Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,111
TANZANIA imetajwa kama nchi yenye uchumi unaokuwa kwa kasi barani Afrika. Katika taarifa yake ya hivi karibuni, Tanzania na hadithi ya mabadiko Afrika, Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limesema kuwa katika miongo miwili iliyopita, uchumi wa Tanzania umekuwa wa mafanikio. Mabadiliko ya uchumi huria na ya taasisi za umma yamesaidia kukuza pato la nchi kwa zaidi ya asilimia saba kwa mwaka, tangu mwaka 2000.
Hata hivyo, taarifa hiyo haiendani kabisa na hali halisi ya maisha ya wananchi. Mafanikio yanayotajwa yameshindwa kuondoa umasikini kwa wananchi huku maendeleo yakielekezwa zaidi kwenye miji mikubwa kama Dar es Salaam.
Ukuaji huo pia umekuwa chanzo cha kuongezeka kwa pengo kati ya masikini na matajiri, huku wananchi masikini wakiendelea kuwa masikini zaidi na matajiri kuendelea kutajirika. Tanzania pia imeshindwa kufikia Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini (Mkukuta) na ikipitwa na nchi nyingine Afrika na Asia.
Ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Policy Forum hivi karibuni, imetaja vipengele kadhaa ikionyesha kuwa ukuaji wa uchumi haujasaidia kupunguza umasikini.
Utafiti uliofanywa na Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), hauonyeshi kupungua kwa umasikini. Kati ya mwaka 2001 na 2007 sehemu ya watu masikini Tanzania ilipungua kidogo tu. Kupungua huko ni kudogo kiasi kwamba huwezi kusema kuwa umasikini umepungua au haukubadilika, inasema taarifa hiyo.
Inasema kwa kipindi cha miaka 16 kuanzia mwaka 1991 hadi 2007, umasikini umepungua kwa asilimia tano tu huku mabadiliko makubwa yakionekana Dar es Salaam wakati maeneo ya vijijini ukuaji wa uchumi ukiwa ni mdogo kiasi kwamba huwezi kuelezea kuwa umasikini umepungua.
Kipengele cha pili kinaonyesha kuwa umasikini umeongezeka kuliko ilivyokuwa mwaka 2001. Inasema wakati kiwango cha watu masikini wanaotumia chini ya Sh500 kwa siku kikipungua, idadi ya watu wanaoishi chini ya umasikini imeongezeka hadi kufikia 1.3 milioni kwa mwaka 2001, hasa kutokana na ongezeko la idadi ya watu nchini.
Umasikini unapimwaje?
Ripoti hiyo inasema kwa Tanzania, watu wanahesabika kuwa masikini wakati matumizi yao yanapokuwa chini ya mstari wa umasikini. Matumizi hayo yanahusisha bidhaa zote zinazonunuliwa na zile zinazozalishwa na kutumiwa nyumbani.
Bidhaa hizo ni kama vile, chakula, vifaa vya nyumbani, nguo, matunzo ya mtu binafsi, starehe, usafi, matumizi ya nyumbani, elimu, michango, mafuta na sabuni. Si matumizi yote yamehusishwa katika umasikini. Kwa mfano, afya, elimu na maji hayajahusishwa.
Mwaka 2001 kiwango cha umasikini kilikuwa ni Sh7,253 kwa mtu mmoja kwa siku 28. Kwa kuwa bei za bidhaa zimepanda kwa asilimia 93 tangu mwaka 2001 hadi 2007, kiwango cha umasikini ni Sh13,998, sawa na Sh500 kwa siku.
Kipengele cha cha tatu kinaonyesha kuwa, matajiri wanazidi kutajirika na masikini wanazidi kuwa masikini. Ripoti inasema kuwa siyo tu kwamba umasikini haukupungua tangu mwaka 2001, bali pia masikini wameendelea kuwa masikini.
Kipengele cha nchi kinabainisha kuwa Tanzania haipo katika mwelekeo wa kufikia Malengo ya Milenia na Mkukuta. Iliridhia Malengo ya Milenia ambayo yanaitaka kupunguza umasikini kutoka mwaka 1990 hadi 2015 kwa asilimia 50.
Ni wazi kuwa hadi mwaka 2000/1, Tanzania ilikuwa nje ya mwelekeo kwa asilimia 5.9. Kati ya mwaka 2001 hadi 2007 hali ikaendelea kuwa mbaya hadi ilipofikia asilimia 7.6. Malengo ya Mkukuta ambayo ni kufikia Malengo ya Milenia hadi mwaka 2010, hayajafikiwa.
Kipengele cha tano kinaonyesha kuwa Tanzania inatembea wakati nchi nyingine zikikimbia. Inaonyesha kuwa utendaji wake ni hafifu kulinganisha na nchi nyingine zinazoendelea ambazo sasa zimejikwamua kiuchumi. Nchi hizo ni pamoja na Ghana na Uganda kwa Afrika. Nyingine ni Vietnam na India kwa Asia.
Wakati Tanzania imepunguza umasikini kwa asilimia 2.4 kati ya mwaka 1991 na 2007, imeshuka ukilinganisha na Uganda, Ghana na Vietnam mara 10. India nayo imefanikiwa kupunguza umasikini kwa asilimia saba katika kipindi kifupi.
Kipengele cha sita kinaonyesha kuwa nusu ya Watanzania hawapati chakula cha kutosha. Moja ya Malengo ya Milenia ni kuondoa njaa.
Tangu mwaka 1991, Tanzania imetekeleza kwa sehemu ndogo malengo hayo kwa kupunguza utapiamlo kwa watoto.
Hata hivyo, takwimu zinaonyesha kuwa watoto wanne kati ya 10 wenye umri kati ya 0 hadi miezi 59, hawapati chakula cha kutosha.
Inaonyesha pia kwamba mtoto mmoja kati ya watano huwa na uzito mdogo. Utapiamlo husabaisha matatizo ya ukuaji wa watoto kwa asilimia 56 na matatizo ya akili kwa watoto kwa asilimia 13 nchini.
Inasema pia kwamba, asilimia 25 ya Watanzania hawapati lishe ya kutosha na wengi wao hufanya kazi nyepesi hasa za ofisini. Ni nusu tu ya idadi ya wananchi ambao hupata lishe ya kutosha kwa ajili ya kufanya kazi zao hasa za kutumia nguvu. Hata hivyo, inakisiwa kuwa kati ya watu wanaofanya kazi ngumu, wapo wasiopata lishe ya kutosha.
Ripoti hiyo inabainisha madhara yatokanayo na ukosefu wa lishe ya kutosha kuwa ni ukosefu wa madini ya chuma na vitamini A na madini joto. Hali hiyo husababisha kuzorota kwa nguvu kazi ya Taifa.
Kipengele cha saba kinabainisha kuwa watu wanamiliki rasilimali nyingi lakini haziwathaminishi. Ripoti inasema kuwa tangu mwaka 2001 umilikaji wa mali kama vile televisheni uliongezeka mara tatu wakati manunuzi ya vyandarua yaliongezeka mara mbili.
Bidhaa nyingine kama vile, radio, baiskeli na simu za mikononi zimeongezeka kwa kasi. Mwaka 2007, robo ya Watanzania walikuwa wakimiliki simu za mkononi.
Kwa mujibu wa Ofisi ya Takwimu ya Taifa, kuongezeka kwa manunuzi ya bidhaa kama hizo ni dalili ya kuboreka kwa hali za maisha ya watu igawaje, mabadiliko yake hayaridhishi.
Kulingana na kutobadilika kwa matumizi, thamani ya rasilimali zinazomilikiwa haijabadilika. Ukiondoa simu za mkononi, thamani ya bidhaa hupungua. Lakini simu hizo zinapoingizwa, thamani ya rasilimali zinazomilikiwa na wananchi huongezeka kwa asilimia tatu tu.
Kutokana na takwimu hizo, ripoti hiyo inabainisha kwamba, uboreshaji wa uchumi wa Tanzania umeshindwa kupunguza umasikini kwa watu wengi.
Watu wengi wanamiliki rasilimali, lakini inaonyesha kuwa Watanzania wengi wamekosa uwezo wa kujikimu kimaisha.
Kwa hali hii ni vigumu kusema kuwa mabadiliko ya uchumi Tanzania yameleta mafanikio. Changamoto hizo zinapaswa kuwa agenda za kisera na kisiasa, inasema ripoti hiyo.
Chanzo. Ripoti: Uchumi unakua, umasikini unaongezeka
Hata hivyo, taarifa hiyo haiendani kabisa na hali halisi ya maisha ya wananchi. Mafanikio yanayotajwa yameshindwa kuondoa umasikini kwa wananchi huku maendeleo yakielekezwa zaidi kwenye miji mikubwa kama Dar es Salaam.
Ukuaji huo pia umekuwa chanzo cha kuongezeka kwa pengo kati ya masikini na matajiri, huku wananchi masikini wakiendelea kuwa masikini zaidi na matajiri kuendelea kutajirika. Tanzania pia imeshindwa kufikia Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini (Mkukuta) na ikipitwa na nchi nyingine Afrika na Asia.
Ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Policy Forum hivi karibuni, imetaja vipengele kadhaa ikionyesha kuwa ukuaji wa uchumi haujasaidia kupunguza umasikini.
Utafiti uliofanywa na Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), hauonyeshi kupungua kwa umasikini. Kati ya mwaka 2001 na 2007 sehemu ya watu masikini Tanzania ilipungua kidogo tu. Kupungua huko ni kudogo kiasi kwamba huwezi kusema kuwa umasikini umepungua au haukubadilika, inasema taarifa hiyo.
Inasema kwa kipindi cha miaka 16 kuanzia mwaka 1991 hadi 2007, umasikini umepungua kwa asilimia tano tu huku mabadiliko makubwa yakionekana Dar es Salaam wakati maeneo ya vijijini ukuaji wa uchumi ukiwa ni mdogo kiasi kwamba huwezi kuelezea kuwa umasikini umepungua.
Kipengele cha pili kinaonyesha kuwa umasikini umeongezeka kuliko ilivyokuwa mwaka 2001. Inasema wakati kiwango cha watu masikini wanaotumia chini ya Sh500 kwa siku kikipungua, idadi ya watu wanaoishi chini ya umasikini imeongezeka hadi kufikia 1.3 milioni kwa mwaka 2001, hasa kutokana na ongezeko la idadi ya watu nchini.
Umasikini unapimwaje?
Ripoti hiyo inasema kwa Tanzania, watu wanahesabika kuwa masikini wakati matumizi yao yanapokuwa chini ya mstari wa umasikini. Matumizi hayo yanahusisha bidhaa zote zinazonunuliwa na zile zinazozalishwa na kutumiwa nyumbani.
Bidhaa hizo ni kama vile, chakula, vifaa vya nyumbani, nguo, matunzo ya mtu binafsi, starehe, usafi, matumizi ya nyumbani, elimu, michango, mafuta na sabuni. Si matumizi yote yamehusishwa katika umasikini. Kwa mfano, afya, elimu na maji hayajahusishwa.
Mwaka 2001 kiwango cha umasikini kilikuwa ni Sh7,253 kwa mtu mmoja kwa siku 28. Kwa kuwa bei za bidhaa zimepanda kwa asilimia 93 tangu mwaka 2001 hadi 2007, kiwango cha umasikini ni Sh13,998, sawa na Sh500 kwa siku.
Kipengele cha cha tatu kinaonyesha kuwa, matajiri wanazidi kutajirika na masikini wanazidi kuwa masikini. Ripoti inasema kuwa siyo tu kwamba umasikini haukupungua tangu mwaka 2001, bali pia masikini wameendelea kuwa masikini.
Kipengele cha nchi kinabainisha kuwa Tanzania haipo katika mwelekeo wa kufikia Malengo ya Milenia na Mkukuta. Iliridhia Malengo ya Milenia ambayo yanaitaka kupunguza umasikini kutoka mwaka 1990 hadi 2015 kwa asilimia 50.
Ni wazi kuwa hadi mwaka 2000/1, Tanzania ilikuwa nje ya mwelekeo kwa asilimia 5.9. Kati ya mwaka 2001 hadi 2007 hali ikaendelea kuwa mbaya hadi ilipofikia asilimia 7.6. Malengo ya Mkukuta ambayo ni kufikia Malengo ya Milenia hadi mwaka 2010, hayajafikiwa.
Kipengele cha tano kinaonyesha kuwa Tanzania inatembea wakati nchi nyingine zikikimbia. Inaonyesha kuwa utendaji wake ni hafifu kulinganisha na nchi nyingine zinazoendelea ambazo sasa zimejikwamua kiuchumi. Nchi hizo ni pamoja na Ghana na Uganda kwa Afrika. Nyingine ni Vietnam na India kwa Asia.
Wakati Tanzania imepunguza umasikini kwa asilimia 2.4 kati ya mwaka 1991 na 2007, imeshuka ukilinganisha na Uganda, Ghana na Vietnam mara 10. India nayo imefanikiwa kupunguza umasikini kwa asilimia saba katika kipindi kifupi.
Kipengele cha sita kinaonyesha kuwa nusu ya Watanzania hawapati chakula cha kutosha. Moja ya Malengo ya Milenia ni kuondoa njaa.
Tangu mwaka 1991, Tanzania imetekeleza kwa sehemu ndogo malengo hayo kwa kupunguza utapiamlo kwa watoto.
Hata hivyo, takwimu zinaonyesha kuwa watoto wanne kati ya 10 wenye umri kati ya 0 hadi miezi 59, hawapati chakula cha kutosha.
Inaonyesha pia kwamba mtoto mmoja kati ya watano huwa na uzito mdogo. Utapiamlo husabaisha matatizo ya ukuaji wa watoto kwa asilimia 56 na matatizo ya akili kwa watoto kwa asilimia 13 nchini.
Inasema pia kwamba, asilimia 25 ya Watanzania hawapati lishe ya kutosha na wengi wao hufanya kazi nyepesi hasa za ofisini. Ni nusu tu ya idadi ya wananchi ambao hupata lishe ya kutosha kwa ajili ya kufanya kazi zao hasa za kutumia nguvu. Hata hivyo, inakisiwa kuwa kati ya watu wanaofanya kazi ngumu, wapo wasiopata lishe ya kutosha.
Ripoti hiyo inabainisha madhara yatokanayo na ukosefu wa lishe ya kutosha kuwa ni ukosefu wa madini ya chuma na vitamini A na madini joto. Hali hiyo husababisha kuzorota kwa nguvu kazi ya Taifa.
Kipengele cha saba kinabainisha kuwa watu wanamiliki rasilimali nyingi lakini haziwathaminishi. Ripoti inasema kuwa tangu mwaka 2001 umilikaji wa mali kama vile televisheni uliongezeka mara tatu wakati manunuzi ya vyandarua yaliongezeka mara mbili.
Bidhaa nyingine kama vile, radio, baiskeli na simu za mikononi zimeongezeka kwa kasi. Mwaka 2007, robo ya Watanzania walikuwa wakimiliki simu za mkononi.
Kwa mujibu wa Ofisi ya Takwimu ya Taifa, kuongezeka kwa manunuzi ya bidhaa kama hizo ni dalili ya kuboreka kwa hali za maisha ya watu igawaje, mabadiliko yake hayaridhishi.
Kulingana na kutobadilika kwa matumizi, thamani ya rasilimali zinazomilikiwa haijabadilika. Ukiondoa simu za mkononi, thamani ya bidhaa hupungua. Lakini simu hizo zinapoingizwa, thamani ya rasilimali zinazomilikiwa na wananchi huongezeka kwa asilimia tatu tu.
Kutokana na takwimu hizo, ripoti hiyo inabainisha kwamba, uboreshaji wa uchumi wa Tanzania umeshindwa kupunguza umasikini kwa watu wengi.
Watu wengi wanamiliki rasilimali, lakini inaonyesha kuwa Watanzania wengi wamekosa uwezo wa kujikimu kimaisha.
Kwa hali hii ni vigumu kusema kuwa mabadiliko ya uchumi Tanzania yameleta mafanikio. Changamoto hizo zinapaswa kuwa agenda za kisera na kisiasa, inasema ripoti hiyo.
Chanzo. Ripoti: Uchumi unakua, umasikini unaongezeka