Ripoti iliyotuhumu Tanzania si rasmi-UN

Ng'wanza Madaso

JF-Expert Member
Oct 21, 2008
2,268
333
Ripoti iliyotuhumu Tanzania si rasmi-UN Thursday, 03 December 2009 07:01 Na Tumaini Makene

UMOJA wa Mataifa (UN) umetoa taarifa rasmi kuhusu ripoti inayoituhumu Tanzania kuwasaidia waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Congo (DRC) kuwa ililalamikiwa wakati haijachapishwa rasmi.

Pia umoja huo umejitenga na ripoti hiyo, ukieleza kuwa ilitolewa na jopo la wataalamu walioteuliwa na kupewa mamlaka ya kutafiti iwapo maamuzi ya kuviwekea vikwazo vikundi vya waasi vilivyoko DRC yanatekelezwa.

Taarifa ya UN iliyolifikia gazeti hili jana ilisema ripoti hiyo haipaswi kuhusishwa moja kwa moja na Sekretarieti ya UN wala mashirika yake yaliyopo nchini, bali ihusishwe na jopo hilo chini ya Mwenyekiti wa Kamati ya Vikwazo vya DRC, ambayo kwa sasa inaongozwa na Uturuki.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Afisa Habari wa UN, Bi. Usiah Ledama imekuja siku chache baada ya Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Bernard Membe kutoa tamko la kulaani ripoti hiyo kwamba ni ya uongo na kuitaka UN kuiomba radhi Tanzania.

Ufafanuzi huo wa UN unamaanisha kuwa Bw. Membe alilalamikia taarifa hiyo kabla ya kuchapishwa wala kujadiliwa na Baraza la Usalama la umoja huo, hivyo kuondoa uhalali wake.

Tayari Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimetoa tamko la kumkosoa Bw. Membe, kikimtaka kujibu hoja moja moja na kuwaacha waliotajwa katika taarifa hiyo kuwajibika badala ya 'kufunika kombe mwanaharamu apite'.

Hata hivyo, pamoja na UN kujitenga na ripoti hiyo, imesema baada ya kukamilika itajadiliwa na Baraza lake la Usalama.

"Kundi hilo wa wataalamu limekuwa likitoa taarifa mara kwa mara juu ya utafiti wao kuhusu masuala ya vikwazo vya silaha huko DRC, ripoti ya sasa ambayo imezua mjadala katika vyombo vya habari haijachapishwa wala kupitishwa rasmi, ingawa hatua hiyo itafanyika hivi karibuni.

"Kwa hiyo kikundi hicho cha wataalamu kimepewa mamlaka ya kufanya utafiti wa mara kwa mara na kutoa mapendekezo katika taarifa ambayo inajadiliwa na Kamati ya Vikwazo na Baraza la Usalama ambako kikundi hicho kinawajibika," ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo ya UN nchini huku ikiongezea kuwa wataalam hao wameongezewa muda wao wa kufanya kazi kwa mwaka mzima.

"UN inafanya kazi kama kitu kimoja kwa kujumisha idara, mifuko, mashirika, na mipango mbalimbali bado kuna umuhimu wa kutofautisha kati ya mihimili ya utendaji kama Baraza la Usalama na ile inayohusika na utekelezaji wa sera kama vile sekretarieti ya UN na mashirika yake yaliyoko nchini yakishirikiana na serikali katika shughuli za kimaendeleo," ilisema taarifa hiyo.


Source: Majira
 
Naona Mahiga na Migiro wana work magic zao UN !

Hapa kuna politics kibao zishaanza kuingia, Ban ki-moon mwenyewe ni suspect kama a Tanzania goon.
 
Ndo maana akina Mnyika et all, wasikurupuke. haya mambo ni mazito. All in all pia emage ya TZ inabdi tuilinde, sio tu kushangilia eti UN wametoa report basi na watanzania nao wako kipaumbele kuiunga mkono.........UN hawa au mataifa ya magharibi, wana destroy sana amani Africa, ni kuwa nao waangalifu sana, na si kuwa entertain au kuwashangilia.

Katika mambo haya bwanamdogo MNYIKA, maslahi ya taifa hayana chama. Jifunze hata marekani, walipompiga Saddam Hussein...Bush alipata kura kutoka republican na democrats. Hii inamaana USA walikubaliana wote kuilinda interest ya USA, na kuondoa uchama. Sasa wewe bwa mdogo MNYIKA katika swala hili pia maslahi ya TZ yalinde na uuondoe uo u CHADEMA.

Sawa?
 
Cha msingi hapa ni kwamba tujitahidi pale inapowezekana tuwe wasafi kama nchi. Na tusikubali wajanja wachache wapige deal kwa kutumia udhaifu au uzembe tulionao kama nchi. Tukikaa kimya siku mambo yakiharibika sifa mbaya zitakuja kwa nchi nzima. Tusaidiane kuwanyooshea vidole wahalifu kama wapo miongoni mwetu.
 
Kwa hiyo Membe alichofanya ni pre-emptive attack against the UN?
 
Ripoti iliyotuhumu Tanzania si rasmi-UN Thursday, 03 December 2009 07:01 Na Tumaini Makene

UMOJA wa Mataifa (UN) umetoa taarifa rasmi kuhusu ripoti inayoituhumu Tanzania kuwasaidia waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Congo (DRC) kuwa ililalamikiwa wakati haijachapishwa rasmi.

Pia umoja huo umejitenga na ripoti hiyo, ukieleza kuwa ilitolewa na jopo la wataalamu walioteuliwa na kupewa mamlaka ya kutafiti iwapo maamuzi ya kuviwekea vikwazo vikundi vya waasi vilivyoko DRC yanatekelezwa.

Taarifa ya UN iliyolifikia gazeti hili jana ilisema ripoti hiyo haipaswi kuhusishwa moja kwa moja na Sekretarieti ya UN wala mashirika yake yaliyopo nchini, bali ihusishwe na jopo hilo chini ya Mwenyekiti wa Kamati ya Vikwazo vya DRC, ambayo kwa sasa inaongozwa na Uturuki.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Afisa Habari wa UN, Bi. Usiah Ledama imekuja siku chache baada ya Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Bernard Membe kutoa tamko la kulaani ripoti hiyo kwamba ni ya uongo na kuitaka UN kuiomba radhi Tanzania.

Ufafanuzi huo wa UN unamaanisha kuwa Bw. Membe alilalamikia taarifa hiyo kabla ya kuchapishwa wala kujadiliwa na Baraza la Usalama la umoja huo, hivyo kuondoa uhalali wake.

Tayari Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimetoa tamko la kumkosoa Bw. Membe, kikimtaka kujibu hoja moja moja na kuwaacha waliotajwa katika taarifa hiyo kuwajibika badala ya 'kufunika kombe mwanaharamu apite'.

Hata hivyo, pamoja na UN kujitenga na ripoti hiyo, imesema baada ya kukamilika itajadiliwa na Baraza lake la Usalama.

"Kundi hilo wa wataalamu limekuwa likitoa taarifa mara kwa mara juu ya utafiti wao kuhusu masuala ya vikwazo vya silaha huko DRC, ripoti ya sasa ambayo imezua mjadala katika vyombo vya habari haijachapishwa wala kupitishwa rasmi, ingawa hatua hiyo itafanyika hivi karibuni.

"Kwa hiyo kikundi hicho cha wataalamu kimepewa mamlaka ya kufanya utafiti wa mara kwa mara na kutoa mapendekezo katika taarifa ambayo inajadiliwa na Kamati ya Vikwazo na Baraza la Usalama ambako kikundi hicho kinawajibika," ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo ya UN nchini huku ikiongezea kuwa wataalam hao wameongezewa muda wao wa kufanya kazi kwa mwaka mzima.

"UN inafanya kazi kama kitu kimoja kwa kujumisha idara, mifuko, mashirika, na mipango mbalimbali bado kuna umuhimu wa kutofautisha kati ya mihimili ya utendaji kama Baraza la Usalama na ile inayohusika na utekelezaji wa sera kama vile sekretarieti ya UN na mashirika yake yaliyoko nchini yakishirikiana na serikali katika shughuli za kimaendeleo," ilisema taarifa hiyo.


Source: Majira

UN, YALIYOMO KWENYE RIPOTI NI KWELI AU SIO KWELI??????? FULL STOP.

ikiwa ni kweli lakini sio rasmi na ikiwa ni kweli lakini rasmi kutakuwa na tofauti yoyote????? Wasitufanye mazoba hawa.
 
Back
Top Bottom