Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naanza kuwa na wasiwasi na vijana walioko kwenye politics, napata hisia za kushiriki politics, maana wengi wao ni waoga wa kushindana, wanataka mwenzao asishiriki ili wapata mteremko, jamani pandeni mlima! hapo ndipo tutajua kweli mmekomaa na mnastahili kuwa viongozi wa siku za usoni, haiwezekana mfanye siasa za majungu then mseme mnastahili, Malisa na Mavunde kuna kipi ambacho ni tangible kama kipindi cha uongozi wenu? acheni siasa za rejareja. Pigeni mzigo, wanaume gani mnaona kivuli harafu mnakimbia! hamfai hata kuwa viongozi wa familia zenu.
Mtoto Rais Jakaya Kikwete, Riziwan, ambaye yupo Dodoma kuhudhuria vikao vya Kamati ya utekelezaji na Baraza kuu la vijana huko Dodoma amewavuruga vijana wenzake baada ya kuzidiwa hoja na vijana wengi nchi nzima kwenye vikao hivyo, sasa akaanza kutumia nguvu ya mamlaka/dola na mabilioni ya pesa ambayo amejitengenezea katika kipindi hiki cha Urais wa baba yake.
kwanza, anamtumia mtumishi wa UVCCM, Mzee Mipiko kubadilisha muhtasari/minutes za vikao vyote ili kuweza kulinda hoja zake ambazo alishindwa kwenye vikao. na kwasababu maamuzi ya UVCCM bado yanahitaji baraka za baba yake/ mwenyekiti wa chama, basi anataka kupeleka mapendekezo ambayo ni ya kulinda maslahi yake na Membe. bahati mbaya Katibu mkuu Shigela amekuwa makini sana na hata akamtonya Makamu Beno na muhtasari zote zikabadilishwa na zinaendelea kubadilishwa kutokana na mapendekezo ya vikao vya vijana.
pili, katika kujaribu kuanza kufanya kampeni ya watu kwenye uchaguzi nchi nzima na taifa, kwanza ni jambo ambalo linashangaza wengi, kwasababu anafanya kama vile Kikwete anautafuta Urais wa awamu ya tano au labda yeye angaombea. Kwakweli amejenga historia mpya ya familia za marais kwa nchi yetu ya Tanzania. Kwahiyo jana usiku aliwaita MAKATIBU WOTE wa MIKOA wa UVCCM na kuwapatia kila mmoja Tsh MILIONI MOJA, maana yake kama takribani MILIONI 30 jumla, na akwapa maelekezo na kuwatishia wengine kwamba wasipotii, ajira zao zitasitishwa. Haya nia matumizi mabaya sana ya madaraka na fedha za umma. Tunaomba tuikemee wote.
huyu si anataka kugombea ubunge kwenye jimbo la mjomba wake singida magharibi?
ndo maana wakamhonga msaliti ghambaku ili jimbo lisiangukie mikononi mwa chadema sasa yule msaliti wakampa ukuu wa wilaya huko usukumani.
huyu mtoto ni kirusi kibaya sana katika nchi yetu.