Roma: Nimechagua maisha ya shida

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
ROMA-34.jpg


Nyota wa muziki wa Rap Bongo ‘Rhymes Of Magic Attraction’ Roma amethibitisha fununu za kuwa muziki anaoufanya umekua ni msalaba mzito kwenye maisha yake.

Akizungumza na eNewz Roma alisema kuwa hayo ndiyo maisha aliyoyachagua na ni mwanaharakati anaetetea haki na amani katika taifa lake, maendeleo bora na hicho ndicho kitu kikubwa anachojaribu kukipigania.

“Natamani nipate utawala au uongozi ambao utamfanya Roma asiimbe hip hop na ukiona kila siku Roma anatoa mawe basi ujue bado hatujapata uongozi huo ama utawala huo,” alisema Roma na kuongeza, “Kwa hiyo inabidi niendelee kushindilia ili taifa langu siku moja lione kwamba Roma alikuwa ni mmoja kati ya wapigania haki”.
 
ROMA-34.jpg


Nyota wa muziki wa Rap Bongo ‘Rhymes Of Magic Attraction’ Roma amethibitisha fununu za kuwa muziki anaoufanya umekua ni msalaba mzito kwenye maisha yake.

Akizungumza na eNewz Roma alisema kuwa hayo ndiyo maisha aliyoyachagua na ni mwanaharakati anaetetea haki na amani katika taifa lake, maendeleo bora na hicho ndicho kitu kikubwa anachojaribu kukipigania.

“Natamani nipate utawala au uongozi ambao utamfanya Roma asiimbe hip hop na ukiona kila siku Roma anatoa mawe basi ujue bado hatujapata uongozi huo ama utawala huo,” alisema Roma na kuongeza, “Kwa hiyo inabidi niendelee kushindilia ili taifa langu siku moja lione kwamba Roma alikuwa ni mmoja kati ya wapigania haki”.
POLE KWA KUAMUA KUJIPIGILIA MSUMARI WA MOTO MWENYEWE..
 
Ila nyimbo zake zilichachafya sana awamu ileee...

Sasa, awamu hii najua ina makando kando yake ILA awe makini wanamlia target tu kama CHURA ... Teh!

Akijichanganya wanamla NYUNDO.

Ila alikuwa anafanya kazi nzuri kipindi hicho.
 
Fanya kitu kinachokupa furaha...naimani kile anachokifanya ndicho kinacho mpa furaha...ili mradi hakiharibi maisha yake.
 
afu mbona kama anatengeneza ganja hapo kwny picha au maharage ndo yanazidi kuniathiri!
 
afu mbona kama anatengeneza ganja hapo kwny picha au maharage ndo yanazidi kuniathiri!
Mkuu...inawezekana yakawa maharage..maana mi nimeona ni foil paper na mfuko wa plastic kuashiria labda anapiga kiepe...au na mi ndo nmekariri 1+1...?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom