Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Well... Tunashukuru vyanzo vyetu vya "kuaminika" once again.. we set the standard!
On Technicality?
Habari Leo
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuacha siasa kwenye masuala yanayohusu maslahi ya Taifa.
Membe amesisitiza kuwa tuhuma kwamba Tanzania imeshiriki kusambaza silaha haramu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ni za uongo.
Kiongozi huyo ametoa changamoto kwa yeyote anafahamu kwamba Serikali ya Tanzania imeshiriki katika biashara hiyo kuweka hadharani ushahidi wake.
Chadema iache kuleta siasa kwenye maslahi ya taifa. Serikali ya Tanzania haijahusika katika biashara haramu ya silaha Kongo, na madai hayo ni upuuzi, na Chadema ije na uthibitisho badala ya kungangania ripoti ya Umoja wa Mataifa ambayo tumesema ni ya uongo, na inataka kutudhalilisha, amesema Membe.
Membe ametoa kauli hiyo mjini Havana baada ya kuulizwa na gazeti hili msimamo wake siku moja baada ya Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chadema, John Mnyika kuwaeleza waandishi wa habari mjini Dar es Salaam kuwa Membe anapaswa kuomba radhi kwa kile ilichodai kuudanganya umma kuhusu taarifa hiyo ya UN.
Taarifa ya Wataalamu na wachunguzi wa UN imeituhumu Tanzania na baadhi ya nchi, ikidai zinahusika katika usambazaji wa silaha haramu kwa kikundi cha waasi cha FDLR cha Kongo kinachopigana dhidi ya raia wa Rwanda, mashariki mwa nchi hiyo ya Maziwa Makuu.
Membe akionekana dhahiri kukasirishwa na kauli ya Chadema, alisema hakuna mahali popote katika ripoti hiyo ya UN kunakothibitisha ushiriki wa Serikali ya Tanzania katika tuhuma hizo, lakini hilo pia haliondoi ukweli kuwa nchi inapaswa kuombwa radhi kwa kuchafuliwa jina lake katika medani ya kimataifa.
Amesema, hoja kwamba kumeonekana mawasiliano ya simu kati ya Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Francis Mndolwa na baadhi ya viongozi waasi, haina uzito kwa sababu haina uthibitisho kuwa mawasiliano yao yalihusu biashara ya kuuziana silaha haramu.
Hoja kwamba namba ya simu ya Balozi Mndolwa imeonekana ikifanya mawasiliano na waasi haina uzito wowote, kwani hakuna uthibitisho kuwa mawasiliano yao yalikuwa ni kwa ajili ya kuuziana silaha, amesema Membe anayefuatana na Rais Jakaya Kikwete ziarani hapa Cuba na kuongeza:
Watoe uthibitisho wa kuuziana silaha, kwani hata mimi nimekuwa na mawasiliano na watu hao wa upinzani au wanaoitwa waasi, lakini si mawasiliano ya kuuziana silaha, yanaweza kuwa mawasiliano ya kupatanisha migogoro yao. Sasa tuje na uthibitisho, siyo tuhuma zisizo na ukweli.
Alisema waliotoa tuhuma hizo wanapaswa kueleza jinsi Balozi Mndolwa na Watanzania wengine ambao simu zao zimeonekana kwenye ripoti hiyo ya UN, walivyoshiriki katika biashara hiyo haramu, na si kutoa tuhuma ambazo hazina uthibitisho zenye nia ya kuchafua jina zuri la Tanzania kimataifa.
Chadema wasidandie ripoti, watoe uthibitisho wa Tanzania kushiriki katika biashara hiyo. Kuonekana kwa simu za Watanzania siyo uthibitisho, tunataka uthibitisho wa ushiriki wa Serikali ya Tanzania katika tuhuma hizo. Serikali inatoa changamoto kwa ye yote mwenye ushahidi wa ushiriki wake katika biashara hiyo autoe, vinginevyo hizo ni tuhuma zisizo na ukweli, ni upuuzi na tunadai kuombwa radhi, amesema Membe.
Mnyika katika mkutano wake na wanahabari juzi alidai kuwa Membe alikurupuka katika kujibu tuhuma hizo alizodai chama hicho inaamini ni za kweli, kwa kuwa mifano ya vitendo hivyo na baadhi ya majina ya watu wakiwemo viongozi wa nchi yamo katika taarifa kuonesha kuwa walihusika.
Maoni yangu:
a. Kuna kitu hakiko sahihi katika mtiririko wa hoja za Bw. Membe. Kitu ambacho ni matumizi ya lugha ya kiufundi:
b. Sikutaka kurudia somo hili tena lakini CCTI inaandika barua ya wazi kwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na kujaribu kujibu baadhi ya changamoto zake. Inshallah, tutaweka barua hiyo muda si mrefu ujao.
c. Membe na serikali ya Tanzania wasichukulie jambo hili kiutani utani au kimzahamzaha. Kuna ushahidi mkubwa sana wa ushiriki wa maafisa wa Tanzania (aidha kama watu binafsi au vinginevyo) katika usafirishaji wa silaha katika eneo hili. Jambo hili siyo geni kwa wachunguzi wengi. Nendeni taratibu kina Membe... very careful.. mtamfungua sanduku la Pandora bure..
On Technicality?
Habari Leo
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuacha siasa kwenye masuala yanayohusu maslahi ya Taifa.
Membe amesisitiza kuwa tuhuma kwamba Tanzania imeshiriki kusambaza silaha haramu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ni za uongo.
Kiongozi huyo ametoa changamoto kwa yeyote anafahamu kwamba Serikali ya Tanzania imeshiriki katika biashara hiyo kuweka hadharani ushahidi wake.
Chadema iache kuleta siasa kwenye maslahi ya taifa. Serikali ya Tanzania haijahusika katika biashara haramu ya silaha Kongo, na madai hayo ni upuuzi, na Chadema ije na uthibitisho badala ya kungangania ripoti ya Umoja wa Mataifa ambayo tumesema ni ya uongo, na inataka kutudhalilisha, amesema Membe.
Membe ametoa kauli hiyo mjini Havana baada ya kuulizwa na gazeti hili msimamo wake siku moja baada ya Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chadema, John Mnyika kuwaeleza waandishi wa habari mjini Dar es Salaam kuwa Membe anapaswa kuomba radhi kwa kile ilichodai kuudanganya umma kuhusu taarifa hiyo ya UN.
Taarifa ya Wataalamu na wachunguzi wa UN imeituhumu Tanzania na baadhi ya nchi, ikidai zinahusika katika usambazaji wa silaha haramu kwa kikundi cha waasi cha FDLR cha Kongo kinachopigana dhidi ya raia wa Rwanda, mashariki mwa nchi hiyo ya Maziwa Makuu.
Membe akionekana dhahiri kukasirishwa na kauli ya Chadema, alisema hakuna mahali popote katika ripoti hiyo ya UN kunakothibitisha ushiriki wa Serikali ya Tanzania katika tuhuma hizo, lakini hilo pia haliondoi ukweli kuwa nchi inapaswa kuombwa radhi kwa kuchafuliwa jina lake katika medani ya kimataifa.
Amesema, hoja kwamba kumeonekana mawasiliano ya simu kati ya Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Francis Mndolwa na baadhi ya viongozi waasi, haina uzito kwa sababu haina uthibitisho kuwa mawasiliano yao yalihusu biashara ya kuuziana silaha haramu.
Hoja kwamba namba ya simu ya Balozi Mndolwa imeonekana ikifanya mawasiliano na waasi haina uzito wowote, kwani hakuna uthibitisho kuwa mawasiliano yao yalikuwa ni kwa ajili ya kuuziana silaha, amesema Membe anayefuatana na Rais Jakaya Kikwete ziarani hapa Cuba na kuongeza:
Watoe uthibitisho wa kuuziana silaha, kwani hata mimi nimekuwa na mawasiliano na watu hao wa upinzani au wanaoitwa waasi, lakini si mawasiliano ya kuuziana silaha, yanaweza kuwa mawasiliano ya kupatanisha migogoro yao. Sasa tuje na uthibitisho, siyo tuhuma zisizo na ukweli.
Alisema waliotoa tuhuma hizo wanapaswa kueleza jinsi Balozi Mndolwa na Watanzania wengine ambao simu zao zimeonekana kwenye ripoti hiyo ya UN, walivyoshiriki katika biashara hiyo haramu, na si kutoa tuhuma ambazo hazina uthibitisho zenye nia ya kuchafua jina zuri la Tanzania kimataifa.
Chadema wasidandie ripoti, watoe uthibitisho wa Tanzania kushiriki katika biashara hiyo. Kuonekana kwa simu za Watanzania siyo uthibitisho, tunataka uthibitisho wa ushiriki wa Serikali ya Tanzania katika tuhuma hizo. Serikali inatoa changamoto kwa ye yote mwenye ushahidi wa ushiriki wake katika biashara hiyo autoe, vinginevyo hizo ni tuhuma zisizo na ukweli, ni upuuzi na tunadai kuombwa radhi, amesema Membe.
Mnyika katika mkutano wake na wanahabari juzi alidai kuwa Membe alikurupuka katika kujibu tuhuma hizo alizodai chama hicho inaamini ni za kweli, kwa kuwa mifano ya vitendo hivyo na baadhi ya majina ya watu wakiwemo viongozi wa nchi yamo katika taarifa kuonesha kuwa walihusika.
Maoni yangu:
a. Kuna kitu hakiko sahihi katika mtiririko wa hoja za Bw. Membe. Kitu ambacho ni matumizi ya lugha ya kiufundi:
b. Sikutaka kurudia somo hili tena lakini CCTI inaandika barua ya wazi kwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na kujaribu kujibu baadhi ya changamoto zake. Inshallah, tutaweka barua hiyo muda si mrefu ujao.
c. Membe na serikali ya Tanzania wasichukulie jambo hili kiutani utani au kimzahamzaha. Kuna ushahidi mkubwa sana wa ushiriki wa maafisa wa Tanzania (aidha kama watu binafsi au vinginevyo) katika usafirishaji wa silaha katika eneo hili. Jambo hili siyo geni kwa wachunguzi wengi. Nendeni taratibu kina Membe... very careful.. mtamfungua sanduku la Pandora bure..