Risk Assessment and Management: CHADEMA nayo Imuondoe Dr. W. Slaa!

Natumaini hiki ulichosema hapo juu kimetoka kwenye mwitikio wa kihisia (emotional response) na siyo kutoka katika mwitikio wa kiakili (a rational response) kwani inasema mengi:

a. Umejuaje Waislamu "hawawataki"?
b. Waislamu gani hawawataki?
c. Kwanini ni Waislamu tu hawawataki?
d. Je ndani ya Chadema kuna muislamu yeyote?
e. Kama kuna muislamu japo hata mmoja - inaweza vipi kusemwa kuwa "waislamu hawawataki"?
f. Unafikiri Dr. Slaa akiondoka ndio Waislamu wataitaka hata kama haiwakilishi maslahi yao?

Nadhani ni hoja nyingine ambayo ni extremely prejudicial, biased and inherently offensive. Yaani, kukubalikwa kwa Chadema kunapimwa na kukubakika na Waislamu? Sasa wakimuondoa Dr. Slaa halafu waislamu wakakubali na Wakristu wakianza kukimbia wamuondoe huyo mtu mwingine ili wakubalike na "wakristu". Yaani, hatuna kanuni tena isipokuwa kufanya mambo kwa kujaribu kuridhishana tu?

Kuita majibu ya watu wengine wasiokubaliana nwewe kuwa ni "ujinga" ni kujaribu kulazimisha hoja pale ambao umeshindwa kusimamia hoja yako.

Nyerere aliposema nchi inakosa wasomi akumanisha watu weliofika chuo au maprofesa kama wengi walivyomuelewa vibaya, ila alimanisha people who can think critically like you, big up.
 
Yaani mtu aliyewafanya wakubalike zaidi na kupata kura zaidi na kuwa chama cha kitaifa zaidi ndio aondolewe? Well.. itakuwa ni kufanya mambo kinyume nyume. Wenzenu wameondoa watu waliokiletea chama matatizo siyo waliokijenga. Sasa pendekezo kuwa Dr. Slaa aondoke kwa sababu ni tatizo - ni gumu kuliwekea msingi kwa sababu itabidi uangalie namba na kulinganisha namba uweze kusema kuwa Dr. Slaa ni tatizo.

Kama Chadema inataka ife kwa haraka na ikose hata nafasi ya pili 2015 basi ifanye hili unalopendekeza. Ukiniuliza mimi Dr. Slaa anahitaji kuwa mwenyekiti kabisa wa Chadema tena mtendaji. Na I have to admit it kwa sababu nilimuunga mkono na ninaamini kabisa kuwa Tanzania inahitaji mtu kama yeye kulipeleka taifa kunakotakiwa.
Hata mimi nashangaa amefanyaje hii risk assessment, umtoe mtu aliyekipa chama umaarufu kutoka kura laki 5 hadi mil. 2 na nusu kutoka wabunge watano hadi 50, kutoka Halmashauri 1 hadi kumi, nafikiri hiyo degree ya waberoya ya ufundi chundo haikumstaarabisha.
I know waberoya is not that he doesn't understand the power of Dr.Slaa he knows very well, but he is a person who doesn't appreciate in another words he is a selfish kind of person, he is been driven by internal force of grievances towards others and he always think he is clever than others, but one day he will come to realise that he was wrong.
 
Hata Tambwe Hiza alikuwa na wazo kama la Weborya. What does that mean? Je hiyo inamaanisha Tambwe ana busara kama za Weborya or the percentage of Weborya's MCHEMKO is the same as of Tambwe's?
Just asking, no offense intended
 
Sasa wakimuondoa Dr. Slaa halafu waislamu wakakubali na Wakristu wakianza kukimbia wamuondoe huyo mtu mwingine ili wakubalike na "wakristu". Yaani, hatuna kanuni tena isipokuwa kufanya mambo kwa kujaribu kuridhishana tu?

Kuita majibu ya watu wengine wasiokubaliana nwewe kuwa ni "ujinga" ni kujaribu kulazimisha hoja pale ambao umeshindwa kusimamia hoja yako.

hahaha!

basi mzee mwanakijiji; inatosha!

mtu mzima havuliwi nguo hadharani! please, please Mwanakijiji Pleeeeeeeeeeeease!!!
 
tatizo la CHADEMA wengi hawana uwezo wa kufikiri kwa kina wengi ni WAUZA DUKA ukijua kujumlisha na kutoa basi inatosha.
kujivua gamba ni kuboresha baada ya kuji assess wenyewe. CCM haijivui gamba eti kisa ni SLAA.wakati kwenye uchaguzi CHADEMA Mmeshindwa vibaya. wanacho taka ccm ni ushindi wa kishindo 90% ambazo zimepunguzwa kutokana na UDINI wa CHADEMA na CUF. mwaka 2015 ndiyo kifo rasmi cha CHADEMA maana ccm ikimsimamisha mkristo (KATOLIKI) MAASKOFU WATAKIUNGA MKONO na kukiacha CHADEMA SOLEMBA na waislamu wengi wanakipenda ccm kwasababu ndiyo waliokiasisi

Good for you.Endeleeni kukipenda nacho kitaendela kuwafisadi.

Tatizo la waathirika wa virusi vya udini ni upofu unaowakwaza kufahamu kuwa wahanga wa ufisadi ni sote bila kujali madhehebu yetu.Waliokwapua fedha za EPA,na waliofanikisha ujambazi wa Richmond hawakufanya hivyo kwa minajili ya kupeleka fedha hizo kanisani au msikitini.Sansana zimeishia kwenye nyumba ndogo zao sambamba na kuongeza idadi ya mahekalu yao na magari yao ya kifahari.

Kutumiwa bila kujua unatumiwa ni tatizo,lakini kutumiwa wakati unajua bayana kuwa unatumiwa ni upumbavu
 
At least now mnaondoka kwenye thread za CCM! wanafiki wakubwa

Toka majuzi CDM woote ndio mnaamua mnataka CCM wafanye nini! kamasi unafiki ni nini??

tujadili ya kwetu sasa!! haya endeleeni!

CDM kimeishakufa kwa tuhuma za sasa! kubalini kataeni!
Angalieni hoja za wana CDM-JF mpaka wanatia huruma, kichefuchefu tupu nwaonea huruma sijaona hoja , waislamu hawawatki BADALA YA KUWAAMBIA VIONGOZI WENU WAPIGANE NA HIYO HALI, MNABAKI KUTUMATUMA VIPOST VYA KISHABIKI..UJINGA HUO
Nafikiri waberoya jaribu kupunguza jaziba wakati unapotaka kuandika habari za Chadema mara nyingi huwa naona akili yako ina cease kufikiri na mara nyingi huwa imefunikwa na wingu la udini. Unavyoonekana wewe ni pro CCM sawa lakini ili kutunza heshima yako jaribu uwe unakuja na criticism za weledi si za kujificha kwenye gamba la udini.

Turudi kwenye mada mbali na maneno yako ya kubeza posts za watu(hapo juu), unaposema Chadema kimeshakufa kwa tuhuma za sasa ni zipi hizo, kama ni tuhuma wewe umezipa uzito gani tuhuma za uongo au za ukweli kama zipo na unaposema waislam hawawataki ni wepi hao ulioongea nao au nayo bado ni tuhuma.

Ukijenga hoja kuwa Slaa kashindwa uongozi kwa sababu badala ya kura kuongezeka zimepungua tutakuelewa lakini ukisema kwa sababu waislam hawamtaki hautakuwa na hoja. Kwa sababu CDM si chama cha waislam na hakikuanzishwa msikitini kwamba bila kuwa na shehe ndani kitakufa. Ni ushauri wangu tu kama wewe ni mwislam na unaona CDM hakuna waislam kwa nini usumbuke chagua chama chenye waislam wengi ujiunge nacho, hata kama unasema unatoa ushauri kwa nini ulazimishe ushauri kama wenyewe hawautaki au wewe ni consultant wa CDM. Kama ukiona CDM hawataki ushauri try CUF au CCM uwape ushauri vinginevyo utaonekana msumbufu kuliko kuwa mshauri, ni hayo tu.
 
Sasa wakimuondoa Dr. Slaa halafu waislamu wakakubali na Wakristu wakianza kukimbia wamuondoe huyo mtu mwingine ili wakubalike na "wakristu". Yaani, hatuna kanuni tena isipokuwa kufanya mambo kwa kujaribu kuridhishana tu?
You are real Great Thinker hii quotation inajitosheleza yenyewe kama ni mwenye kuelewa ataelewa.
 
tatizo la CHADEMA wengi hawana uwezo wa kufikiri kwa kina wengi ni WAUZA DUKA ukijua kujumlisha na kutoa basi inatosha.
kujivua gamba ni kuboresha baada ya kuji assess wenyewe. CCM haijivui gamba eti kisa ni SLAA.wakati kwenye uchaguzi CHADEMA Mmeshindwa vibaya. wanacho taka ccm ni ushindi wa kishindo 90% ambazo zimepunguzwa kutokana na UDINI wa CHADEMA na CUF. mwaka 2015 ndiyo kifo rasmi cha CHADEMA maana ccm ikimsimamisha mkristo (KATOLIKI) MAASKOFU WATAKIUNGA MKONO na kukiacha CHADEMA SOLEMBA na waislamu wengi wanakipenda ccm kwasababu ndiyo waliokiasisi
Sasa hapo mwenye mawazo ya udini ni nani lakini si haba kuna mtu kakugongea senkis kwa mawazo yako

The Following User Says Thank You to seki6 For This Useful Post:

 
Muasisi wa Udini TZ ni CCM,Imekuwa ikitumia Dini kupakazia chama chochote kinachoonekana kuwa tishio walianza na Nccr-mageuzi,TLP na juzi-juzi CUF hivyo usishangae kuona CDM wanasingiziwa zengwe kama hili yote hayo ni uongo wa CCM
 
Ni mpenda watu, mkweli, ana uchungu na Taifa na katika watu watakaokumbukwa katika kizazi cha sasa Dr. Slaa hatasahaulika. Kikwete anaweza kusahauliwa tena haraka na jina la Slaa likachukua muda. Kwani yuko mioyoni mwa watu wengi.

Lakini katika hulka za binadamu au tabia tulizonazo kuna wakati mtu muhimu huwa tunampinga, tunampiga na hatuoni thamani yake mpaka pale anapokufa! Kuna wakati watu walio na upendo na mawazo mazuri , mawazo na nia zao nzuri zikachukuliwa au kupokelewa tofauti na baadhi ya makundi ya wat.

Chadema walipaswa kujua kuwa kuna position na situation za kisiasa ..ambazo mara nyingi hazina logic zinaweza kuinua chama au kukiua, Ni vile tukaona Salim A. Salim hatakiwi kuwa rais wa Tanzania na Kikwete akawekwa! Tumeona mpenda vidosho Jacob Zuma akipendwa ....bila sababu

Chadema ilifanya kosa kumteua Slaa kuwa mgombea urais, makosa haya kisiasa ni ya kawaida, kwani haujui adui yako anasema nini, japo swala la kupakwa uchafu wa udini kutokana na background ya Slaa lilikuwa wazi na hapa risk management ilitakiwa

Leo hii wote tunajua position na mchango wa Slaa katika taifa bila kujali dini wala kabila..

Lakini kwa bahati mbaya kwa sababu zilezile nilizozisema 'no logic' existence ya Slaa ndani ya chadema inaonekana kukiua chadema zaidi kuliko kukipaisha na hali hii inaendelea na ikitokea makundi ya wale wanaoipinga chadema yakafikia kuwa na umoja, basi mwisho wa chadema ndio utakuwa umefika..historia inaonyesha huwa hivyo

Chadema; wakati CCM inajivua gamba , na nyie ni wakati wa Slaa kuondoka na kukisafisha chama chenye tuhuma za udini na wanaowachukia hawafichi kabisa.Situation is worse and if you will not do something , I am afraid!

Huu ni ushauri tu, kuna technic nyingi zinaweza kufanyika,.....ila zenu hatujaziona bado

Just Imagine maandamo mliyoyatangaza tayari yamegubikwa na udini! tunaposema hivi ni kwa upendo tu.

Najua wengi wanaweza wakatukana kama kawaida yao, wengine tumejifunza kupambana kuwaondoa watu tongotongo na kusimamia ukweli--mapambano ya fikra hayako kuipinga CCM bali na blind followers, ukweli mara nyingi ambao kama ungefanyiwa kazi tusingekuwa hapa tulipo

Mkitaka kusubiri subirini tu, will recall this post one day

I wish you good Luck!

Wabe.

Opinion potofu ndizo hizi na kama kuna mtanzania kama wewe unaona hii ni speech yako ina meat, basi tutafunga siasa Tanzania. Unaona chadema ina udini kwa sababu inaonekana kupedwa na wakristo waliowengi sio? Kuna kosa gani kwa wakristo kufunguka macho kabla ya waislamu? Hii analysis yako ya chadema ni potofu na unaonekana wazi kwamba fikra za kidini ndizo zinazowasumbua nyie. Unajitahidi kuleta hoja ya udini ndani ya chadema bila ushahidi wowote ule, tuonyeshe basi. Watanzania wanakiu ya mabadiliko na hata siku moja wasiwe-victims wa kuitwa wadini kwa sababu ya kukubaliana na chadema. Hata kama kungekuja chama kinaitwa Bismilah au Mecca na wana-policies za kupinga sera za ccm wangepokelewa na kupata support kubwa Tanzania. Please msilete mawazo yenu binafsi na kuunganisha na nia na malengo ya watanzania. Kutokana na maelezo yako unamaanisha CUF wanakataliwa na wananchi kwasababu ni waislamu sio? Sio kwamba wanaonekena hawana sera za maana wala upinzani wa kweli? Vipi UDP na TLP tena? Kwasababu gani wao hawakubaliki Tanzania? Ni vizuri kama unatoa opinions zenye ushahidi na nafikiri ume-cross the line, tupe ushahidi.

Mpe Dr Slaa heshima watanzania wanayompa sio chini ya hapo. Nimekukusikia hapo juu ukisema wananchi watamkumbuka kwa muda mrefu then ukamshambulia kwamba haoni chama chake kina udini. Are you really serious on what you said? Tena naomba ushahidi katika hoja yeyote ile au tamko lolote Dr Slaa amesimama na kuleta prospective ya udini Tanzania, give us examples. Nilichokisikia na watanzania wengi tulipata ushahidi wa uhakika pale tu kikwete alipokwenda kwenye vyombo vya habari hotuba yake ya mwaka na kufungulia ushahidi wake wa udini kwenye vyombo vya serikali. Kikwete anajitahidi kuelekeza defense yake yote kwa uzembe wa kutokuwa kiongozi mzuri term ya kwanza kwenye udini, ilikuwaje hao hao maaskofu walimuunga mkono na wananchi wengi kumpigia kura uchaguzi 2005?. Kikwete is still sort out support from weak people like you na wale wasiosoma au kupata elimu. Kweli kikwete anajitahidi sana na shehe simba kadhibitisha yote haya kwamba wanataka wananchi waamini kikwete hapati support Tanzania kwasababu yeye ni muislamu, thats weak defense. In short here umetudanganya, you might get a lot people to comment here but nothing here. What was your choice for chadema presidential candidate 2010? (maybe you want to say Zitto? Sorry)

Hii article inanikumbusha uchaguzi wa Obama Marekani, ni kweli wananchi walimchagua kwa asilimia kubwa lakini tuwashutumu kwa kumpa kura Obama au Bush alivyoharibu sana na Obama ku-promote Alternatives Policies?​
 

The Law Of Nature States That:


An object (CCM) will remain at rest or in uniform motion in a straight line unless acted upon by an external force (Dr Slaa)
 
arrogance isiyokuwa na msingi!!!!

Dr Slaa has done by far a lot more than anyother opposn politician, he had the choice of refusing to run for presidency as he was assured of his seat @ Karatu, but due to his selfless nature he did run...and what a good run he gave JK!!!

No one should forget that its by huge sacrifices that u emerge victorius...

Waberoya..why should he be removed by your shallow agenda ? Jenga hoja, CDM sio fuata upepo, just bcoz CCM inajivua gamba nayo ijivue...pls bring sth better
 
Kutumia dini kumkosoa mtu au chama bila kuweka wazi mezani hoja yenye vielelezo ni ubinafsi na ishara ya mtu mwenye mawazo hayo kuishiwa mtu hoja ya kuendeleza tamaa yake na ni mtu hatari wa kupuuzwa na mtu mwenye akili (tukitarajia kwamba wengi tuna akili na wanyonge wa aina hiyo ni wachache katika jamii). Hizi empty statements, allegations and accusations ni za upotofu na mara nyingi za uwongo wa kuchafua amani lakini kama zina ukweli basi anayezitoa aidha ni muoga au siye anayejua ukweli huo hivyo yamtaka kwanza achunguze badala ya kuropoka au asubiri wanaojua ukweli waseme. Mwenye hoja hasa aeleze PROBLEM, ANALYSIS (POSTMORTEM), POSSIBLE CAUSES, CONCLUSION AND SOLUTIONS. Tukienda hivi tutaelewana haraka (kati ya watu wenye nia njema na nchi hii) na hata upenyo wa adui wako kukushambulia ni mdogo. ANAYEKUJA NA SIASA ZA KUPAKANA MATOPE HUWA ZINA-ASSUME WATU NI WAJINGA NA NI YEYE TU MWENYE AKILI. ACHA WEE!
 
At least now mnaondoka kwenye thread za CCM! wanafiki wakubwa

Toka majuzi CDM woote ndio mnaamua mnataka CCM wafanye nini! kamasi unafiki ni nini??

tujadili ya kwetu sasa!! haya endeleeni!

CDM kimeishakufa kwa tuhuma za sasa! kubalini kataeni!

Tuko kitaifa zaidi
 
Miaka ya 1990's DP ya Mtikila, 1995+ NCCR ya Mrema, 2005+ Chadema. Kipindi chote hiki CCM wameendelea kuongoza. Kupendwa kwa ushabiki tusijidanganye. Kama kuna uchafu fatiki ya usafi ifanyike. Tusiwe wabishi Chadema ikitajwa na kushangilia CUF, CCM au NCCR vikipondwa.



je chama gani kinachopendwa zaidi kwa sasa tz? Na kwanini wabe? Cdm inakuwa au inashuka kulinganisha na ilipotoka? Fafanua jibu lako wabe!
 
Jamani wana jamvi na dhani huo ni mtazamo wake na uwezo wake wa kufikiri umefikia hapo. Hivi ni nani na yuko katika tanzania hii ambaye ajui jinsi Dr. Slaa alivyoifikisha hapa CDM, na CCM mpaka inajivua GAMBA ni kwaajili ya kupelekwa pelekwa na CDM kweli. nani ajui jamani WEBU fikiri kwanza sisi atuna muda huo ila nyie mnakazi mwaka huu.
 
Chadema; wakati CCM inajivua gamba , na nyie ni wakati wa Slaa kuondoka na kukisafisha chama chenye tuhuma za udini na wanaowachukia hawafichi kabisa.Situation is worse and if you will not do something , I am afraid!

Wabe.
Ukitaka kumbagua mtu hutakosa kigezo.Hata kipato kinaweza kutumika.
Pale SUA morogoro mtaa wa kididimo wanakoishi wahadhiri ni msafi magari machache so watoto hupenda kucheza mpira na whatever barabarani na maeneo ya wazi.Hii huvutia watoto wa mitaa masikini kuja kucheza katika eneo hili kila wiki lazima watoto wa wahadhiri na wale wa mtaa jirani wapigane tena kwa mawe fimbo yaani fujo usiipimie kabisa.
Wale watoto wanachukiana kuliko mwarabu na mmarekani.Majina kama watoto wa mama na watoto koko utayasikia sana hapa moro
 
Waberoya,
Umeandika ukiwa na 'pre-judice' na kuhukumu uamuzi wa CDM kumteua Dr Slaa kugombea Urais. Ukahukumu aondoke, na waislam hawaitaki CDM.Hakuna mahali ulipotuonyesha kwa hoja za mashiko ni vipi Dr Slaa anakiua chama.Ningelikuwa katika nafasi yako ningeuliza au kuchangia ni vipi CDM kijiimarishe kwa zaidi ili kuepuka yale tunayoyaona leo.

Dr Slaa anajulikana kwa kabila, dini na kijiji alichotoka.Alipokuwa CCM alizushiwa kuwa ni hila za CCM kuingiza 'udini' bungeni. Akahamia CDM na kuendelea na kile alichoamini ni sahihi kwa watanzania. Dr amekuwa chachu kubwa sana hata wabunge kukiri ya kuwa kutokuwepo kutakuwa ni pengo bungeni.

Slaa hakutaka kugombea urais, na wala hakuonekana kuwa tishio lakini kadri siku zilivyosonga mbele alikubalika sana miongoni mwa wananchi. CCM wakatumbukiza hoja ya 'ndoa' , ikashindwa. Fisadi mmoja kwa hofu akatumia magazeti yake kuingiza udini kuwa Dr ametumwa na kundi fulani la jamii.

Ndipo hoja ya baadhi ya watu kutuhumu chadema ilipozuka. Miaka ya Mzee Mtei na Bob Makani au Slaa akiwa mbunge hayakuonekana haya yote. Maandamano yanayoungwa mkono na wananchi wengi yakadhihirish uongo, ndipo kikundi cha watu kikapewa jukumu la kusambaza mbegu za udini. Ukiuliza kikundi hiki ni wapi udini wa CDM ulipo, hakuna mwenye jibu ila utasikia magazeti yameaandika(ndiyo watu wa nchi yetu walivyo). Ukiuliza kikundi hiki je CUF kilikuwa cha waislam?, jibu ni hapana, na je kwanini CDM iwe cha kidini, utaitwa si 'muumini safi'.

CDM imejengwa kwa misingi mizuri tukizingatia historia ya kuchagua viongozi na kumaliza migogoro na linapozuka jambo wazee waasisi husimamia kile kilicho sahihi. CDM inatakiwa kuboreshwa kwa fikra na si kuiga kuvua gamba.

Hitimisho: CDM kisimamie kanuni na misingi ya chama, kuepuka makundi na kiwe chama na si mtu au watu, kisione haya kuwaadhibu wote wanaoleta fujo kwa nia ya uroho wa madaraka na si ufanisi.
CDM ielewe kuwa siasa ni mchezo mchafu, hata huko marekani bado Obama anatuhumiwa si raia.
Jambo la muhimu ni kusimama katika misingi imara bila kumuudhi au kumfurahisha mtu au watu na ukweli waachiwe wananchi.

Wimbi la kupinga chama kwa misingi ya uchochezi tumewahi kuliona kwa CCM na CUF,na CDM isichukuliwe na upepo unaovuma tu, hao wanaodai udini historia inaonyesha waliwahi kukituhum CCM na CUF na leo hatujui kuwa wapo CCM au CUF. Ni makosa kufuata matakwa ya watu wachache wanaotumika na kusahau mamilioni yanayounga mkono. CDM isimamie kile inachokiamini ni kwa masilahi ya Watanzania.
Ushahidi wa kuwa ni watu wachache, juzi profesa Safari amejiunga, sasa kwanini watu wachache waitwe waislam wote?

Hakuna sababu ya Dr kuondolewe bila ushahidi wa takwimu au hoja. Chama hakijengwi kwa dhana au hisia bali 'facts'. Mchango wa Dr bado unahitajika sana na kuwa yeye na wenzake wamekuwa chachu kubwa sana ya mageuzi nchini.
Ukimuondoa Slaa ili Hassan au Mohamed awe kiongozi, utasikia hao si waislam safi au hao ni Bakwata! je utaondoa uongozi tena!!! Na kwanini chama kijengwe kwa misingi ya dini? na kwanini chama kiendeshwe na kundi nje ya chama na si miiko na maadili yake?

Wabunge na viongozi wa CDM waepuke malumbano yasiyo na tija, wasimame na kuwa kitu kimoja wakijenga hoja zenye mashiko kwa jamii.
Halmashauri ziongoze kwa mifano ya mipango na uadilifu, wabunge waongoze kwa uimara, uadilifu na uwajibikaji.
CDM ipenyeze sehemu zote ili kuleta uwiano wa wanachama, kijatanue pwani na kusini kwa kujenga hoja mbele ya wananchi bila woga.

Na wanachama ambao wengi ni wanaJF mnawajibu wa kuepuka kukuza hisia hizi, badala yake msaidie kuinua taswira ya chama. Nimewahi kuonya(ushahidi wa post- JF) kuwa uchochezi wa kuandika thread za kidini ulibeba sura ya kukichafua CDM pindi wachochezi watakapounda hoja.
Jukumu la kutengeneza chama ni la wanachama na haliangalii mtu mmoja kama Wabe anavyotuamisha. Je CDM watafute kiongozi asiye na dini au mwenye dini fulani! na kuondoka kwa Dr kutaondoaje hisia za wanaokituhumu.
 
Back
Top Bottom