BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,032
- 3,944
Mkuu, tumeshaona pinda, lowassa, kikwete, lipumba, slaa na wengine wakivaa uchifu wanapotembelea, tena nadhani kwa jeykey huwa hata wanarecycle... these are ceremonial ni kama ambavyo unakwenda japan unapewa kimono na unapiga picha...
Unakumbuka JK alipigwa ngwala pale Mwanza akivishwa vazi la kichifu?? do you remember Nyerere alikua chieef wa makabila mangapi??
Cha maana ku-note ni kwamba Ridhwani amekua overpromoted sana na ccm yenyewe na hatujui agenda ni ipi kwani yeye wala si mwenyekiti wa vijana wa wa kamati ya ushindi
kinachonisikitisha zaidi ni promo anayopewa na baadhi ya waandhishi kuliko hata akina bilal au makamba, this will work against ridhwani (thats my concern)
...Mkuu Acid, nilishaanza kushituka kuwa ulikuwa huoni issue yoyotew kuhusu bwana mdogo kuvikwa uchifu. Bahati nzuri umeyatamka mwenyewe yanayochangia issue hii kuwa issue. nimeyapigia mstari.
Na kwa kuongezea tu, hao wote ambao umeishawataja kuwa wamevikwa uchifu ceremonial, unadhani Riz ametenda lipi ambao linaweza kumfanya awekwe kundi moja nalo kama sio tu kujigongagonga kwa hao wazee wa Kinyakusya ambao unaweza usiwalaumu sana kwa sababu wanakuwa wanatumiwa tu na watu wanaotaka kujiweka karibu na watawala??
Inanikumbusha picha ya gazeti la Mwananchi la wiki iliyopita ambapo inaonyesha wazee wa sehemu moja ya huko kusini wakiwa wameacha kazi zao za kujitafutia kula yao na badala yake kujipanga barabarani kumpokea 'mwana wa mfalme'!!
Hapa ndipo tulipofikishwa.
Kibaya zaidi tumeanza kuwa sugu na kuona kuwa sio issue. Poor We.