iringa na hata alikufa vipi ana kuzikwa vipi.........nisingependa kuzungumzia mengi lakini wapinzani wake(MAKAMBAs) wanajua yote haya....na wasambaa wanajali sana hivi vitu mnavyoviona kuwa ni vidogo...nabaki kuamini kuwa atachafuka!!!
 
ok
Kwanza si raia wa Tanzania kama alivyo NAMBUA MLAKI
atagombea vipi ubunge ?

unless TZ inayo dual nationality na anaruhusiwa kugombea ununge

mimi nafurahi kuona vijana wanagombea

du kwani Nambua Mlaki sio raia?
 
1. Oh yeah Januari kaoa Mchagga wao wanauraia huku; lakini yeye kabla ya hapo alitafuta makaratasi ili akae US ufanya Masters Pale DC shule yake ya Bachelors haikuwa DC kwahiyo alikuwa muda kidogo nje ya shule na status

2. Baraka ana watoto 2 na sio 3

3. Kwa sasa Januari hana kibali cha kuja USA

4. Tulisoma na College Pamoja London sasa wewe unasemaje ilikuwa ya kina Kafulila?

5. Utaona Kampeni January hakufanya alifanyiwa na wanafunzi na kuwapa posho

January aliwahonga wagombea ubunge kwa tiketi ya cuf na chadema wakajitoa...ndio akajitangaza amepita bila kupingwa.
Na hii ni kwa maeneo mengi ambayo ccm walijinadi "wamepita bila kupingwa" walicheza mchezo huo mchafu.
next time chadema kuweni makini sana na uchafu huu.
 
so far makamba keshafanya mengi. Huyu another son aache ubinafsi na chuki kisa tu baba yake alipigwa chini. Nafasi na majukumu aliyo nayo makamba serikalini, bungeni na jimboni huyu dogo wa shelukindo hawezi. Cha msingi aungane tu na 'kaka' yake wawatumikie wana Bumbuli

Jamani Embu Tuambie hayo Mengi January aliyoyafanya zaidi ya kuwekewa VISA NON GRANTA hawezi kukanyanga USA kwahiyo hawezi kuteuliwa Waziri Mpaka Issue Iwe Resolved...

Utuambia Amefanya nini Jimboni kwake Tangu achaguliwe? Tushituke !!!
 
so far makamba keshafanya mengi. Huyu another son aache ubinafsi na chuki kisa tu baba yake alipigwa chini. Nafasi na majukumu aliyo nayo makamba serikalini, bungeni na jimboni huyu dogo wa shelukindo hawezi. Cha msingi aungane tu na 'kaka' yake wawatumikie wana Bumbuli

Wote wawili wanajidanganya tu,2015 kunawasomi mazao ya shule za kata wenye 1st degree,masters,phD NA Wazawa wa huko wamejipanga kisawasawa,hawajali pesa wala matunguli.TUSUBIRI NANI ATA 'ONDOLWA'
 
Japo sina uhakika sana ila nadhani January anafanya vema ameanza vizuri kazi yake

Amefanya nini? UMEME MGWASHI NI MPANGO WA WILLIAM.LABDA UJENZI WA OFISI YA MBUNGE NA VYOO VYA SHULE.AHADI KUBWA ATAKAYOTIMIZA NI LAMI TOKA SONI,BUMBULI,DINDIRA,MASHEWA.AKIFANYA HILO NITAMPIGIA SALUTI.
 
hivi kumbe majimbo ni mali ya watu yanachukuliwa tu mtu akitaka duh
Ah si majimbo ya watu bali majimbo ya familia au koo fulani,ni kama uchifu vile kama baba yako (hasa ambao wamewahi kuwa vigogo wa serikali)alikuwa mbunge huwa encourage watoto wao nao kuchukua mikoba yao,kaka siasa za Tanzania siku hizi ni za kurithishana kama ilivyokuwa Kenya enzi za Moi (siku wamebadirika kuwa mbunge lazima uwe kibaraka wa yule anayeonekana ndio mwakilishi wa kabila),na siku hizi ubunge umekuwa kitu cha hovyo hovyo hata madodoki yanapata nafasi ya kuwa wabunge,na wengine ndio hao kazi yao kusinzinzia ,kubinukabinuka n.k
 
Binafsi sioni kwanini Baraka aende kushindana na kijana mwenzake kule wakati ana nafasi ya kufanya mengine mengi tu katika jamii. Lakini kama akiamua, hii ni haki yake kikatiba, and dont under estimate mtu huyu, ana kichwa kizuri sana, anakaa vizuri sana na watu, na ana uwezo mkubwa sana wa kujieleza, na pia ni mzuri sana kwenye issue ya PR. Hii aina maana kwamba January sio mzuri, kwani tunaona uwezo wake mkubwa katika nafasi zake za sasa. January ni hazina kwa taifa hili kama kina Mnyika, Zitto, Shilinde, Halima Mdee, Lissu na wengine wengi tu, na nina uhakika hazina hii itaongezeka zaidi katika uchaguzi mkuu ujao ambapo bila shaka vijana wengi kutoka vyama mbalimbali wataenda kutumia haki zao za kikatiba kuomba ridhaa ya wananchi, kwa lengo la kuikomboa nchi hii ambayo ipo vipande vipande.


Ukisikia kuzibiana ndio huku

Kama baraka anajiona uwezo anao wa kuendeleza bumbuli kwa nini asichukue forms?

Nyinyi kila kitu mnataka ku monopolize hii haiwezekani enzi hizo zishapitwa na wakati
 
Back
Top Bottom