Ripoti ya Richmond kutojadiliwa

mjadala wa Richmond baada ya kushindwa kujadiliwa ktk kikao hichi cha Bunge kuna uwezekano mkubwa kujadiliwa 2011 baada tu serekali mpya kuapishwa na bunge jipya ,Bunge ambalo litakuwa hawamo akina
Anna Malechela
SS
Mwakyembe
seleli
Mpendazoe
hii itaufanya mdala huu kuwa rahisi kumalizika na kufungwa.
kwani kwa mujibu wa naibu wa Bunge alisema kwamba kwa sasa mjadala huu hawezi kujadiliwa kwani umeigawa wabunge makundi 2 ambalo ni hatari kwa taifa letu.

Imekuwa kama wimbo wa "Masantula Ngoma ya Mpwita" Kutwanga maji kwenye kinu
 
Tumeshachoka na hiyo Richmond, jana TBC naibu katibu wa bunge alisema haitajadiliwa kwakuwa mjadala wa Richmond hauna tija kwa watanzania akasisitiza vikao vya bunge vitamalizika jumamosi, vipi tena Shelukindo anasema litajadiliwa? nani zaidi hapo.

Hapa nimeamini mafisadi wana nguvu za ajabu na impliedly ndiyo hao waloshika dola na wanapanga nchi iongozweje na nini kifanyike kwa wakati gani.

Hii imeonyesha wazi kuwa kelele za wabunge kwa serikali hazina msaada kwa wananchi kwakuwa hakuna kinachotekelezwa. Tunaelekea pabaya,HV SERIKALI NI NANI, NA IPO KWA MASLAHI YA NANI? NISAIDIENI KTK HILI.
 
Shughuli za bunge zinaweza kusimamishwa kwasababu spika yupo msibani? acha hizo Anne yupo, ila sema JK amempigia magoti 6.

wewe ndio sifuri kabisa JK ampigie magoti 6 kwa lipi?mnabore na arguments zenu za kitoto
 
hakuna kitakacho jadiliwa tena ndani ya bunge maana wote ni wabunge wa ccm pamoja na spika ni mafisadi,kwenye ccm hakuna mtu msafi....yote yamejadiliwa kwenye vikao vya mzee mwinyi juzi na jana....sasa wewe kama ni mwananchi wa tanzania chagua moja kunyoa au kusuka.....kupenda chama cha mapinduzi au kupenda cha cuf,chadema,tlp,n.k
 
Katibu wa Bunge na mwenyekiti wa kamati, wote wako sahihi.

Taarifa ya Richmond ITAWASILISHWA kama kawaida, lakini HAITAJADILIWA.

Kama nimeelewa vizuri, kamati ndiyo yenye wajibu wa kuliambia bunge kama imeridhika au haijaridhika na hatua zilizochukuliwa na serikali.
 
wakulu

Nimepata tetesi kuwa repoti ya richmond kutojadiliwa, kwani mh six yupo bize na mambo ya msiba ivo kurudi dodoma wiki ijayo kwa ajili ya kufunga bunge tu...TiaTia maji

Details please
Tumepewa taarifa mambo yote kesho jmosi.tusubiri kwani mr six atarudi leo toka Luangwa kwa ndege ya kukodi moja kwa moja mpaka Dodoma.
 
aisee hata mimi naona hiki chama ni cha mafisadi papa maana mpaka sasa hili la richmond linapigwa danadana, wanasema halina tija eti
 
Jamani naomba kuto hoja, hivi ni kweli kuwa suala la Richmond halina tija kama linavyodaiwa na katibu wa bunge ,jamani si wanalindana hawa, tuchukue hatua jama
 
Kwa nchi nyingine CCM ingeweza kufutika kkatika anga za siasa Tanzania kwa kushindwa vibaya sana kutokana na madudu chungu nzima yaliyojaa ndani ya chama cha mafisadi na Serikali, lakini kwa nchi yetu ambayo ni kichwa cha Mwendawazimu CCM watarudi madarakani tena kwa ushindi mkubwa tu.
Nani anajua chama kilicholeta uhuru wa marekani kilikuwa kinaitwaje?
The First Two-Party System: Federalists v. Republicans, 1789-1801
George Washington became America’s first president in 1789. After his re-election in 1793, a group of Americans began seeking change through electoral politics. Traditional political theory regarded opposition in a republic as illegitimate, but this view would change as time passed. The opposition leaders, Thomas Jefferson and James Madison, felt that the government favoured wealthy commercial interests at the expense of agriculture and that the United States was at the risk of being ruled by a corrupt, aristocratic government. Jefferson, Madison, and their followers in Congress began calling themselves Republicans. Washington retired from office in 1797, and in his Farewell Address, outlined two principles that would guide American policy well into the twentieth century: to maintain commercial but not political ties to other nations and to enter no permanent alliances. (source American History from colony to superpower: www.threemonkeysonline.com)

Kwa kweli chama kilicholeta uhuru hakijulikani ila kilichoshika madaraka kikiwa cha kwanza wenyewe walijiita Federalists. Kwa sababu nilizoziwekea rangi nyekundu, upinzani ulizuka na kujiita Republicans ambao wapo mpaka leo, lakini hao federalists hawapo tena, wamefutika kabisa - hii ndiyo itatokea kwa CCM
 
Source: Gazeti la mwananchi
CHENGA ya mwili ambayo serikali iliipiga Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini katika utoaji wa ripoti ya utekelezaji wa maazimio dhidi ya kashfa ya Richmond, ilihitimishwa jana baada ya suala hilo kuyeyuka, bila ya wabunge kupata nafasi ya kuhoji.

Hali ilikuwa ya utulivu wakati spika wa Bunge, Samuel Sitta akiorodhesha shughuli ambazo zilitakiwa zijadiliwe kwenye mkutano huo wa 17 wa Bunge, ikiwemo suala la ripoti ya utekelezaji wa maazimio hayo dhidi ya kashfa ya Richmond, sakata la mgodi wa Kiwira na kampuni ya Reli (TRL), lakini haikuwezekana kujadiliwa kwa sababu mbalimbali.

“Hili ni Bunge ambalo liko makini na linalotaka kutatua matatizo ya wananchi,“ alisema Spika Sitta na kuongeza kuwa shughuli zote ambazo hazikuweza kujadiliwa, zitashughulikiwa kwenye mkutano ujao.

“Ninasikitika kwamba tumefikia muda wa kuahirisha mkutano huu wakati bado kuna viporo. Liko suala la ripoti ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu Richmond, suala la mgodi wa Kiwira, suala la (Kampuni ya Reli) TRL na Ticts (kampuni inayoendesha kitengo cha makontena Bandari ya Dar es salaam).”

Sitta alisema ilikuwa ni nia yake kwamba suala la utekelezaji wa maazimio 23 ya Bunge kuhusu Richmond lifikie mwisho mkutano huo, lakini jambo hilo limeshindikana.

Baada ya kutoa maneno hayo yaliyoonekana kuwa na nia ya kuwatuliza, Sitta aliwataka wabunge waunge mkono hoja ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda ya kuahirisha mkutano huo, lakini hakukuwepo na sauti kubwa za kuunga mkono hoja hiyo kama ilivyo kawaida kiasi cha Spika Sitta kulazimika kutumia mbinu nyingine.

“Sasa matokeo ya kura hii nitayatoa baada ya wimbo wa taifa,” alisema Sitta na kuruhusu wimbo huo upigwe.

Mara baada ya kumalizika kwa wimbo huo, Spika Sitta alisema kuwa baada ya kuuliza ni wabunge wangapi wameafiki hoja ya kuahirisha mkutano huo wa Bunge, amegundua kuwa waliosema ndio wameshinda na kuahirisha rasmi hadi Januari.

“Tumeshangaa sana maana jana (juzi) serikali ilituahidi kwamba ingeleta ripoti hiyo leo(ya Richmond jana) ili Jumamosi iwasilishwe bungeni, sasa sijajua nini hasa kimetokea,” alidokeza mjumbe mmoja wa kamati ya Bunge ya Nishati na Madini ambaye aliomba jina lake lisitajwe.

Mbunge wa Iramba Mashariki, Mgana Msindai (CCM) alisema: “tuko stranded (tumekwama)... wananchi hawatatuelewa kuhusu kuahirishwa kwa suala la Richmond na kwa kweli linazidi kutuchanganya.”

Mbunge wa Karatu, Dk Willibroad Slaa (Chadema) alisema kitendo serikali ya CCM ni kielelezo kingine cha ubabaishaji akisema suala hilo si miliki ya chama hicho pekee.

“Jambo pekee litakalofanywa na Chadema ni kwenda kwa wananchi kwa sababu ndio mahakama kubwa kuliko zote,” alisema katibu huyo wa Chadema.

Mbunge wa Sumbawanga Mjini, Paul Kimiti alisema alitegemea serikali ingetoa taarifa ya nini kilichotokea kwa sababu hata mpangilio wa ratiba ulikuwa ni wa kubalikabadilika.

Serikali ilishindwa mara mbili kuwasilisha ripoti hiyo kwa Kamati ya Nishati na Madini jijini Dar es salaam kwa kutoa sababu tofauti, ikiwa ni pamoja na kutokuwepo nchini kwa Waziri William Ngeleja na aliporejea nchini waziri huyo aliwaambia waandishi kuwa wamekubaliana suala hilo lipelekwe moja kwa moja Dodoma.

Hata hivyo, suala la kuwasilishwa kwa hoja hiyo likawa kitendawili baada ya mkutano huo wa 17 kuanza baada ya kutojumuishwa kwenye shughuli za Bunge na iliripotiwa baadaye kuwa suala hilo lingerejeshwa kwenye Kamati ya Nishati na Madini.

Juzi mwenyekiti wa kamati hiyo, William Shelukindo aliiambia Mwananchi kuwa ana uhakika suala hilo lingejadiliwa leo lakini katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alikaririwa akisema kuwa Richmond haitajadiliwa tena kwa kuwa mjadala wake ni malumbano ambayo hayana faida kwa nchi.
Miongoni mwa maazimio hayo 23 ni kuwajibishwa kwa mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hoseah.
 
Mhhhhhhhhh.....
Natabiri uspika wa sita mwisho mwaka 2010.
Lets wait and see....
Sio kwamba yuko wrong....
Ni kwamba amezidiwa ubavu na mafisadi.
 
Katika mihimili MINNE (4) ya uongozi Tanzania, MHIMILI WA UFISADI ndio wenye nguvu zaidi. Mhimili wa TANO (5) unakuja muda si mrefu. Wananchi watafagia viongozi wote na wabunge wasiokuwa na Uzalendo wala Tija.
 
sitakaa nishangae hata mwakani wakiaahirisha hii.as far as i know mafisadi wana nguvu sana na wanaweza kupasua hii nchi ndio maana hata Mizengwe Pinda alisema wana nguvu sana hawa..hahaaaaa Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo woteeeeee
 
bunge gani hili ambalo hata spika wake ana yumbishwa

wananchi wa vijijini wakielimika tu mchezo kwisha...hao ndio majority ya wapiga kura, lakini wakihongwa elfu 10 na pea mpya ya kanga baasi wanauza kura,

ku i kick out CCM kwa nguvu zote ndio kuta saidia kuwakumbusha kwamba cheo ni dhamana
 
hii inanikumbusha jamaa walivyo muweka lowasa katikati, karamagi na kulia na msabaha kushoto, sasa hii kweli inathibitisha huyu kweli ni mwana wa mafisadi, maana bado anawatokea mafisadi kwenye ndoto na kila anapopita.
 
Back
Top Bottom