Ripoti ya BOT mbona haitolewi!? Walioiandika wanawekewa shinikizo ili waibadilishe?

Posted Date::12/19/2007
Chadema wadai ripoti ya ukaguzi BoT

*Wahoji serikali inasubiri nini?

Muhibu Said na Mwanaid Omary

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka serikali kuiweka hadharani ripoti ya ukaguzi wa Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambayo tayari mkaguzi ameiwasilisha serikalini.

Tamko hilo lilitolewa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe wakati akifungua Mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho, katika Hoteli ya Land Mark, jijini Dar es Salaam jana.

Alisema wamefikia uamuzi huo kwa kuwa muda uliotolewa kwa Kampuni ya Ernest and Young kuchunguza tuhuma hizo, kumalizika, huku ripoti ya uchunguzi huo ikiwa imekumbatiwa serikalini.

"Hivyo, tunamtaka Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Waziri wa Fedha, Zakhia Meghji watupe ripoti hiyo," alisema Mbowe.

Alisema ameshangazwa kusikia ripoti hiyo kwamba imepelekwa kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa ajili ya kupitiwa, kitendo alichodai kuwa, kinatia shaka huenda kuna njama za makusudi zinazofanywa na serikali ili kutaka kuificha.

"CAG anaipitia nini? Au wanataka kuificha? Fedha zetu tumeibiwa, tumewatangazia, sasa tunataka ripoti iwekwe hadharani," alisema Mbowe.

Alisema pamoja na kuwataja hadharani watuhumiwa wa ufisadi, hadi sasa serikali imeshindwa kuchukua hatua dhidi yao na pia dhidi ya wale walioibua tuhuma hizo kuthibitisha kama waliyoyadai ni ya uongo.

Alihoji safari za mara kwa mara za Rais Kikwete nchini Marekani akiitaka serikali kueleza kilichoko nchini humo, zinawanufaisha nini wananchi na sababu za safari hizo kutogharamiwa na serikali.

Pia aliitaka serikali kueleza sababu za mkutano wa Sullivan unaotarajiwa kuwashirikisha wafanyabiashara Wamarekani weusi zaidi ya 1,000, kufanyika nchini.

Mkutano huo unatarajiwa kufanyika mkoani Arusha Juni 2-6, mwakani.

Pia aliitaka serikali kueleza tuzo alizopewa Rais Kikwete katika ziara yake ya hivi karibuni nchini Marekani, kwamba zinasaidia vipi maisha ya Mtanzania wa kawaida.

Katika ziara yake aliyoifanya Marekani Desemba 12-14, mwaka huu, Rais Kikwete alitunukiwa tuzo kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo na kwa kuhutubia kweye mkutano wa nchi hiyo.

Pia Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Dk Asha-Rose Migiro alitunukiwa tuzo kwa mchango wake wa kuleta amani katika nchi za Maziwa Makuu.

"Mwekezaji akikusifu, ujue kuwa wewe ni ndondocha. Wawekezaji wananeemeka kupitia kwa Kikwete, sisi tunateseka," alisema Mbowe.

Kutokana na hali hiyo, Mbowe alisema wasiwasi juu ya mkutano wa Sullivan mjini Arusha, unakuja kutokana na mwanzilishi wake (Sullivan) kuwamo miongoni mwa washauri wakubwa wa Kampuni ya madini ya Barrick inayomiliki migodi kadhaa hapa nchini.

Alidai wasiwasi huo unatiwa nguvu kutokana na safari za Rais Kikwete Marekani, kugharamiwa na wawekezaji waliompa tuzo hizo.

"Huyu Sullivan ndiye aliyesababisha mgogoro wa mafuta Nigeria. Kama Tanzania kutagundulika kuna mafuta chini ya utawala wa CCM, basi tumekwenda na maji, Rais anaingizwa kwenye kiini macho," alisema Mbowe.

Naye Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amemjibu Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, kuhusu tuhuma za ubaguzi na upendeleo alizozielekeza kwa chama hicho na kusema kwamba, hajui analolisema.

Dk Slaa alitoa kauli hiyo alipozungumza na Mwananchi katika mahojiano maalum, jijini Dar es Salaam jana.

Alisema Wangwe ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, hawezi kuthibitisha tuhuma hizo na kwamba, ana wasiwasi huenda matamshi aliyoyatoa yana lengo la kupandikiza jambo katika chama na kuupotosha umma.

"Anayetoa tuhuma hizo hajasoma na hajui analosema. Matamshi yake yanapandikizwa kimalengo. Kama ana ushahidi wa hayo anayoyasema autoe na siyo maneno matupu," alisema Dk Slaa.

Dk alisema madai ya Wangwe kwamba fedha za ruzuku zinaishia makao makuu ya chama, hayana ukweli, badala yake fedha hizo zimekuwa zikipelekwa pia mikoani.

Alisema katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, chama kilisambaza Sh 60 milioni katika mikoa yote nchini, isipokuwa Lindi na Mtwara, kwa ajili ya kugharamia ziara zilizofanywa na viongozi katika mikoa hiyo.

Pia alisema zaidi ya Sh 200 milioni zilisambazwa katika mikoa yote nchini kugharamia manunuzi ya vifaa mbalimbali vya chama, kama vile bendera na kadi, kitu ambacho hakuna chama chochote kilichoweza kufanya hivyo.

Kuhusu madai ya ubaguzi na upendeleo wenye misingi ya kidini na kikanda, Dk Slaa alisema hayana ukweli wowote na kwamba, kinachozingatiwa na chama katika uteuzi wa viongozi, hasa wabunge wa viti maalumu, ni uwezo na sifa na si sura wala vigezo vilivyotajwa na Wangwe.

"Chadema ni chama pekee cha kitaifa, hakifanyi ubaguzi, hakuna masuala ya kifamilia kama anao ushahidi wa watu hao na autoe. Nina uhakika hata mkimfuata (Wangwe) sasa hivi atoe huo ushahidi, hana," alisema Dk Slaa.

Wangwe alitoa tuhuma hizo kupitia vipeperushi vilivyosambazwa nchi nzima na wafuasi wa chama hicho wanaomuunga mkono vikiwatuhumu baadhi ya viongozi wa Chadema kuendesha chama kwa upendeleo, hasa katika mgao wa ruzuku na ubaguzi wa misingi ya kidini na kikanda.

Akizungumza na mwandishi wa Mwananchi muda mfupi kabla ya kuingia kwenye kikao cha Kamati Kuu juzi, Wangwe alisema kutokana na kasoro hizo, atahakikisha analeta mabadiliko ya kweli ndani ya chama ili kukiepusha kuendeshwa kama Shirika lisilo la kiserikali (NGO).

Alisema jambo kubwa linalokitia dosari chama ni ofisi za wilaya na kata kutokuwa na mawasiliano na makao makuu, hasa katika mgao wa ruzuku na uteuzi wa wabunge wa viti maalum.

Wangwe alidai mgao wa ruzuku pamoja na uteuzi wa wabunge wa viti maalum, vimekuwa vikitolewa na uongozi wa Chadema kwa kuangalia upande mmoja wa wanachama wanaotoka katika Kanda ya Kaskazini nchini.

"Chama kimekuwa mali ya koo na familia fulani. Tunataka kiwe cha wanachama," alisema Wangwe ambaye anawania nafasi hiyo na Mbunge wa Mpanda Kati (Chadema), Said Arfi.

Wakati Wangwe akisema hayo, wafuasi wa chama hicho wanaomuunga mbunge huyo (Wangwe) katika kinyang'anyiro hicho, jana walisambaza vipeperushi vinavyotuhumu kuwapo na upendeleo katika mgao wa ruzuku za chama na ubaguzi wa kidini na kikanda katika chama hicho.

Vipeperushi hivyo vilivyotawanywa Makao Makuu ya Chadema, mikoani na katika eneo ambalo Kamati Kuu ilikutana jana, vinadai kwamba chama hicho kimekuwa kikipata ruzuku ya Sh 60 milioni kila mwezi, lakini fedha hizo zimekuwa zikiishia makao makuu matumizi yake hayawekwi bayana.

"Tunasema inawezekana kila mkoa ukapata Sh 1.5 milioni kila mwezi na Makao Makuu itabaki na zaidi ya Sh10 milioni ambazo zinawatosha kwa shughuli za chama," ilieleza sehemu ya kipeperushi hicho.

Kipeperushi hicho ambacho Mwananchi inayo nakala yake, pia kimedai kuwapo kwa "ubinafsi" katika chama ambao umesababisha karibu wabunge wote wa viti maalum kuteuliwa kutoka katika mkoa mmoja ulioko eneo la Kaskazini mwa nchi.

"Wabunge viti maalum karibu wote wanatoka upande mmoja na kutoa ruzuku ya chama kwa upande mmoja (Kaskazini) haya yote yanatukera," kilieleza kipeperushi hicho na kuwataka wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho kumchagua Wangwe ili kukinusuru chama na mambo hayo.

Wabunge hao ambao wote wanatoka katika Mkoa wa Kilimanjaro, ni Halima Mdee na Grace Kihwelu, Maulida Komu na Lucy Owenya.

Katika kipindi cha mwezi mmoja, Wangwe amekuwa akiibua hoja ambazo zimezua mjadala mkubwa ndani ya chama hicho. Hoja ya hivi karibuni ni ile aliyodai kuwa Zitto hakupaswa kuingia katika Kamati ya kupitia upya mikataba ya madini.
 
Kuna dalili ya JK kudhalilila nini ? Kama watachelewa basi itavujishwa na tutaitoa hapa muda si murefu . We are working on it .

Hicho ndo kilichobakia.. hata hivo nadhani kuipata original bado ni muhimu kwani lazima kucheleweshwa huku si bure!! tutaletewa kanyaboya.. wanayopenda tuisikie.
 
mwanakijiji hebu tutafutie ile waliyopewa wabunge mtuwekee humu ndani tuanze kuifanyia kazi najua Jf wanaweza tulipata buzwagi sembuse huu upuuzi tu.
leteni mambo wazee!
 
Hivi hamjaunganisha mbili na mbili..? kwani kikao cha Rais na waandishi leo kinahusu nini?

hapo ndipo naanza kumpenda lydia Ngosha,MWanakijji tabia yako ya kukaa na watu wa usalama unatupa sana taabu..

haya tutegemee nini jioni?
 
Waungwana hivi kuna anayefahamu wakaguzi wa Ernst & Young walikagua transactions za kuanzia lini mpaka lini? Nina wasi wasi waliangalia kipindi kifupi na labda kama wangeangalia kipindi kirefu kwa mfano transactions za tangu 2000 mpaka 2007 september basi wizi ambao ungegundulika ungekuwa ni mkubwa zaidi labda hata shilingi bilioni 500.
 
Walianaglia 2005/2006, in audit we just take a universe is only a sample reviewed. utachanganyikiwa my friend kukagua vitu vyote.
 
Walianaglia 2005/2006, in audit we just take a universe is only a sample reviewed. utachanganyikiwa my friend kukagua vitu vyote.

Kama waliangalia mwaka mmoja na wizi ni mkubwa kiasi hicho basi imagine kama wangeangalia miaka mingine miwili au mitatu. Nina imani kwamba wizi huu haukuanza 2005, umeanza miaka mingi tu. Wakaguzi wanapogundua makosa mengi katika sample yao basi hutakiwa kuongeza sample hiyo ili kujua ukubwa wa tatizo. Siri kali labda hawakutaka waendelee miaka miwili nyuma 2003/2004 na 2004/2005 kwa kuwa madudu yaliyofanyika hapo BOT yangeongezeka kwa kiasi kikubwa sana.
 
Kama waliangalia mwaka mmoja na wizi ni mkubwa kiasi hicho basi imagine kama wangeangalia miaka mingine miwili au mitatu. Nina imani kwamba wizi huu haukuanza 2005, umeanza miaka mingi tu. Wakaguzi wanapogundua makosa mengi katika sample yao basi hutakiwa kuongeza sample hiyo ili kujua ukubwa wa tatizo. Siri kali labda hawakutaka waendelee miaka miwili nyuma 2003/2004 na 2004/2005 kwa kuwa madudu yaliyofanyika hapo BOT yangeongezeka kwa kiasi kikubwa sana.

Nakubaliana na wewe mkuu, inabidi kupitia upya kipindi chote cha Ballali.

Huko nyuma si ajabu kuna madudu hata mabaya zaidi ya hayo ya mwaka 2005.
 
Hivi kuna Mtu anaweza kutuwekea Rights and Duties za Auditor, Na Auditor anapo kumbana na Mgt Fraud inakuwaje? Ambayo Mgt hawakubalini nae?
Pili Appoint ya Auditor na wajibu wa Appointed Auditor kujua sababu ya Previous Auditor kutoka, na wajibu wake wa kuongea na Previous auditor, ili kujua sababu za wao kutoendelea na Kazi hiyo na kama kuna sababu za Kikazi or Professional ilikwamisha wao kutoendelea na Kazi.
Maana tunaambiwa wale wa Delloite & Touche from SA wal;ikuwa na Mis-understanding na Mgt kwenye huo Wizi( Though Taarifa ya Serekali inasema kwa Walitofautiana kwa sababu zao, kama vile ni za ki-binafsi kuliko za Kikazi)
 
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,

Heri ya mwaka mpya! Pole pia kwa msiba wa Jenerali Marwa!

Kwa mara nyingine tena nakuandikia hii email ambayo kama kawaida yangu nitaiweka katika jamvi tukufu la Jamboforums kukukumbusha tu kuwa unatakiwa kuiweka hadharani report ya ukaguzi wa fedha za Benki kuu ya Tanzania iliyofanywa na kampuni ya Ernst & Young.

Wote tunajua kuwa mamilioni ya pesa yametumika kuwalipa hao Ernst & Young na mchovu wao Massawe ili kufanya huu ukaguzi. Wote tunakubaliana kuwa hayo mamilioni ni yetu sisi watanzania tunaolipa kodi za aina karibu kumi ili kuendesha serikali yako. Wote tunajua kuwa uliahidi kuiweka wazi hii report na kuwataja wote waliohusika na wizi huu mkubwa kabisa kutokea.

Inashangaza kuwa umeamua kutoa sehemu tu ya report hii hata baada ya kukaa nayo kwa zaidi ya mwezi mzima. Inasikitisha kuwa umetaja majina ya makampuni hewa bila kutaja majina ya wanao(lio)miliki makampuni haya. Inasikitisha kuwa umetangaza kumfuta kazi Balali wakati ukijua kabisa kuwa alishakuandikia barua ya kuacha kazi. Inasikitisha kuwa unataka kumtwisha Balali huu mzigo yeye peke yake huku ukijua kuwa wewe na wengi katika serikali yako mnahusika kwa njia moja au nyingine katika wizi huu.

Mheshimwa rais, nakukumbusha kuwa wewe ni mwajiriwa tu na sisi watanzania ndio tumekuajiri kufanya kazi ya kutuongoza. Hii habari kuwa umeiagiza bodi ya benki kuu kufanya uchunguzi wa kile kilitokea benki kuu wakati tayari kuna makampuni mawili ya kigeni yamelipwa mabilioni kufanya uchunguzi huu ni matusi makubwa sana kwa watanzania.

Nimechoka kukuita mheshimwa kwa sababu unatuonyesha watanzania dharau kubwa sana kwa kile unachofanya. Kwanza uchunguzi ulifanywa na Deloitte, kisha CAG ikaingilia, kisha E&Y, na sasa unataka bodi ichunguze? ichunguze nini na kwa gharama gani? ni pesa ya nani italipa hizo gharama za vikao vya uchunguzi? na kwa madhumuni gani bodi itachunguza kile ambacho wanabodi wengi sana wamehusika?

Wewe Kikwete, sasa unazidi kuwadharau na kuwatusi watanzania. Ni lazima uweke report ya ukaguzi hadharani ili isomwe na watanzania wote. Kuna taarifa kuwa report imebadilishwa na kwa vile unajua kuwa huu mtandao tukufu wa JF unareport ya awali, basi umeamua kutotoa report maana utabainika jinsi mambo fulani unayotakiwa kufanya ulivyoyaacha au kuyafuta.

Kisingizio cha kudai kuwa umemfuta kazi Balali ni cha dharau kwa watanzania. Kwanza kabisa ungeanza na mkoloni, mwizi mkuu na rafiki yako wa karibu Rostam Azizi ambaye mlishirikiana naye kuchukua pesa hapo benki kuu kwa ajili ya kampeni yako ya uraisi kwa mwaka 2005. Tubu makosa na uombe msamaha kwa watanzania na kisha uanze kushughulikia wote waliohusika na wizi huu. Kikwete muogope Mungu maana hata ukipanda juu kiasi gani kuna siku utashuka chini na inatia huruma nikifikiria jinsi kizazi kijacho cha watanzania kitakuadhibu vibaya kwa unayofanya leo.

Anza kwanza na kuweka wazi report ya ukaguzi wa BOT, hili tu ndilo naomba kwa sasa!

Asante
 
welcome back mwafrika wa kike..........

Yes!! ripoti iwekwe wazi watu tuichambue
 
mama wee.. she is baaack! honey I missed you.. lete vitu maana nilikuwa nakusubiri urudi toka safari ili unipe "nyeti za huko". Haya na miye nakuunga mkono na miguu, hii ripoti iwekwe hadharani tu ili yaishe na wananchi waamue wenyewe. Sasa akisema ni kwa ajili ya usalama wa Taifa ndio maana haitoi itakuwaje?
 
Mee too! Welcome back my sister. And I like the style you walked back in.
 
welcome back mwafrika wa kike..........

Yes!! ripoti iwekwe wazi watu tuichambue

Asante Ogah...

Hii report ni muhimu sana maana watu watajua nini kimefanyika na nini hakijafanyika. Kuna watu wanadhani kuwa ukaguzi wa BOT ni wa miaka yote ambayo kumekuwa na utata wa wizi na ubadhirifu kumbe Kikwete na wasanii wenzake wameamua kuongelea EPA tu na kuacha vingine vyote.

Hii report iwekwe wazi ili tujue pa kuanzia.
 
mama wee.. she is baaack! honey I missed you.. lete vitu maana nilikuwa nakusubiri urudi toka safari ili unipe "nyeti za huko". Haya na miye nakuunga mkono na miguu, hii ripoti iwekwe hadharani tu ili yaishe na wananchi waamue wenyewe. Sasa akisema ni kwa ajili ya usalama wa Taifa ndio maana haitoi itakuwaje?

yaani wewe subiri tu,

JF iko loaded na kuna mambo yatamwagwa hapa hadi Kikwete na wenzake wakimbie. Huu ni mwaka wa mapambano. Wakienda Bagamoyo sisi tutaenda Pemba, wakienda Tanga sisi tutaenda Kisumu. Nimechoshwa na wizi na udanganyifu wa kisanii unaondelea hapa.

Kikwete get ready for the fight, we want our country back na ni bora uwe upande wetu maana Mungu yuko nasi.
 
Mee too! Welcome back my sister. And I like the style you walked back in.

Jasusi,

get your dancing shoes ready!

Watu walidhani 2007 ni mwaka wa shetani kwa Kikwete, mimi nasema kuwa 2008 ni mwaka wa .... hata sina jina la kuuita kwa Kikwete.

Wameshachemsha maana Balali bado yuko hai na yuko tayari kutubu na kuomba msamaha. Network yetu inazidi kupanuka na kwa kweli hata kama si kesho au wiki ijayo lakini ni matter of days before tuwafikishe kwenye adhabu hawa wezi hatari kabisa kuwahi kushika serikali yetu.

Just wait for the tone............
 
Kikwete is the biggest joke Tanzanians had in Ikulu, period.

Bigger than even the much underappreciated "Ruksa"
 
Mwafrika welcome back na ahsante kwa makala yako!

Thanks kwa kila ulichoandika ila kubwa kuliko yote kumkumbusha JK kwamba sisi watanzania ndio mabosi wake kwani sidhani kama analimbuka hilo. Ninashawishika kwamba alijuwa hivyo kwamba sisi ndio mabosi wake wakati wa kampeni mpaka uchaguzi mpaka kuapishwa baada ya hapo sisi hatuna maana kwake zaidi ya washikaji wake wanaokula nao nchi. Otherwise angekuwa anakumbuka hilo asingekuwa anatutukana kila siku kwa usanii anaofanya KUWALINDA BILA KUCHOKA MAFISADI WENZIE KWA GHARAMA YA MAMILIONI YA WATANZANIA AKIWEMO MAMA MJAMZITO ANAYEKUFA KWA KUKOSA HUDUMA YA MATIBABU.Ila chonde chonde tunamsubiri kwa hamu hiyo 2010, akajifunze mapema kwa kibaka wa kenya namna ya kuiba kura.

Ahsante pia kwa kumtaja FISADI MKUBWA KULIKO WOTE NINAOWAFAHAMU ROSTAM. Hii nchi mimi nimeichoka kabisa kwa maagizo na lack of seriousness kwenye issues ambazo ni serious.Rostam ametajwa kwenye report ya CAG, sio E&Y wala Delloite kwamba amekula bilioni 3 kupitia makampuni yake fake. Cha ajabu hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa dhidi yake. Fisadi huyo bado ni mbunge na mengineyo mengi bado anafanya-jamani hii hali mpaka lini?
 
Mwafrika welcome back na ahsante kwa makala yako!

Thanks kwa kila ulichoandika ila kubwa kuliko yote kumkumbusha JK kwamba sisi watanzania ndio mabosi wake kwani sidhani kama analimbuka hilo. Ninashawishika kwamba alijuwa hivyo kwamba sisi ndio mabosi wake wakati wa kampeni mpaka uchaguzi mpaka kuapishwa baada ya hapo sisi hatuna maana kwake zaidi ya washikaji wake wanaokula nao nchi. Otherwise angekuwa anakumbuka hilo asingekuwa anatutukana kila siku kwa usanii anaofanya KUWALINDA BILA KUCHOKA MAFISADI WENZIE KWA GHARAMA YA MAMILIONI YA WATANZANIA AKIWEMO MAMA MJAMZITO ANAYEKUFA KWA KUKOSA HUDUMA YA MATIBABU.Ila chonde chonde tunamsubiri kwa hamu hiyo 2010, akajifunze mapema kwa kibaka wa kenya namna ya kuiba kura.

Ahsante pia kwa kumtaja FISADI MKUBWA KULIKO WOTE NINAOWAFAHAMU ROSTAM. Hii nchi mimi nimeichoka kabisa kwa maagizo na lack of seriousness kwenye issues ambazo ni serious.Rostam ametajwa kwenye report ya CAG, sio E&Y wala Delloite kwamba amekula bilioni 3 kupitia makampuni yake fake. Cha ajabu hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa dhidi yake. Fisadi huyo bado ni mbunge na mengineyo mengi bado anafanya-jamani hii hali mpaka lini?


Sidhani kama Kikwete anakumbuka kuwa ameajiriwa na wapiga kura in fact viongozi wengi Afrika hawakumbuki hili ndio maana wanatumia polisi na majeshi kuzuia haki za raia wenzao.

Kikwete hawezi kabisa kumtosa Rostam ingawa kila siku anazidi kutajwa kwenye kashfa kibao za wizi. This guy ni mkoloni na mbaguzi mkubwa kabisa. Alitumia magazeti yake ya habari corp wakati wa kampeni ya ccm ya 2005 kumchafua kabisa Salim Ahmed Salim kwa kumuita majina ya ajabu ya kibaguzi.

Amekuwa anatumia biashara zake na pesa zake kuwanunua waandishi wa habari ili kuchafua wapinzani wa Kikwete. Amesikika mara kwa mara akimtukana Jenerari majina ya kibaguzi kutokana na msimamo wa Ulimwengu wa kutonunuliwa kwa pesa za wizi. Rostam alisaidia sana kampeni ya Kikwete kwa vitenge na kofia za bure kwa wananchi ili Kikwete ashinde urais. Rostam ni mtu hatari, mwizi mwenye mawazo ya kikoloni na mtu anayetumika sana kumaliza upinzani nchini (hebu soma majira na mtanzania).

JF imeamua kuendeleza mapambano. Baadhi yetu tuko mbali kwa hiyo hawataweza kutumwagia tindikali kwa sasa na wakijaribu tu basi moto utawaka. Tutawashikia bango hadi tuchukue nchi yetu. Huu ni mwanzo tu!
 
Back
Top Bottom