Mr. Tanganyika
Member
- Nov 13, 2010
- 91
- 7
Alhamisi tarehe 25 Oktoba, mapadri wa Consolata walikwenda baharini kumaliza siku huko Bagamoyo. Ilikuwa ni pale Stela Maris, hoteli mpya kabisa ya kanisa katoliki. Waliingia baharini kuogelea na kusahau taabu za kazi za kitume. Walipochoka waliamua kutoka majini ili warejee nyumbani. Mmoja wao hakuweza kutoka baharini. Huyu ni baba Salutaris Massawe, mkuu wa Consolata Fathers Tanzania. Alizolewa na mkondo wa maji na huo ukawa ndio mwisho wa maisha yake. Mwenzake alimuona jinsi alivyonyanyua mikono kuomba msaada lakini ilikuwa too late. Mwili wake ulipatikana Ijumaa tarehe 26 Oktoba saa tatu na nusu asubuhi. Mungu amuweke mahali pema peponi.